SAMAKI

Samaki


Miaka kadhaa iliyopita watu walisikia kuwa kula samaki kuli leta afya sana.  Watu wengi waliacha kula nyama nyekundu na kuhamia kula mlo wa samaki.  Kiwango chao cha mafuta mabaya kwenye damu (cholesterol) kilipungua na walikuwa wakijisikia furaha.  Watumiaji wa vyakula vya mimea walianza kutumia samaki na viwango vya (cholesterol) vilipanda kidogo!  Je, hasa samaki ni kitu kizuri kwako?  Tuta angalia jambo hili kwa ukaribu.  Kuna visa viwili katika jambo hili.

                                                  

Watu walihamasika kuhusu ulaji wa samaki kwa wingi kwasababu ya baadhi ya mafuta yanayo patikana ndani ya samaki wakubwa na wanene.  Mafuta hayo yanaitwa omega 3 fats.  Yaani aina 3 muhimu za mafuta.  Na yana weza kupigana dhidi ya magonjwa ya moyo.  Tatizo ni kuwa samaki ni kundi la nyama na kwahiyo ina cholesterol ndani yake.  Hivyo unapokula samaki una inua cholesterol yako mwenyewe katika damu yako.  Na kama unataka unufaike zaidi ni heri ujiepushe kabisa na ulaji wa mafuta yato kanayo na wanyama badala yake na uwe mtumiaji wa vyakula vya mimea tu.  Kwa nini?  Kwa kuwa aina kuu tatu za mafuta zinapatikana katika vyakula vya mimea ambayo ndani yake havina athari ya cholesterol.  Hapa kuna mifano ya vyakula vyenye aina kuu tatu za mafuta:  Maharage ya soya; mafuta ya soya; spinachi; parachichi; viazi vitamu; ndizi; apples; viazi mviringo; tango; mkate wa ngano kamili.
                     

Hapa kuna mfano mwingine wa njia nyingine ya ajabu ambayo Mungu ali tuandalia lishe kamili katika vyakula vya mimea.  Kitu kingine tunacho paswa kufahamu ni uchafu.  Siku za leo Bahari nyingi zimecha fuliwa pamoja na mito mikubwa na maziwa.  Wana sayansi wamegundua kuwa samaki wamejawa na sumu (toxins) ambazo zina kuwa na nguvu.  Hivyo maji yaliyo na mchanganyiko na uchafu yanaweza kusababisha samaki walio wachafu zaidi.  Kwanini ni vibaya kula samaki walio katika maji yaliyo chafuliwa hivyo? Sumu zipatikanazo ndani ya samaki mwenyewe zimekuwa na usababishi wa kansa kwa mwanadam na inatakiwa kuzuiliwa.  Kwa ajili ya afya ni vizuri zaidi kula mlo wenye afya wa chakula cha mimea.  Kumbuka siri ya kuwa mtumiaji wa vyakula vya mimea ni kula aina mbalimbali nzuri za vyakula vyenye afya. 



Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU