Kisa Maarufu Cha Nyama




Daima tumekuwa tukiamini kuwa tunahitaji kula nyama ili tuwe na nguvu na afya.  Kwanini?  Kwasababu nyama ina ‘protini’ na ni ya muhimu sana kwa miili yetu.  Inajenga na kutengeneza miili yetu.  Lakini mwaka 1950 wana sayansi waligundua kuwa hasa tunaweza tukawa tunakula protini kupita kiasi.  Hasa kama tuna kula nyama nyingi.  Wana sayansi hawa ni Daktari Hardinge na Daktari Stare walithibitisha kuwa mtu ambaye anatumia vyakula vya mimea tu (vegetarian) hupata protini zote ambazo mwili wake unazihitaji.  Watu wameamini kuwa kula sana vyakula vya protini za mnyama itatufanya tuwe na nguvu na uwezo.  Vilevile waliamini kuwa husaidia akili na mwili.  Lakini ni jambo la kweli?  Ni wapi jambo hili la umaarufu wa nyama lilikotokea?  Protini iligundulika 1838.  Protini ni muhimu kwa namna yoyote ya maisha!  Ni yamuhimu sana!  Tunahitaji protini ili misuli yetu itende kazi vizuri, kuwa na homoni nzuri na uwiano wake mzuri, tuweze kukua na kutengeneza sehemu tulizo jikata na vidonda na vitu vingine vingi.  Kwahiyo umuhimu wa protini hakuna ‘kisa’ ni ya muhimu tu!  Lakini watu wamechanganyikiwa na kufikiri kuwa tunaweza tu kupata protini toka kwa vyakula vya nyama.  Protini moja ina kemikali asidi 20 au inaitwa (amino acids).  12 ya hizi asidi hutengenezwa miilini mwetu, lakini 8 zinazobaki sivyo.  Tunahitaji kupata hizi asidi 8 tokana na vyakula tulavyo.  Watu walifikiri unaweza kupata kwa kula nyama tu.  Lakini hawakujua kuwa ng’ombe ni kama wanadamu tu!  Nao pia wanahitaji asidi 8 na wanaipata kwa kula majani!  Kwa kweli tunaipata asidi 8 iliyotumika kwa sababu ng’ombe kwanza lazima ale majani.  Hatuhitaji kula nyama, hivyo, tunaweza kula mimea – vyakula muhimu na kupata protini ifaayo ambayo kamwe haijatumika na ngombe, nguruwe, au samaki!
                                   

Wanasayansi vilevile wameona kuwa miili yetu haihitaji protini nyingi kama ilivyo fikiriwa!  Tunaweza hasa kula protini – protini ambayo ni ya kutuletea afya.
Chakula cha mimea kilicho na matunda, nafaka, mboga za majani na jamii ya karanga ni vya kiwango cha pekee sana kwa protini!  Siyo protini kupita kiasi au pungufu mno.  Tunapo kula nafaka za aina mbalimbali, mboga za majani, karanga na matunda tutapata zaidi kuliko protini tu.  Tutapata virutubisho vingine ambavyo ni vyamuhimu pia!  Hapa kuna baadhi ya mifano ya vyakula vyenye uwingi wa protini na vina asidi zote zinazo hitajika mwilini:

1.  Viazi vitamu                       2.  Viazi mviringo                   3.  Mchele wa rangi ya kahawia (au
4.  Nyanya                               5.  Maboga                              mchele mweupe usio kobolewa upo
6.  Unga wa ngano kamili       7.  Mahindi                              hapa Tanzania)
8.  Maharagwe                                    9.  Mboga kijani kibichi          10.  Kitunguu saumu

                 


                                                                

Protini kupita kiasi mwilini vilevile ‘huiba’ virutubisho vingine vinavyoitwa ‘kasiamu’ kasiamu ni ya muhimu sana kwasababu hutupatia mifupa yenye nguvu na afya ya meno.  Watu husema kuwa tunahitaji kula nyama nyingi na kunywa maziwa ilikujipatia kasiamu.  Lakini wanasayansi wamegundua kuwa maziwa na nyama hutupatia protini nyingi kupita kiasi na protini hiyo ‘huiiba’ kasiumu.  Na hutusababishia udhaifu wa mifupa hasa kwa akina mama wazee.  Unaitwa osteoporosis – ugonjwa wa mifupa kwa kukosa kalisiumu mwilini.
Tunapokula vyakula vya mimea vyenye wingi wa kalisium, tutapata kalisium zaidi kuliko kunywa maziwa kwasababu miili yetu haitumi kwa wingi kama 60%- 80% ya kalisium ya maziwa kwa vyovyote vile!  Ni aina gani ya vyakula vilivyo na wingi wa kalisium?

1.  Dengu                               2.  Nafaka                               3.  Mchicha na mgoa kijani
4.  Maharage                           5.  Ufuta                                  6.  Rapu
7.  Maharage ya soya              8.  Maziwa ya soya                 9.  Alizeti

Siri ya kuwa mwana matengenezo mwenye afya:  Kula aina mbalimbali za vyakula.  Kama ukiamua kula tu ugali na maharage na bila kingine mwili wako utakosa lishe nzuri na mwishowe utaugua.  Kula aina anwai za mboga na matunda katika juma.  Changanya na vyakula vingine.  Andaa chakula chako vizuri, kionekane kizuri na chenye afya na ufurahie unapokila!
Vilevile wanasayansi wamethibitisha kuwa nyama pamoja na uwingi mno wa protini husababisha kansa, ugonjwa wa moyo na athari nyingine mbaya za afya.  Ni wakati wa kufanya mabadiliko!!

Tafadhali Kumbuka:  Ujumbe wa afya ni muhimu sana, lakini tunahitaji daima kumwomba Mungu atusaidie kuwa na uwiano.  Ni muhimu sana kuto wa kwaza watu kwa kuwa piga nyundo (gonga – hammering) kuhusu kula nyama na kuwa ambia vitu vya kijinga kama ‘hutaokolewa kamwe kama si mwana matengeneto!’
Na amini wengi wameukataa ujumbe wa Adventista kwasababu ya misimamo mikali ya watu kanisani.  Wewe mwenyewe uwe mfano!  Onekana unaishi kiafya na watu wengine watafuata ushauri wako mzuri.           
dsaResource:      




Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU