Posts

Showing posts from February 16, 2020

YALIYOMO KATIKA KITABU CHA MWANZO

1.     UTANGULIZI Kitabu cha Mwanzo ni miongoni mwa Vitabu vitano vya Musa ( Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati ). Hapo awali kabisa, vitabu hivi vitano vya Musa vilikuwa kitabu kimoja, na baadaye kilitenganishwa na kuwa vitabu vitano kama tulivyo navyo siku hizi katika Biblia. Kwa ujumla, vitabu hivi vitano vinajulikana kwa jina la Pentatuki (maana yake, vitabu vitano).   Jina hili la Pentatuki linatokana na maneno mawili ya Kiyunani (Kigiriki), yaani “penta” maana yake ‘tano’ na “teuchos” maana yake ‘kitabu’ . Waebrania walimanisha Pentatuki yote ni “sheria” au “torati” (2Nyakati 17:9; Nehemia 8:14, 18; Mathayo 5:17; Mathayo 11:13; Mathayo 12:5; Luka 24:44). Majina ya vitabu hivyo katika tafsiri ya kale ya Kiyunani ya Septuaginta yalikuwa Genesis kwa kitabu cha Mwanzo, Exodus kwa kitabu cha Kutoka, Leviticus kwa kitabu cha Walawi, Numeri kwa kitabu cha Hesabu na Deuteronomium kwa kitabu cha Kumbukumbu la Torati. Mapokeo ya Kiebra