Posts

HATARI KWA LAODIKIA

BY: MWL. FRANK PHILEMON. Fungu : Ufunuo 3:15-16   A.    UTANGULIZI JUU YA LAODIKIA Laodikia ni mji ambao umetajwa katika maandiko matakatifu na umekuwepo kati ya mwaka 261BC na 253BC . Kama vile Kolosai na Hilapoli, mji huu ulikuwa katika bonde la rutuba upande wa mashariki mwa mji wa Efeso (Ufunuo 3:14). Baina ya Efeso na Laodikia, palikuwa na umbali takribani maili 40 hivi.  Hapo awali mji wa Laodikia ulikuwa ukiitwa Diospolis baade Rhoas na hatimae Laodicea ambalo ni jina la mke wa mfalme Antiochus II wa Syria ambaye alihusika katika kuujenga mji huo.  Mfalme Antiochus II aliuita mji huu jina la mke wake kama heshima ya pekee kwa mke wake aliyeitwa Laodice. Laodikia ulikuwa ni mji muhimu, uliokuwa na mwingiliano wa watu wengi na uliochangamka sana katika Asia Minor . Na ulikuwa kituo kikubwa cha biashara na huduma za kibenki, kwani mji huu ulikuwa katikati ya miji mingine. Mji wa Laodikia ulikuwa pia mashuhuri katika utengenezaji wa nguo zitokanazo

FALSAFA YA MUNGU KATIKA NDOA

Fungu: Wimbo Uliobora 5:16 “Kinywa chake kimejaa maneneo matamu, Ndiye mzuri sana pia. Ni huyu mpendwa wangu, Ni huyu rafiki yangu , Enyi binti za Yerusalemu” 01: UTANGULIZI Ufafanuzi wa fungu kuu: Fungu kuu limebeba mkitadha wa mambo makuu matano (5) yafuatayo: 1.      Maneno ya hekima, busara, staha, faraja, upendo, shime na kutia moyo. 2.      Msistizo juu ya uzuri: 1. tabia na mwenendo, 2. umbo na muonekano, 3. usafi na unadhifu. 3.      Upendo usiokuwa na chembe ya ubinafsi. 4.      Uwazi na ukweli. 5.      Urafiki miongoni mwa wapendanao. Ombi: 02: KIINI CHA SOMO Sambamba na hivyo vipengele vitano (5) juu ya muktadha mzima wa fungu letu kuu (Wimbo Uliobora 5:16), leo tutaangalia kwa kina kipengele kimoja tu kinachohusu, urafiki miongoni mwa wanandoa (wapendanao). “Ili Mkristo ye yote aweze kuifikia ndoa lazima aanze na hatua mama mbili, ambazo ni urafiki na uchumba .    Bila hatua hizo mama, itakuwa ni ndoa iliyotokana na utashi wa watu