Posts

Showing posts from June 6, 2016

EVENTS

Image

MAKABURI MAJINI

Image
“Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua  katika  wafu”  (Kol.2:12). Katika ubatizo wa Biblia mtu anazikwa katika kaburi la maji na kutoka humo akiwa amefufuliwa kuishi maisha mapya katika Kristo kwa nguvu za Mungu, yaani, Roho Mtakatifu.  Hivyo ubatizo una maana yenye kina na ni zaidi ya kuzikwa tu ndani ya maji na kutoka.  Unawakilisha kifo, kuzikwa na kufufuka kwa Yesu Kristo. Paulo anafafanua kwa kusema, “Hamfahamu  ya  kuwa  sisi  sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi t ue ne nde  k ati k a  upy a  wa  uz i ma ” (Rum.6:4).  Wokovu wetu unategemea kifo na kuzikwa na kufufuka kwa Yesu Kristo. Kama hatua zote za awali zimechukuliwa, mtu anayebatizwa anatarajiwa kuendelea kuishi maisha mapya ya ushindi dhidi ya dhambi kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Ubatizo waweza kuwa ni kwa sababu