UNAUUGUAJE?

Nina Uguaje?


Kuna sababu nyingi tofauti zinazo sababisha ugonjwa.  Sababu yenye umuhimu sana ni mfumo mbaya wa maisha!  Kuvunja kanuni 8 za afya na kuishi katika namna isiyo ya kiafya hutuongoza kwenye shinikizo la damu, kansa, TB, ukimwi, ugonjwa wa moyo (heart attack) mfadhaiko, kisukari na mengine mengi.

Magonjwa mengine husababishwa na virusi, bakteria na vijidudu vidogo vya magonjwa.  Mifano michache ni:
-  Surua            -  Kuharisha     -  Ukimwi        -  Kupooza      -  Homa           -  Kichomi
-  Homa ya uti wa mgongo                 -  TB                            -  Upele  na mengine mengi
                                
Magonjwa mengine husababishwa na minyoo na wadudu wanao ambukiza: 
-  Malaria                     -  Kichocho                 -  Tegu     -  Michango             -  Michango uzi

Magonjwa mengine husababishwa na ajali.  Mengine kwasababu ya miili yetu kuzeeka na kuchakaa.  Magonjwa mengine hurithiwa toka kwa wazazi na mengine wakati wa kuzaliwa. 
‘Kuna milango 3’ kwa vijidudu vya magonjwa kuingia mwilini mwetu.

1.  Mdomo:  Wadudu huingia midomoni tunapokula chakula kilicho haribika, kunywa maji mabaya na machafu na kutoosha mikono.
2.  Pua:  Wadudu wa maradhi huingia kupitia puani mpaka kwenye mapafu yetu tunapovuta hewa mbaya.
3.  Ngozi na Utando wa Kamasi:  Daima ngozi huzuia vijidudu isipokuwa kama kuna kidonda kilicho wazi au kuumwa na mdudu na mara tunapo endekeza mazoea mabaya ya kutozingatia usafi kwa ujumla.
                    
Mwili daima hushambuliwa na wadudu wa maradhi.  Mtu anaugua kutegemeana na kiasi cha wadudu walio ingia mwilini,  jinsi vijidudu vilivyo na nguvu, na mwili una nguvu kiasi gani.  Mtu ambaye ni mgonjwa gonjwa na hali chakula kifaacho huwa na kinga kidogo kwa vijidudu hivi, hivyo huugua haraka zaidi.



Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU