HATARI KWA LAODIKIA



BY: MWL. FRANK PHILEMON.
Fungu: Ufunuo 3:15-16  

A.   UTANGULIZI JUU YA LAODIKIA
Laodikia ni mji ambao umetajwa katika maandiko matakatifu na umekuwepo kati ya mwaka 261BC na 253BC. Kama vile Kolosai na Hilapoli, mji huu ulikuwa katika bonde la rutuba upande wa mashariki mwa mji wa Efeso (Ufunuo 3:14). Baina ya Efeso na Laodikia, palikuwa na umbali takribani maili 40 hivi.

 Hapo awali mji wa Laodikia ulikuwa ukiitwa Diospolis baade Rhoas na hatimae Laodicea ambalo ni jina la mke wa mfalme Antiochus II wa Syria ambaye alihusika katika kuujenga mji huo.  Mfalme Antiochus II aliuita mji huu jina la mke wake kama heshima ya pekee kwa mke wake aliyeitwa Laodice.

Laodikia ulikuwa ni mji muhimu, uliokuwa na mwingiliano wa watu wengi na uliochangamka sana katika Asia Minor. Na ulikuwa kituo kikubwa cha biashara na huduma za kibenki, kwani mji huu ulikuwa katikati ya miji mingine. Mji wa Laodikia ulikuwa pia mashuhuri katika utengenezaji wa nguo zitokanazo na nyuzi za mazao ya miti pamoja na manyoya ya kondoo.

Laodkia ulikuwa imebobea katika masuala ya elimu ya tiba pamoja na utengenezaji wa dawa za tiba; hivyo Laodikia ilikuwa ina shule kwa ajili ya kuandaa wajuzi na watalaamu wa mambo ya tiba na dawa.

Mji wa Laodikia ulikuja kuwa sehemu ya utawala wa Pargamo, na mnamo mwaka 133BC ulitwaliwa na utawala wa Kirumi (Roman empire).  Na Cicero akiwa kama msemaji na gavana wa kirumi aliifanya Laodikia kuwa makazi makuu ya jimbo alilokuwa akilitawala.

Wakazi wa Laodikia walikuwa na jeuri na kiburi cha mali na utajili; mfano, mnamo mwaka wa 60 AD mji wa Laodikia ulipatwa na janga la tetemeko la ardhi ambapo mji huu uliharibiwa vibaya; kwa sababu ya mali na utajiri walionao wakazi wa mji huu walikataa msaada kutoka serikali ya Kirumi iliyokuwa ikitawala ili kufanikisha kuujenga upya tena mji huo.

Mji wa Laodikia ulikuwa na chemchemu ya maji moto mahali palipoitwa hierapelis mile 6 karibia na bonde la mto Lycus kwa upande wa kusini, ambapo pia maji yaliyokuwa yakitililika yalijengelewa mifereji iliyofunikwa kwa mawe na maji hayo pia yalitoka kupitia pipe zilizoegeshwa kwenye chanzo cha maji moto hayo.

Maji moto yaliyokuwa yakitoka yalikuwa na kiasi kingi cha madini ya calcium hivyo mara nyingi pipe zilikuwa zikiziba. Aidha, bonde la mto Lycus na bonde la mto Kolosae kwa pamoja yalitumika kama njia za usafiri wa majini.

Wakazi wa mji wa Laodikia walikuwa na imani zao za kipagani. Kama ilivyokuwa kwa miji mingine. Mji huu (Laodikia) ulijulikana kama The City of Zeus yaani mji wa baba wa miungu, wanadamu, watawala na walinzi wa vyote.  Baadae Laodikia ulikuja ukawa mji mkubwa uliokaliwa na Wakristo baada ya kufikishiwa injili kipindi cha mitume wa Yesu (angalia Wakolosai 2:1, 4:15 na Ufunuo 1:11).

Wenyeji wa Laodikia kwa jumla walifanikiwa kwa namna nyingi nao waliridhika na hali yao, na tabia hiyo ya kuridhika na hali iliingia hata katika kanisa, hivyo hawakuweza kuonesha kwamba Kristo ndiye anayeridhisha kabisa. Hawakutambua kwamba Kristo peke yake angeweza kujenga tabia za kweli za kiroho maishani mwao, hasa kwa kutubu dhambi zao na kutafuta msaada wake kwa unyenyekevu (Ufunuo 3:15-22).

Ingawa Paulo alikuwa mtu wa kwanza kupeleka injili Asia, hakuna fununu kwamba alitembelea mji huo wakati wa safari zake kuu za kueneza injili kama tunavyosoma katika Matendo ya Mitume (Wakolosai 2:1).  Labda kanisa la huko lilianzishwa wakati wa Paulo alipoishi Efeso  kwa muda mrefu, yaani wakati wa safari yake kuu ya tatu baada ya waamini wa Efeso kuipeleka injili kwa miji jirani na Efeso (Matendo 19:8-10; Wakolosai4:12-130.

Paulo alipoandika barua kwa kanisa la Kolosai, vilevile aliliandikia kanisa la Laodikia. Alitaka makanisa hayo mawili yabadilishane barua zao, ili yote mawili yaweze kusoma barua zote mbili  (Wakolosai 4:16). Hivyo, barua ya Walaodikia haikuingizwa katika mkusanyo wa Maandiko Matakatifu (imepotea).

Barua nyingine kwa kanisa la Laodikia ilihifadhiwa. Barua hiyo iliandikwa karibu na mwisho wa karne ya kwanza (Ufunuo3:14). Ni barua yenye ujumbe wa Kristo kwa kanisa nayo I namaneno mengi ya kuonya na kukemea kanisa. 

Kipindi cha utawala wa Kirumi; Proconsular Asia lilikuwa ni jimbo, ambapo mji wa Efeso ulikuwa mji mkuu hapo awali (soma Matendo 2:9; 6:9; 16:6; 19:10, 22; 20:4, 16, 18 n.k) na baade Asia Minor ulikuja ukawa mji mkuu (soma Matendo 19:26, 27; 21:27; 24:18;27:2). Jimbo la Proconsular Asia lilikuwa na makanisa saba yaliyooneshwa katika unabii aliooneshwa Yohana (angalia Ufunuo1:11).

Viongozi (ambao ni machifu) walikuwa ni wenye mali nyingi, na matajiri pia ambao walichaguliwa kila mwaka ili kuongoza vikao, michezo, sherehe na shughuli mbalimbali za kidini katika maeneo waliyosimamia. Biblia inathibitisha kuwa; Miongoni mwa machifu au viongozi wengine walikuwa rafiki zake Paulo (Matendo 19:31).

Kwa sasa eneo la mji huu ni sehemu yenye jangwa linaloitwa “The Turks Eskhissar au Old castle”. Asia minor ambapo ulikuwepo mji  huu kwa sasa panaitwa Uturuki (yaani nchi ya Uturuki).

Asia-minor (Uturuki) inakumbukwa hadi leo hii kwa matukio makuu mawili:
(a)  Palikuwa ni mahali ambapo serikali ya Rumi ilipatenga kuwa makao makuu ya nchi za mashariki kulingana na hali hiyo pakaitwa Laodikia yaani hukumu.
(b) Ndipo pale agizo la maaskofu wote lilipotolewa mnamo mwaka 364AD juu ya badiliko la sabato lililotolewa na Baraza la Laodikia.

B.   UWASILISHAJI WA HUBIRI JUU YA LAODIKIA
Laodikia ni kanisa la mwisho katika mpangilio wa makanisa saba yaliyotajwa katika Ufunuo 1:11. Mpangilio wa haya makanisa saba unaakisi nyakati katika unabii na utimilifu wake kama ifuatavyo:

1.     Kanisa la Efeso (33 – 100 AD)
(a)  Ni kanisa safi, sawa na farasi mweupe
(b) Lilikuwa na upendo uliopoa (Ufunuo 2:4)

2.     Kanisa la Smirna (100 – 313 AD)
(a)  Ni kanisa la mateso, sawa na farasi mwekundu (Ufunuo 2:10)

3.     Kanisa la Pergamo (313 – 538 AD)
(a)  Ni kipindi ambacho mfalme Constantine anachanganya giza na Nuru
(b) Ndipo kipindi ambacho ibada ya Jumapili ilianzishwa rasmi
(c)  Kanisa lenye upagani, sawa na farasi mweusi (Ufunuo 2:14-15)

4.     Thiatira (538 – 1517 AD)
(a)  Kanisa lenye mchanganyiko wa nuru na giza sawa na farasi wa kijivu (Ufunuo 2:20)

5.     Sard (1517 – 1798 AD)
(a)  Kanisa katika kipindi cha matengenezo (Ufunuo 3:2)

6.     Filadefia (1798 – 1844)
(a)  Kanisa katika kipindi cha mapumziko ya mateso (baada ya mateso kuisha)
(b) Kanisa linalotunza neno (Ufunuo 3:8)

7.     Laodikia (1844 – kuendelea)
(a)  Kanisa la mwisho (Kanisa la masalia)
(b) Waumini wake sio wakamilifu
(c)  Kanisa la hukumu ya mwisho
(d) Kanisa vuguvugu (Ufunuo 3:15).

C.   SIFA ZA LAODIKIA NA HATARI KWA WASHIRIKI WAKE
Kanisa la Ladikia halitaharibiwa kwa sababu siyo kamilifu (bali litatapikwa). Zifatazo ni sifa za Kanisa la Mungu la Laodikia na hatima kwa mstakabali wa washiriki wake:
1.     Kufanana na ulimwengu - Vuguvugu (Ufunuo 3:15 – 16)
2.     Maombi duni (Ezekieli 9:4)
3.     Kutosoma neno (Ufunuo 3:17)
4.     Kuridhika na hari mbovu za kiroho (Ufunuo 3:17; Isaya 55:1-2). Kuchanganya mambo ya kidunia na mambo ya kiroho na kuhifadhi dhambi na kupuuzia mambo ya kiroho
5.     Umasikini wa maandiko (Ufunuo 3:17-18; Marko 4:18-19)
6.     Uchi wa matendo yasiyotengenezwa (Ufunuo 3:17). Kupenda matendo maovu. Matengenezo duni ya kiroho, matendo na vyakula
7.     Kanisa la Laodikia na washiriki wake wamejikita katika kutafuta umaarufu wa mali – Bwana anatutaka tununue dhahabu safi itokayo kwake ili tuwe matajiri wa mambo ya kimbingu.
8.     Kanisa la Laodikia na washiriki wake wamejikita katika kutafuta umaarufu wa mavazi ya kidunia – Bwana anasema tununue mavazi safi na meupe yatakayohifadhi uchi na aibu za matendo yetu.
9.     Kanisa la Laodikia na washiriki wake wamejikita katika kutafuta tiba za macho katika mambo ya kidunia – lakini Yeye Bwana anasema tununue kwake dawa ya kujipaka macho yetu ili tupate kuona mambo ya kiroho. (Ufunuo 3:18)
10.                         Bwana Yesu anatualika tule naye chakula cha jioni (Ufunuo 3:19-20). Neno lililotumika hapa ni “Dine” au “sup” ni sawa na “Deipon” (mlowa jioni): ambapo katika Kigiriki kuna milo mitatu: Akratisma (Breakfast), Ariston (Lunch) na Deipon (dinner). na mlo wa msingi ni wa jiosni


D.   HITIMISHO - WITO
Bwana huwarudi: Ufunuo 3:19; Waebrania 12:6.
Neema iokoayo imefunuliwa: Tito 2:11 – 15.

Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU