SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU


FUNGU KUU: (Mwanzo 6:6-8). “BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. BWANA akasema, nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitaambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi kwamba nimewafanya. Lakini Nuhu akapata neema machoni pa Bwana”

UTANGULIZI:
Katika somo hili “Madhara ya kukataa Kumtii Mungu” limehusisha kitabu kilicho andikwa na Musa hususani sura ya 3, sura ya 4, sura ya 5, sura ya 6 na ile sura ya 7. Katika sura hizi kunamambo makubwa ya kujifunza ili yatujenge katika safari yetu ya wokovu. Tutaona jinsi gani anguko la mwanadamu linavyotokea kwa sababu tu ya kukataa kumtii Mungu pamoja na madhara yake. Katika sura hizo zote; visa vyake vimefupishwa mno katika biblia, hivyo wengi huwa wanashindwa kuelewa mambo mengi na yamsingi.

KIINI CHA SOMO:
1. Dhambi iliingia duniani kwa sababu Adamu na Hawa hawakuweza kutii taratibu na sheria za Mungu (Mwanzo 3:1-3). Ukisoma kwa umakini katika Mwanzo 3:3 Hawa alijua ni kosa kwa kuwa yeye na Adamu walikuwa wameonywa na kufundishwa madhara yake, ndiyo maana Hawa ananukuu kauli ya Mungu anapojibishana na nyoka (Shetani) ….. Mungu amesema “msiyale wala msiyaguse, msije mkafa” (Hawa ananukuu kauli ya Mungu)

2. Shetani anamchanganyia uongo na ukweli hawa ili kumpotosha na kumwaminisha kuwa maelelekezo ya Mungu hakuyaelewa vizuri (Mwanzo 3: 4)
3. Shauku ya hawa ya kujua maarifa (mema na mabaya) pamoja na kuutamani kutoka mchoni; Hawa anachukua jukumu la kuchuma matunda katika ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya, kisha anakula na kumpelekea Adam mumewe. (Mwanzo 3:6)
4. Kwa makosa waliyotenda Hawa na Adamu wanajificha uso wa Bwana (Mwazo 3:8) ili asiweze kuwaona.
5. Kutupiana lawama kunaanza; Adamu anamtupia lawama Hawa, Hawa anamtupia lawama Nyoka (Mwanzo 3:12).
6. Mungu mwenye huruma anapanga mpango wa wokovu katika anguko la mwanadamu (Mwanzo 3:15).
7. Kwa mala ya kwanza mnyama anachinjwa ili kutengeneza nguo za ngozi kustili miili yao (Mwanzo 3:21).
8. Mungu anawafukuza Hawa na Adamu kutoka nje ya Bustani ya Edeni ili kupusha kula tena matunda ya ujuzi wa mema na mabaya ili asije kuishi milele katika dhambi (Mwanzo 3:22-24).
9. Watoto wawili wanazaliwa ‘Kaini, Habili’ (Mwanzo 4:1). Kaini mtoto wa kwanza (Mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani) na mkulima. Habili mtoto wa pili na mfugaji wa kondoo. Katika biblia habili kama mtoto wa pili ametajwa tu kwa makusudi makuu kama mfia dini.
10. Makundi mawili ya ibada ya kweli na ya uongo yanajitokeza baina ya Kaini na Abili (Mwanzo 4:3-5).
11. Mungu anamuonya Kaini kutokana na kukengeuka kwake (Mwanzo 4:6-7).
12. Kaini anamuua mdogo wake Habili kwa sababu ya wivu wa kiibada (Mwanzo 4:8).
13. Kutomsikiliza Mungu, Kaini banakuwa jeuli hata katika majibu yake (Mwanzo 4:9).
14. Mungu anampatia Kaini laana kuwa mbali na uzao wa familia ya watakatifu (Mwanzo 4:10-16).
Ufanano wa kaini na Habili na Kaini:
*    Wote walifundishwa na wazazi wao jinsi ya utoaji wa sadaka katika ibada zao kwa Mungu
*    Wote walitengeneza madhabahu kwa ajili ya kutoa sadaka zao kwa Mungu
*    Wote walisimama kama wafanya ibada mbele za Mungu wa Mbinguni.
Utofauti wa Kaini na Habili:
*    Kaini alikengeuka na kufanya matakwa yake badala ya yale ya Mungu katika ibada
*    Habili alienenda katika taratibu na sheria za Mungu katika ibada na utoaji wa sadaka
*    Kaini anawakilisha kanisa/mtu asiyefuata taratibu alizoziweka Mungu
*    Habili anasimama kama kanisa au mtu ambaye ni mtiifu na mfuata taratibu na sheria za Mungu
Fundisho kutoka kwa kaini na Habili:
*    Habili ni mfia dini
*    Mungu haangalii matukio au matendo yako ya nyuma ili akuhesabie haki na kufuta makosa ya hivi karibuni
*    Mungu anaangalia katika utii wa kufuata taratibu na maagizo yake
*    Mungu anapokea ibada zetu, endapo tutaenenda kwa utaratibu na utii juu yake
*    Dini, madhehebu na watu watungao ibada zao wenyewe zisizompendeza Mungu, kwa Mungu hazipokelewi
*    Kabla ya kumwendea Mungu, yatupasa kujua kuwa ni kitu gani kitasababisha ibada zetu zisipokelewe na Mungu
*    Tunapofanya makosa katika ibada zetu na Mungu asitujibu haitupasi kushupaza shingo kama Kaini hatimae tukapotea milele
*    Siku zote yatupasa kujitahidi ili ibada zetu ziweze kupokelewa na Mungu.
*    Mtu asiyetii juu ya sheria na maonyo; Mungu huongeza laana badala ya Baraka, hivyo mkono wa Mungu huondoka juu yake.

KAZIO LA MAARIFA
Hawa na Adamu wanapoteza watoto wao wote wawili; mmoja kuwa mtangatangaji na mwingine kwa kufa kifo.  Hivyo hapakuwa na yeyote aliyemlithi wa haki ipatikanayo kwa imani. Kumbuka hata Habeli kutajwa ni kwa sababu ya kuifia dini.
Kaini alikuwa anamke toka mwanzo hata kabla ya kulaaniwa. Na kipindi hicho walioana ndugu (hivyo Kaini alikuwa ameoa dada yeke maana kwa kipindi hicho hapakuwa na jamii nyingine tofauti na jamii ya familia ya Hawa na Adamu).

Mtoto wa kwanza wa Kaini ni Henoko (Mwanza 4:17) Adamu naye alizaa watoto wengine tofauti ya wale wawili. Uzao wa kaini na uzao wa Adamu ulitengeneza makundi mawili:

*    Uzao au ukoo mtakatifu mrithi wake ni Sethi
*    Uzao au ukoo wa wana wa wanadam mrithi wake ni Henoko
Kuna Henoko pia kutoka ukoo mtakatifu tofauti na Yule mtoto wa Kaini (Mwanzo 5:18) na huyu alitwaliwa (Mwanzo 5:24). Henoko huyu kabla ya kutwaliwa alimzaa Methusela aliyeishi miaka 969 (METHUSELAH “Muth” and “Shalach” = “His death shall bring judgment). Methusela alimzaa Lameki na Lameki alimzaa Nuhu.        Ikumbukwe kuwa yupo pia Lameki upande wa ukoo wa kaini ambaye ni mwanzilishi wa kuoa mke zaidi ya mmoja. (Mwanzo 4:19)
Mchangamano na mwingiliano kati ya wana wa Mungu na wana wa wanadamu uliathiri sana mwenendo mzima wa ulimwengu na kuongezeka maovu kwa kasi kubwa kwa pande zote. Kwa sehemu kubwa Mwanzo sura ya sita (6) inazungumzia ongezeko la watu ulimwenguni kwa kipindi hicho. Mwingiliano uliotokana na kuoleana kwa pande mbili hizo kulisababisha kuongezeka kwa maovu na uovu kuongezeka sana.
                                                                                                                 Upande wa wana wa wanadamu palizaliwa watoto wengi bila mpangilio na wengi wakiwa watoto wa kike. Pia upande huu palikuwa na kuoana katika umri mdogo pamoja na uoanaji usiokuwa na mpangilio hasa kuoa wanawake wengi. Upande wa wana wa wanadamu palizaliwa watoto waliokuwa wazuri mno wa sura, hivyo kuvutia na kupelekea watoto wa kiume kutoka upande wa wana wa Mungu au ukoo mtakatifu kwenda kuoa mabinti kutoka upande wa wana wa wanadamu (Mwanzo 6:1-2). Kuoleana kwa pande hizo mbili, kulisababisha kuzaliwa kwa vizazi vyenye watu hodari wenye sifa (za ajabu) na majitu au Manefili (Mwanzo 6:4)
Maovu yalipo enea kutokana na kuingiliana kwa pande zote mbili, Mungu alipanga mpango wa wokovu kwa wanadamu, na kwa kindi hicho Nuhu ndiye aliyepata neema machoni pa Mungu (Mwanzo 6:5-8). Pia kutokana uovu ulipozidi katika dunia, Mungu alipunguza umri wa wanadamu kuishi miaka mingi (Mwanzo 6:3)
Nuhu alihubiri injili kwa miaka 120, hatimae gharika ikaja na wengi wao waliangamia kwa kutotii ujumbe wa Mungu. kutokana na tukio la kuigharikisha dunia, watafiti na wataalamu wengi wa masuala ya miamba na mafuta wanaamini kuwa huenda miaka ya nyuma palitoke vifo vya viumbe hai vingi ndiyo maana kunakuwepo na mafuta, gesi, makaa ya mawe na chokaa na kurejea jambo la gharika kutoka katika biblia.

NASAHA:
*    Wokovu ni wa mtu binafsi wala sio wa kirafiki au kundi
*    Tusikilize maonyo ya Mungu na tufanye toba za kweli
*    Mungu katupa nafasi nyingine kama kipindi cha Nuhu ili tuokolewe
*    Tusifungiwe mlango wa rehema kwa kukataa maonyo, wito na sauti ya Mungu
*    Wapo waliokuwa karibu na Nuhu na Kumsaidia kutengeneza safina ili hali kumbe nao walikuwa wasindikizaji (ndivyo hivyo kwetu sisi)
*    Dhambi ya kaini ilipelekea ulimwengu kuangamizwa kwa gharika, vivyohivyo dhambi zetu zaweza kupelekea wengine kuangamizwa katika ziwa la moto.
*    Kuoleana na wana wa wanadamu kunapeleke kuzaa watoto wengi wasiokuwa imara katika imani na kumjua Mungu vyema.
*    Tujitahidi  kuwa na NEEMA Machoni pa MUUNGU. Mwanzo 6:6-8. “BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. BWANA akasema, nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitaambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi kwamba nimewafanya. Lakini Nuhu akapata neema machoni pa Bwana”  

HITIMISHO:
Hatari ya kukataa kutii kwa wanadam, imesababisha gharama kubwa sana kwa Mungu ili kuunusulu upotevu wa mwanadam. Mkakati wa ukombozi kwa wanadamu anaubeba Yesu Kristo aliyemwana na Mwokozi wetu.

                           BWANA ATUTETE                           
 Mwl. Frank Philemon

Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI