HIV/UKIMWI

HIV/UKIMWI


AIDS (Ukimwi) upungufu wa kinga mwilini.
Hii humaanisha kwamba ugonjwa hudhoofisha mfuno wa kinga.  Kwa sababu mfuno wake wa kinga ni dhaifu, watu wenye ukimwi hujenga hofu ya maisha katika magonjwa na maambukizi ya kifua kikuu, kansa na magonjwa mengine.  Virusi (HIV) hufanya kazi polepole na waathirika huweza kuonekana wenye afya njema kwa miaka hata 10 kabla hawajaanza kuugua na kufa.  Hakuna tiba ya virusi / ukimwi.  Hivyo kila apataye virusi vya ukimwi atakufa.  Mamilioni ya watu duniani wameathirika na ukimwi. 
                                       

Unapokuwa na virusi, tunasema ni mwathirika na virusi.  Unapoanza kuugua bila kupata nafuu tunasema una ukimwi.  Wachunguzi wanasema kwamba vifo vya waathrika wa ukimwi vitakuwa milioni 1,7 kwa mwaka ifikapo 2006.  Badala yake vifo milioni 3 viliripoliwa kwa mwaka 2001 peke yake!!  Kwa kweli ugonjwa kuu ni mbaya sana kuliko tunavyo dhani.  Katika mwaka 2001 watu zaidi ya milioni 22 walikufa kwa ukimwi.  Zaidi ya watu milioni 40 waliambukizwa virusi vya ukimwi.  Nani ajuaye idadi tunapoingia katika mwaka wa 2004?  Jana hili limekuwa baa kubwa.  Wachunguzi husema kwamba ifikapo 2010 utapunguza miaka ya kuishi Afrika kufikia mwaka 30.  Idadi kubwa ya waathrika ni vijana.  Kila siku katika Afrika vijana 7, 000 huambukizwa virusi.  Maambukizi husambaa toka kwa vijana hadi kwa watu wazima wanaojamiiana na vijana.  Waganga wengi wa hienyeji huwaambia watu kwamba ukijamiiana na bikira basi umepona.  Hii siyo kweli.  Watu katika Afrika hawapendi kuzungumzia ukimwi.  Hawawa elezi watoto wao kuhusu kujamiiana na watoto wao wengi wanakufa.  Wakati umebadilika na ni wakati wetu kuongea na watoto wetu na majirani kuhusu hatari ya kujamiiana nje ya ndoa.  Vijana wana uelewa au ujumbe potofu na huhatarisha maisha yao wapolala ovyo. 
                                   

Ukimwi husambaa vipi? 

A. Kwa Kujamiiania:
  • Mume kwa mke na mke kwa mume.
  • Mume kwa mume.

B.  Damu:
  • Kuongezwa damu.
  • Kuchangia sindano na vifaa vingine.

C.  Watendakazi wa Afya:
  • Sindano, majeraha yalivyo wazi.


D.  Kuchomwa sindano zisizo chemshwa katika hospitali na kliniki.

E.  Watoto:
  • Tumboni
  • Katika njia ya mzazi
  • Kwa kunyonyesha

Iwapo mjaanzito ana virusi kuna tiba maalum kupunguza hatari ya mtoto kuambakizwa.
Virusi / Ukimwi hauambukizi kwa hugusana.  Na wala hauambukizi kwa njia ya wadudu.  Watu wanaokunywa pombe wako katika hatari ya kupata virusi/ukimwi kwasababu wanafanya maamuzi mabaya.  Pombe pia hudhoofisha kinga ya mwili na hufanya maambukizi ya virusi vya ukimwi kuwa rahisi.  Mungu anayo njia ya utatuzi wa janga hili.  kwa hakika na utatuzi wa awali.  Kama ulimwengu ungekubali agizo hili ungeondosha mara moja gonjwa hili.  Agizo la Mungu ni ndoa kati ya mume na mke kwa maisha yote.  Mungu anasema kujamiiana nje ya ndoa ni chambi.  Kutoka 20: 14 Usizini.  Kuna kanuni nyingine zinazopatikana katika Biblia ambazo kwa hakika zinatulinda.  Mambo ya Walawi 18: 22.  Kumbukumbu la Torati 23: 17.  Kutoka 22: 19. Warumi 1: 24, 26, 27.  1 Wakorintho 6: 9-10.

Mungu anahitaji sisi sote tuwe wenye afya na furaha.  Yeye hututakia tu lililo jema kwetu.  Sasa ni wakati wa kufuata uongozi wake na kuwambia wengine maagizo yake kuhusu afya.  Kumbuka kwamba watu wenye virusi vya ukimwi wanahitaji msaada wetu wa hali na mali.  Wengi wao walikuwa waaminifu walipoambukuzwa na wengine wanajuta kwa kufikira walivyotenda vibaya.  Tunahitaji kuanza kuzungumza juu ya gonjwa hili na siyo kuacha na kukwepa ukweli kabla hatujachelewa!


                               

Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU