VILEO

Vileo

Unywaji wa pombe huwadhuru hao wanywao magonjwa kama yale yanayo weza kuua seli za lini (cirrhosis of the liver) pia huathiri familia na jamii kwa njia nyingi.  Watu wanapolewa hupoteza uwezo wao wa kuamua jema na hali hii husababisha huzuni mkubwa.  Heshima hupotea mara tu mtu aliyelewa kutoka kwenye hali ya kulewa na kuona yale aliyoyatenda wakati alipo kuwa amelewa.

                                                  

Vileo viko katika kundi la kemikali ambazo ni vimiminika katika hali ya hewa ya ndani ya chumba.  Vileo viko katika jamii nyingi.  Jamii zote hizo, isipokuwa moja, huweza kuua hata kwa kunywa kiasi kidogo tu.  Kileo aina ya Ehili (Ethyl) mwili huweza huweza kukivumilia kikiwa ni kiasi kidogo, lakini huweza kuua mtu ikiwa katika kiwango kikubwa.  Ethili ni aina ya kileo inayopatikana katika vinywaji vyote vyenye kileo ndani kileo hupatikana ulimwenguni hote.  Kila nchi na kila jamii ya watu wanayo aina fulani ya kileo.  Tunasoma juu ya kileo katika Biblia.  Mithali 20:1.  Sisi kama Wakristo yatupasa kujiepusha na unywaji wa vileo kwa kuwa hudhuru miili na akili zetu.  Watu wengi hunywa pombe kwasababu wanaamini kwamba vina ndosha matatizo yao au kuwafanya wayasahau.  Wanapotoka kwenye hali ya kulewa huyahuta matatizo yao yako palepale!  Hutokea nini wanapokunywa pombe?

Kwanza huingia tumboni.  Pombe ni mojawapo katika vitu visivyo hitaji kubadilishwa na mwili kabla ya kufyonzwa huingia katika njia ya damu.  Inaenda moja kwa moja kutoka tumboni hadi kwenye damu.  Hii humaanisha kwamba inaenda kwenye damu haraka sana.  Kama tumbo liko tupu, kileo kuenda na kufika kwenye damu kwa dakika 2 – 3.  Wakati pombe imefika tumboni hukera mfuko wa tumbo.  Kero (usumbufu) hii husababisha mfuko wa tumbo huuma, ama vidonda vyenye mwako au kuvimba.  Usumbufu huu huitwa uvimbechungu wa tumboni (gastritis).  Tumbo linapopata usumbufu huu mara kwa mara huweza kusabibisha vidonda tumboni.  Vidonda havitapona kwa muda mrefu iwapo tumbo litaendelea kupata usumbufu huu wa pombe na vikolezo vikali vya vyakula.
Pombe isiyofyonzwa kutoka tumboni kwenda kwenye damu, hukamia kwenye damu taratibu.  Pombe husimamisha kufyonzwa kwa vitamini na protini kwenda kwenye damu.  Vitamini na protini hizi kuhitajika katika mwili kwa ajili ya kulamisha na kulinda.  Pombe hufyonzwa badala ya vitamini ambavyo hutolewa nje kwa njia ya choo.

                                
            Tumbo                                                                        Damu

Katika njia za damu  pombe husababisha chembeche nyekundu za damu kunata na kusinyaa.  Chembechembe nyekundu za damu luinata pamoja na kushusha au kupunguza mzunguko wa damu.  Sehemu nyingi za mwili kukosa oksijeni / hewa safi inayohitajika katika chembechembe zinazoihitaji kwa wingi na matokeo yake hizo chembebchembe kufa.  Mifupa yetu ni kama viwanda.  Hutengezwa chembechembe hizi kwa mamilioni kila siku.  Kunapokewa na pombe katika damu, mifupa haifanyi kazi vema kutengeneza chembechembe za damu.  Hivyo mtu anaye kunywa pombe mara kwa mara anakaribiwa na upungufu wa damu (aneamic).  Chembechembe nyeupe za damu (askari) hutiwa sumu na haiwezi kulinda miili yetu vema hutokana na magonjwa.  Damu huchukua pombe hadi kwenye ini.  Ini ni kama kiwanda kidogo mahali ambapo sukari, mafuta na protini hubadilishwa na kuwa mafuta safi ambayo mwili hutumia kwa ajili ya nguvu na kulamisha (kujenga sehemu zilizo chakaa).  Pombe nayo hubadilishwa katika ini na kuwa hewa chafu (carbon dioxide).  Lakini ini haliwezi kuondosha pombe yote; nyingine hupenya na kwenda katika sehemu zingine za mwili na kurudi tena kwenye ini baadaye na hubadilishwa hatimaye mwili huitoa nje.  Ini huweza kutoa nje kiacha ml 10 kwa saa.  Kwa hadri mtu anapokunywa pombe nyingi kwa muda mrefu ndivyo pia inavyo chukua muda mrefu kulolewa nje.  Pombe hutia sumu katika chembechembe za ini, hivyo huugua na kufa.  Kwa hadiri ini linavyo jaribu kulamisha na kurudishia chembechembe zilizokufa hukutwa zimekuwa na mahovu.  Ugonjwa huu huitwa (chirrhosis of the liver).  (ugonjwa wa kuua celi za ini).

                                                   
                                           Ini                                                                             Moyo

Baada ya pombe huacha ini huhamia kwenye moyo.  Moyo husukuma damu pamoja na pombe kwenye sehemu zote za mwili pamoja na ubongo.  Ni katika ubongo ambapo pombe ina madhara makubwa zaidi.  Pombe hupoozesha chembechembe za ubongo.  Hazitaweza kupeleka ujumbe halika sehemu zingine kama ilivyokuwa awali.  Ujumbe katika ubongo huchanganyika.  Sehemu ya kwanza ya ubongo kuathirika na sehemu ya mbele.  Hapa ndipo sehemu ya udhibili wetu na uwezo wa kuwasiliana na Mungu inaathirika.  Hii ndiyo sababu ni mulimu sana kwa Mkristo anayetaka kujenga uhusiano na Mungu asitumie pombe.  Mtu anayekunywa pombe sana hawezi kutembea vizuri kama inavyopasa; hawezi kutazama vizuri ilivyo kawaida.  Hawezi kufanya kazi yake vema.  Hawezi kupima umbali vizuri.  Kila kitu anacho jaribu kukifanya huwa kigumu.  Mara pombe hufika mgongoni na sehemu za chini ya ubongo mahali ambapo miondoko hudhibiliwa.  Mlevi anaweza kupata tatizo katika kutembea au kuasimama moja kwa moja katika hali kama hii ni hatari kuendelea kunywa.  Sehemu nyingine ya ubongo inayoathirika ni sehemu inayodhibiti utambuzi wetu na sehemu zingine zinazo tufanya uwe hai k.v. kupumua, mapigo ya moyo na msukumo wa damu.  Pombe inapozidi huzunguka katika ubongo mtu huweza kufa. 

                           

Iwapo mnywaji ni mja mzito pombe huweza kuathiri mtoto tumboni.  Watoto hawa huzaliwa na matatizo mengi hawawi na akili kama akina mama wasio kunywa pombe.  Kuna madhara mengine mengi ya pombe:
1.  Msukumo mkubwa wa damu (BP).
2.  Kupooza
3.  Matatizo ya moyo.
4.  Mafuta machafu mwilini (cholesterol).
5.  Msukumo ndogo wa damu.
6.  Kutofaa katika kuja miiana.
7.  Upungufu wa Vitamin E.
8.  Uchovu
9.  Udhaifu wa mifupa.
10.  Upungufu wa damu.

Wanasayansi wamegundua kwamba kunywa pombe nyingi husababisha ubongo kuwa mdogo katika umbo, chembechembe za ubongo zimapokufa, hazirudishwi tena.  Unywaji wa pombe pia husababisha huzuni nyumbani.  Familia nyingi huvurugika kwa ajili hii, na ajali nyingi pamoja na vifo visiyokuwa vya lazima husababishwa na ulevi.
                               

Ni vigumu kuacha kunywa pombe lakini si mara zote isiwekane!  Pombe kuhitaji msaada mkubwa toka kwa ndugu na marafiki.  Mungu ameahidi uwezo wake Wafilipi 4: 13.  Nikazi ya Wakristo na kanisa kuwasaidia ndugu zetu wanao tangatanga katika tatizo hili.


Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU