Uvutaji wa Sigara na madhara yake



Katika tumbaku zipo sumu mbaya zaidi ya 4, 000 ambazo wana sayansi wamezipata.  Kila wakati mvutaji anapovuta sigara sumu hizi zote huenda mwilini mwake.  Nyingi za sumu hizi husababisha kansa (carcinogens).  Zinaweza kusabibisha kansa zenyewe tu.  Tumbaku inaweza kuvutwa kama sigara; kwa kiko; kutafuna; kunusa; au kusokota!  Siyo lazima ivutwe tu.  Haijalishi mvutaji anatumaije tumbaku.  Daima ni mbaya na yenye athari kwa afya yako. 

                              

Moja ya sumu mbaya ni:
1.  Nikotini (Nicotine)
2.  Lami  (Tar)
3.  Hewa chafu  (carbon monoxide)

Nikotini:  Ni dawa inayo ufanya mwili ujisikie haja ya kuvuta na kama mtumiaji atapunguza uvutaji wake (hasa unapo anza kuacha kuvuta) mwili utaanza kuwa na dalili ya kutaabika, kama kuumwa kichwa, mapigo ya haraka ya moyo, kutoa jasho.  Kichefuchefu, maumivu ya misuli, n.k. ni kwasababu ya kutawaliwa na sumu hiyo mvutaji ana taabika kuiacha.

Lami:  Katika tumbaku kuna nta ya lami inayo fanana na ile inayo onekana kwenye barabara ya lami.  Ni sumu zenye nguvu.  Zina nguvu miongoni mwa sumu tuzijuazo.  Wana sayansi wamechukua nta toka kwenye tumbaku na kuipaka mara moja kwa panya katika kijisehemu kidogo cha ngozi yake.  Panya akapata kansa baada ya muda mfupi.

Hewa Chafu (Carbon Monoxide):  Ni gesi inayo patikana kwenye eksosi ya gari.  Gesi hiyo hujinasa yenyewe kwenye chembechembe nyekundu za damu hata oksijeni isisambae mwilini kunako hitajika oksijeni.  Kama chembechembe nyingi zitatiliwa sana sumu mtu anaweza akafa.

Tunaweza kufikiri kuwa huathiri tu mapafu, lakini madhara yake huwa hata sehemu zingine za mwili.  Kuvuta kuna sababisha kansa nyingi.  Kwa mfano:
-  Kansa ya midomo                                                    -  Kansa ya sanduku la sauti
-  Kansa ya mdomo                                                     -  Kansa ya koromeo
-  Kansa ya koo                                                           -  Kansa ya ini
-  Kansa ya kibofu cha mkojo                                     -  Kansa ya figo
-  Kansa ya kizazi                                                        -  Upungufu wa damu
-  Kansa ya utumbo mkubwa                                      -  Kansa ya ngozi
-  Kansa ya uume

Akina mama wajawazito hujiweka katika hatari kwa watoto ambao hawaja zaliwa bado na kuwa sababishia matatizo mengi.  Watoto wanakuwa na matatizo ya kitabia, akili kidogo, kuzaa vitoto vidogo; ugonjwa wa athma, matatizo ya kupumua.  Mama avutaye kuna hatari ya mimba kuporomoka.  Tabia za mvutaji vilevile huathiri wale wasio vuta.  Kuvuta moshi ulio tolewa na mvutaji hukuhatarisha kwa magonjwa yote yaliyotajwa hapo juu. 

                                              
Ni vigumu kuacha kuvuta, lakini hapa zipo njia 10 za kukusaidia kuacha kuvuta. 
1.  Wanapaswa wachague kuto vuta.
2.  Pasiwe wa sigara zilizo fichwa mahali fulani.
3.  Wafanye mazoezi ya kuvuta hewa kwa nguvu na kupumua.
4.  Mazoezi ya kila siku (kutembea).
5.  Wapate usingizi wa kutosha.
6.  Wawe na maji mengi mwilini (vikome 8 wastani kwa siku).
7.  Maji kwa nje – oga mara kwa mara.
8.  Epuka kafeini, milo mizito, vyakula vyenye ukali sana.  Pombe isinywewe kabisa!!
9.  Epuka kushirikiana na watu wanao vuta.  Epuka majaribu.
10.  Saidia mwili wako!!

                                

Ellen White aliandika zaidi karne iliyo pita kuhusu hatari ya kuvuta.  Watu walifikiri ni kitu kigeni na hawa kuelewa. Lakini, wana sayansi leo wamethibitisha kila kitu alicho kiandika muda mrefu ulio pita.

Tumbaku si mwuaji tu.  Pia huiba maisha bora ya mtu, huharibu furaha, husabibisha udhaifu, na hunyang’anya fedha nyingi toka kwa jamii.


Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU