MFANO WA MPANGO KAZI

KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO LIWALE

MPANGO KAZI WA OFISI YA MAKATIBU/MAKARANI WA KANISA (2015/2016)



UTANGULIZI.
Idara/ofisi ya karani/katibu ni idara nyeti ambayo inaunganisha shughuli zote za kanisa. Kutokana na wengi wa wahiriki na viongozi wa kanisa au makarani/makatibu wenyewe kutoipa kipaumbele idara hii ni kwa sababu ya kutojua uthamani wake katika ukamilifu wa safari yetu ya kwenda mbinguni. Kazi ya ukarani imeanza toka enzi za kale, ambapo hadi sasa tunapata takwimu, kumbukumbu na taarifa sahihi kwenye biblia (Mfano; Kutoka 1:1-5 n.k.).

Bila huduma za kiukarani biblia ingekuwa kitabu kisichojithibitisa maana kingejichanganya kwa kukosa kumbukumbu. Mambo mengi yameandikwa juu ya umuhimu wa kuweka mpango kwa kila jambo afanyalo mtu. Kanisa hali kadhalika lina wajibu wa kujua madhumuni ya uwepo wake pamoja na mazingira yanayolizunguka kwa kuzingatia umuhimu wake kama inavyosisitizwa katika maandiko matakatifu; kuwahubiri mataifa habari njema ya wokovu wa Bwana YESU, ili wamjue; Na kuwavua watu. Luka 5: 1-11.  
Aidha kanisa lina wajibu wa kutoa huduma mbalimbali za kijamii kama afya, elimu na kisha kutoa taarifa na takwimu juu ya waliopatiwa huduma hizo. Ofisi ya makatibu wa kanisa iliona umuhimu wa kupanga ili kuweza kutimiza malengo yake ya muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu. Maandiko Matakatifu yanasisitiza umuhimu wa kupanga kabla ya kuanza utekelezaji. Kupanga kunaokoa wakati, kunarahisisha mambo na pia kuepusha migongano na muingiliano wakati wa utekelezaji.





DHUMUNI LA MPANGO KAZI.
Dhumuni la mpango kazi huu ni kubainisha njia sahihi na rasilimali zinazohitajika ili kuweza kutambua, kubaini takwimu na taarifa sahihi za idara na washiriki katika kanisa ili kulijenga kanisa katika misingi ya mitume na manabii kama walivyotoa taarifa sahihi, na takwimu sahihi kwa zama zile.

DIRA                                                                                                                                             “Idara/ofisi yenye kutambua na kufahamu takwimu sahihi za washiki wa kanisa na kuratibu utekerezaji wa idara zote za kanisa na kuhifadhi kumbukumbu zote za kanisa”
DHAMIRA
“Ofisi/idara kuwa na utaratibu wa kutunza kumbukumbu na kutoa taarifa, kuandaa vikao, kusimamia na kuratibu vikao vyote vya baraza na mikutano mikuu ya kanisa”.

KAULI MBIU
Hati safi kwa utendaji mzuri wa kazi yeenye Kiango”

TUNU.
*      Kuwa na mifumo mizuri na ya kisasa na taratibu nzuri za kutunza kumbukumbu za kanisa.  




MALENGO.
Kutokana na uhitaji wa utendaji kazi mzuri, idara/ofisi imekusudia kutekeleza malengo yafuatayo:
*      Kuandaa na kusimamia kikamilifu kalenda za vikao vya mabaraza na mikutano mikuu ya kanisa.
*      Kutoa na kuweka wazi taarifa zote za kanisa na washiriki wa kanisa wanapotoka na kuingia.
*      Kuhakikisha ufuatiliaji wa ushirika kwa kila mgeni ajaye na kukaa kwa muda mrefu sambamba na kutoa elimu juu ya umuhimu wa kuwa na ushirika katika kanisa mahalia
*      Kujenga uhusiano mzuri na idara zingine za kanisani katika kupokea na kutoa taarifa mbalimbali zinazohitajika
*      Kuandaa na kutengeneza benki ya takwimu sahihi za kanisa na idara zote za kanisa.
*      Kusimamia vyema taratibu na kanuni za kanisa kama zilivyo kwenye muongozo wa kanisa.

UTEKELEZAJI

s/n
Malengo
Mikakati
Mhusika
Muda wa utekelezaji
Matokeo
01
Kuandaa na kusimamia kalenda za vikao
Kuandaa ratiba na kutoa tarifa kwa vikao vyote
Frank Philemon
Ifikapo mwezi wa 3 kuwe na karenda/ratiba ya vikao vyote vinavyotakiwa kufanyika
Vikao vilivyo katika mpangilio maalumu
02
Kutoa na kuweka wazi taarifa kanisa za washiriki wake
Kila wiki ya kwanza ya robo ya mwaka kutoa taarifa juu ya ukuaji wa kanisa na maendeleo yake.
Anitha thobias
Mara nne kwa mwaka
Kujua tahimini ya ukuaji na maendeleo ya kanisa
03
Kuhakikisha kila mwadventista mgeni awe na ushirika endapo atakaa kwa muda mrefu
Kutambua wageni wote kwenye siku za ibada
Makarani wote

 Kila wiki kwa ibada za sabato na za katikati ya juma
Kuwabaini wageni ili kuwashawiasi waagize ushirika
04
Kujenga uhusiano mzuri na idara zingine
Kupeana na kupashana habari  zinazohitajika na kuingiliana na idara zingine
Anitha Thobias
Kila wiki na kila robo ya ya mwaka taarifa kukusanywa kutoka idara zote
Kupata taarifa sahihi za mshiriki kwa kila idara
05
Kuandaa na kutengeneza benki ya takwimu ya washiriki wa kanisa
Kujua elimu, kazi, umri, hari,  jinsi na anapoishi mshiriki wa kanisa
Frank philemon
Mwishoni mwa mwezi wa 4
Kujua uhitaji, wa wa kila mshiriki
0606


Kusimamia taratibu na kanuni za kanisa


Kila kikao cha baraza na mkutano mkuu

Makarani wote

Kila Kikao

Kufuata taratibu

CHANGAMOTO.
Ofisi ya makarani inaathirika na changamoto zifuatazo zinazolikabili kanisa:
*      Mfumo hafifu wa mawasiliano ya kiteknolojia.
*      kanisa kutokuwa na mpango mkakati wa muda mfupi na mrefu.
*      Ufinyu wa vyanzo vya mapato (kwani kanisa limejitegemeza sana katika zaka na sadaka pekee)
*      Idadi kubwa ya waumini kutokuwa na ushirika
*      Uhaba na kukosekana kabisa kwa baadhi ya vitendea kazi kwa ajili ya idara/ofisi ya makarani na idara zingine
*      Kukosekana kwa ofisi na umeme katika maeneo ya kanisa

BAJETI (MAHITAJI)
Endapo bajeti ya ofisi ya makarani itatekelezwa, itaondoa changamoto kubwa zinazoikabili idara/ofisi ya makarani. Mpango wa bajeti wa idara hii umebainisha katika uhitaji wa mambo yafuatayo hapo chini ili kukamilisha kujenga msingi wake na hata uwabijibikaji kwa ujumla.

Luka 14: 28-30 “Maana ni nani kati ya ninyi kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kumalizia? Asije akashindwa kumalizia baada ya kupiga msingi watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, wakisema mtu huyu alianza kujenga akawa hana nguvu ya kumalizia”

1. Bajet ya Muda mfupi (Bajeti ya Dharula)
Bajeti ya muda mfupi inahitaji kutekelezwawake ndani ya mwezi wa pili kutokana na uhitaji wake haraka.

S/No
Hitaji
Kiasi
Matumizi Yake Kiofisi
Utekelezaji
Chanzo Cha Pesa
01.
Stepula mashini1
6, 000/-
Kubania karatasi
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
02.
Counter book 1
2, 500/-
Mahudhurio ya kikao
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
03.
Punching mshn1
5, 000/-
Kutobolea  karatasi
Mwezi aa pili
Bajeti ya kanisa
04.
Kalam 10
2, 000/-
kuandikia
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
05.
Rula 1
500/-
Kupigia mistari
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
06.
File 7
14, 000/-
Kutunzia taarifa&takwimu
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
07.
Wino wa printa
20, 000/-
Copy & printing
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
08.
Gundi ya maji
2, 000/-
Kubndikia matangazo
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
09.
Modem
25, 000/-
Kwa ajili ya internet
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
10.
Pesa ya stempu
40, 000/-
Kutuma&kuagiza ushirika
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
11.
Rim paper 2
26, 000/-
Copy, printing & kuandikia
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
12.
Bahasha katoni 1
25, 000/-
Kutumia barua
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
13.
Pesa ya bando
15, 000/-
Kutuma taarifa
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
14.
Pesa ya tahadhari
30, 000/-
Dharula za kiofisi
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa

15
Pesa ya vocha
10, 000/-
mawasiliano
Mwezi wa pili
Bajeti ya kanisa
Jumla Ya Bajeti Ya Muda Mfupi  Ni Tsh. 223. 000/=


2. Bajeti ya muda mrefu.
Bajeti hii utekelezaji wake ni wa muda mrefu kulingana na upatikanaji wa pesa pamoja na kutokuwa na uhitaji wa haraka sana, japo ni muhimu kutekelezwa hadi ifikapo mwaka 2017.

S/N
Hitaji
Kiasi
Matumizi
Utekelezaji
Chanzo Cha Pesa
01.
Laptop
500, 000/-
Kuchapa na kutumia taarifa
2016/2017
Changizo kutoka kwa washiriki
02.
Printer (3 in 1)
350, 000/-
Kuprinti, kuskani na kunakilisha nyaraka za kanisa
2016/2017
Jumla ya pesa Tsh. 850, 000/=


Jumla kuu ya bajeti   =  bajeti ya muda mfupi + bajeti ya muda mrefu
                                             
                                                        223, 0000 + 850, 000
                                                    
                                                               1, 073, 000/=





Mpango kazi huu umeandaliwa na idara ya makara (ofisi ya makatibu) wa kanisa
1.      Anitha Thobias (karani mkuu)  _________________________________
2.      Frank philemon (karani msaidizi) _________________________________


Comments

Post a Comment

Thanks for viewing and passing through NMEE blog. Keep following the blog

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU