UFUGAJI WA MBUZI NA KONDOO

KANUNI ZA UFUGAJI BORA WA MBUZI NA KONDOO
Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi katika mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe. Kutokana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzao wa muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengi kwa kipindi kifupi. Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi, sufu na mazao mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato.

Ufugaji bora wa mbuzi na kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:
i)             Wafugwe kwenye banda au zizi bora,
ii)                  Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji (nyama, maziwa au sufu),
iii)                Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili,
iv)                Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na
mtaalam wa mifugo,
    v) Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na
vi) Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko

Zizi au Banda la Mbuzi/Kondoo
Mbuzi/kondoo wanaweza kufugwa katika mifumo ya huria, shadidi na kwa kutumia njia zote mbili. Zizi hutumika katika mfumo huria ambapo mbuzi/kondoo huchungwa wakati wa mchana na kurejeshwa zizini wakati wa usiku.

Zizi bora ni lile lenye sifa zifuatazo:
Lililo imara linaloweza kumkinga mbuzi/kondoo dhidi ya wanyama hatari na wezi,
Lililojengwa mahali pa mwinuko pasiporuhusu maji kutuama,
Ukubwa wa zizi uzingatie idadi na umri wa mifugo. Ni vema mbuzi/kondoo
watengwe kulingana na umri wao; na Liruhusu usafi kufanyika kwa urahisi.
Pale ambapo mbuzi/kondoo wanafugwa kwa mfumo wa shadidi hufugwa katika banda wakati wote. Banda bora la mbuzi/kondoo linatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:
Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya hewa hatarishi kwa mfano jua kali, upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama hatari,
Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi kufanyika kwa urahisi,
Lijengwe sehemu isiyoruhusu maji kutuama na liwe mbali kidogo na nyumba ya kuishi watu. Pia ujenzi uzingatie mwelekeo wa upepo ili hewa kutoka bandani isiende kwenye makazi,
Liwe na sakafu ya kichanja chenye urefu wa mita 1 kutoka ardhini (Kwa banda la mbuzi),
Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji na mahali pa kuweka jiwe la chumvichumvi; na
Liwe na vyumba tofauti kwa ajili ya majike na vitoto, mbuzi/kondoo wanaokua, wanaonenepeshwa na wanaougua.

Vifaa vya Kujengea na Vipimo vya Banda                                         
Inashauriwa banda la mbuzi/kondoo lijengwe kwa kutumia vifaa vinavyopatikana kwa urahisi katika eneo husika. Ukubwa wa banda utategemea idadi ya mbuzi/kondoo wanaofugwa humo na ukubwa wa umbo
Paa lijengwe kwa kutumia vifaa kama miti, mbao, na kuezekwa kwa nyasi, makuti, majani ya migomba, mabati au hata vigae kwa kutegemea uwezo wa mfugaji,
Kuta zijengwe kwa kutumia mabanzi, mbao, nguzo, wavu wa waya, fito na matofali. Kuta ziwe imara zinazoruhusu hewa na mwanga wa kutosha. Mlango uwe na ukubwa wa sentimita 60 x 150,
Sakafu inaweza kuwa ya udongo au zege. Sakafu ya kichanja inaweza kujengwa kwa kutumia miti, fito, mianzi, mbao au mabanzi na iweze kuruhusu kinyesi na mkojo kupita. Chumba cha majike na vitoto kiwe na nafasi ya sentimita 1.25 kati ya papi na papi, fito na fito au mti hadi mti. Chumba cha mbuzi/kondoo wakubwa iwe sentimita 1.9 kati ya mbao na mbao.
Uchaguzi wa Mbuzi/Kondoo wa Kufuga                                                                        Madhumuni ya kuchagua mbuzi au kondoo wa kufuga ni kuboresha uzalishaji na kuendeleza kizazi bora. Kuna aina nyingi za mbuzi/kondoo wanaoweza kufugwa kulingana na mazingira na mahitaji ya mfugaji. Uchaguzi hufanyika kwa kuangalia umbile, uzalishaji na kumbukumbu za wazazi kama vile umbo kubwa, ukuaji wa haraka, uwezo wa kutunza vitoto na kutoa maziwa mengi. Mbuzi wanaofaa kwa ajili ya maziwa ni aina ya na pamoja na chotara wao
Mbuzi wanaofaa kwa ajili ya nyama ni  na chotara wao, mbuzi wa asili kama  vile  , Newala na Ujiji. Mbuzi aina ya Malya wanafaa kwa ajili
ya nyama na maziwa.


Aidha, kondoo aina ya (BHP), nao wanafaa kufugwa kwa ajili ya nyama.  na  hufugwa kwa ajili ya sufu,  wakati  na  hufugwa kwa ajili ya nyama na sufu. Hapa Tanzania kondoo wanaopatikana kwa wingi ni , Masai Red Dopper na kondoo wengine wa asili
.
Mbuzi/kondoo jike wanaofaa kwa ajili ya kuzalisha maziwa na nyama wawe na sifa zifuatazo:-
Historia ya kukua upesi, kuzaa (ikiwezekana mapacha) na kutunza vitoto vizuri,
Umbo la mstatili linaloashiria utoaji wa nyama nyingi; na Asiwe na ulemavu wa aina yoyote
Sifa za Ziada kwa Mbuzi wa Maziwa                                                                                Awe na miguu ya nyuma iliyo imara na iliyonyooka na yenye nafasi kwa ajili ya kiwele; na                                                                                                                                  Awe na kiwele kikubwa na chuchu ndefu zilizokaa vizuri
Sifa za Dume Dume bora awe na sifa zifuatazo:-
Miguu iliyonyooka, imara na yenye nguvu,
 Asiwe na ulemavu wa aina yoyote,
 Mwenye uwezo na nguvu ya kupanda; na
             • Mwenye kokwa mbili zilizo kaa vizuri na zinazolingana



Utunzaji wa Vitoto vya Mbuzi/Kondoo
Utunzaji huanza mara tu baada ya kuzaliwa. Mfugaji ahakikishe:

Kitoto cha mbuzi/kondoo kinapata maziwa ya mwanzo (dang’a) ndani ya masaa 24 tangu kuzaliwa na kwa muda wa siku 3,

Kama kinanyweshwa maziwa, kipewe lita 0.7- 0.9 kwa siku. Maziwa haya, ni  muhimu kwani yana viinilishe na kinga dhidi ya magonjwa,

Iwapo mama hatoi maziwa au amekufa, inashauriwa kutengeneza dang’a; mbadala au kama kuna mbuzi/kondoo mwingine aliyezaa anaweza kusaidia kukinyonyesha kitoto hicho,
Kitoto cha mbuzi/kondoo kiendelee kunyonya kwa wiki 12 - 16. Wiki 2 baada ya kuzaliwa, pamoja na maziwa, kianze kupewa vyakula vingine kama nyasi laini na chakula cha ziada ili kusaidia kukua kwa tumbo. Aidha, kipewe maji wakati wote,
Vyombo vinavyotumika kulishia vinakuwa safi muda wote,
Kitoto cha mbuzi/kondoo kiachishwe kunyonya kikiwa na umri wa miezi 3 hadi 4 kutegemea afya yake; na
Vitoto vipatiwe kinga na tiba ya magonjwa kulingana na ushauri wa mtaalam
wa mifugo.

Matunzo Mengine Utambuzi
Mbuzi huwekewa alama ili atambulike kwa urahisi na kuwezesha utunzaji wa kumbukumbu zake. Shughuli hii hufanyika kwa mbuzi/kondoo akiwa na umri wa siku 3 - 14. Njia zitumikazo ni pamoja na:
Kuweka alama sikioni kwa kukata sehemu ndogo ya sikio,
 Kumpa jina kwa wafugaji wenye mbuzi wachache,
Kumvisha hereni ya chuma au plastiki yenye namba kwenye sikio,
Kumvalisha mkanda wenye namba shingoni; na

Kuweka namba kwa kuunguza sehemu ya ngozi ya mbuzi. Pale mfugaji anapotumia njia hii inashauriwa aweke alama kwenye eneo ambalo halitaathiri ubora wa ngozi




Kuondoa vishina vya pembe                                                                            Mbuzi/kondoo aondolewe vishina vya pembe akiwa na umri kati ya siku 3 hadi 14. Visipoondelewa hukua na kusababisha kuumizana na kuhitaji nafasi kubwa kwenye banda. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa mifugo.
Kuhasi                                                                                                                            Vitoto vya mbuzi/kondoo ambavyo havitatumika kwa ajili ya kuendeleza kizazi vihasiwe kabla ya kufikia umri wa miezi 3. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa mifugo.
Utunzaji wa Mbuzi/Kondoo wa Miezi 4 - 8                                                             Mbuzi wa miezi 4 mpaka 8 ni wale ambao wameacha kunyonya mpaka umri wa kupandishwa kwa mara ya kwanza. Mbuzi wa umri huu wana uwezo wa kula aina mbalimbali za malisho kama nyasi, mikunde, miti malisho na mabaki ya mazao wakati kondoo hupendelea zaidi nyasi fupi. Wakati wa kiangazi huhitaji kupatiwa chakula cha ziada au kupewa pumba za nafaka mbalimbali, mashudu ya alizeti, pamba na dengu, majani ya mikunde yaliyokaushwa, madini  na vitamini.
Katika ufugaji huria ni vema kuzingatia idadi ya mbuzi/kondoo inayoweza kuchungwa katika eneo, aina na hali ya malisho.
Ili mbuzi/kondoo aweze kukua na kufikia uzito wa kuchinjwa/kupevuka mapema, mfugaji anapaswa kufuata kanuni za ufugaji bora zifuatazo:                                      
Kumpatia vyakula vya ziada kwa muda wa miezi 2 mfululizo kiasi cha kilo 0.2 –
0.7 kwa siku kuanzia anapoachishwa kunyonya,

Kumpatia dawa ya kuzuia minyoo kila baada ya miezi 3 na kutoa kinga za
magonjwa mengine kama itakavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo,


Kuchanja na kuogesha ili kuzuia magonjwa mbalimbali, Kukata kwato mara zinapokuwa ndefu; na Kuhasi madume yasiyotumika kuzalisha.
Umri wa Kupandisha Mbuzi/Kondoo                                                                           Mbuzi/kondoo wakitunzwa vizuri wanaweza kupandishwa wakiwa na umri wa miezi 8 hadi 12 kwa mbuzi/kondoo walioboreshwa na miezi 18 hadi 24 kwa mbuzi wa asili kutegemea afya yake. Hata hivyo, inashauriwa wapandishwe wanapofikia uzito wa kilo 12 au zaidi na wasipandishwe mbuzi/kondoo wa ukoo mmoja.
Dalili za joto                                                                                                                       Mfugaji anashauriwa asimpandishe jike kabla hajafikisha umri wa kupandwa wa miezi 8 hadi 12 kwa mbuzi/kondoo walioboreshwa na miezi 18 hadi 24 kwa mbuzi wa asilihata kama ataonyesha dalili ya kuhitaji dume. Mbuzi/kondoo aliyezaa anaweza kupandishwa siku 30-60 baada ya kuzaa. Mbuzi/kondoo aliyeko kwenye joto huonyesha dalili zifuatazo:-
Hutingisha/huchezesha mkia,
 Hupanda na kukubali kupandwa na wengine,
Hutoa ute mweupe ukeni,
 Huhangaika mara kwa mara na kupiga kelele,
Hufuata madume,
Hamu ya kula hupungua,
 Hukojoa mara kwa mara,
Uke huvimba na huwa mwekundu kuliko ilivyo kawaida; na
Kwa mbuzi anayekamuliwa hupunguza kiwango cha maziwa
Mbuzi/kondoo apelekwe kwa dume mara tu dalili za joto zinapoonekana kwani joto hudumu kwa wastani wa siku 2 (saa 48). Chunguza tena dalili za joto baada ya siku 19 hadi 21 na kama dalili hazitaonekana tena kuna uwezekano mkubwa


kuwa mbuzi/kondoo amepata mimba. Mfugaji apange msimu mzuri wa mbuzi/kondoo kuzaa. Msimu mzuri ni mara baada ya mvua.
Utunzaji wa Mbuzi/Kondoo Mwenye Mimba                                                                   Kwa kawaida mbuzi/kondoo hubeba mimba kwa muda wa miezi 5. Utunzaji wa mbuzi/kondoo mwenye mimba ni muhimu kwani ndiyo chanzo cha kupata vitoto vyenye afya bora. Mfugaji anashauriwa kufuata kanuni zifuatazo:
Apatiwe vyakula vya ziada kilo 0.2 – 0.7 kwa siku ili kutosheleza mahitaji yake na kitoto kinachokua tumboni,
Apatiwe nyasi, miti malisho na mikunde mchanganyiko kilo 1.8 – 2.5 kwa siku.
Dalili za Mbuzi/Kondoo Anayekaribia Kuzaa                                                 Huhangaika kwa kulala na kuamka mara kwa mara,
 Sehemu ya nje ya uke hulegea,
Hujitenga na kundi na hutafuta sehemu kavu na yenye kivuli,
Hupiga kelele; na
Hutokwa na ute mzito ukeni.

Mfugaji akiona dalili hizi anashauriwa asimruhusu mbuzi/kondoo kwenda machungani, bali amtenge kwenye chumba maalum, ampatie maji ya kutosha na kumuandalia sehemu ya kuzalia.
Utunzaji wa Mbuzi/Kondoo Anayenyonyeshan                                                        Mbuzi/kondoo anayenyonyesha huhitaji chakula kingi zaidi ili kukidhi mahitaji ya mwili na kuzalisha maziwa kwa ajili ya kitoto/vitoto. Pamoja na nyasi, mikunde na majani ya miti malisho kilo 1.8 – 2.5 kwa siku ni muhimu apewe chakula cha nyongeza kilo 0.3 – 0.8 kwa kila lita ya maziwa inayoongezeka baada ya lita 2 na maji safi, salama na ya kutosha wakati wote.
Taratibu za Kuzingatia Katika Ukamuaji wa Mbuzi wa Maziw


Lengo la ufugaji wa mbuzi/kondoo wa maziwa ni kupata maziwa mengi, safi na salama pamoja na mazao yatokanayo na maziwa. Mambo muhimu ya kuzingatia ni:-
Sehemu ya kukamulia iwe safi na yenye utulivu,
 Mbuzi/kondoo awe na afya nzuri, msafi, na kiwele kioshwe kwa maji safi ya
uvuguvugu,
Mkamuaji asibadilishwe badilishwe awe msafi, mwenye kucha fupi na asiwe
na magonjwa ya kuambukiza,
 Vyombo vya kukamulia viwe safi; na
 Maziwa ya mwanzo kutoka kila chuchu yakamuliwe kwenye chombo
maalum (strip cup) ili kuchunguza ugonjwa wa kiwele.
Utunzaji wa Dume Bora la Mbegu                                                                                    Dume bora la mbegu ni muhimu litunzwe ili liwe na uwezo wa kutoa mbegu bora, kupanda na kuzalisha. Dume bora huanza kupanda akiwa na umri kati ya miezi.8 10 kwa mbuzi walioboreshwa. Katika msimu wa kupandisha dume moja liruhusiwe kupanda majike 40 hadi 50. Aidha, inashauriwa madume wenye umri wa miezi 8 – 9 waruhusiwe kupanda majike ambao ndio mara ya kwanza kupandwa.
Dume apatiwe:
 Malisho ya kutosha na vyakula vya ziada kiasi kisichopungua kilo 0.2 – 0.7 kwa siku na maji ya kutosha,
Majani ya miti malisho, mikunde na nyasi mchanganyiko na mabaki ya mazao; na
Kilo 0.45 hadi 0.9 za chakula cha ziada za nyongeza kwa siku kulingana na uzito wake na wingi wa majike anayopanda.wiki 2 kabla na baada ya kuanza kupanda.

Matunzo Mengine Kukata Mkia
Mara nyingine kondoo hukatwa mkia ili kuruhusu mtawanyiko mzuri wa mafuta katika misuli mwilini. Pia kondoo aliyekatwa mkia huwa msafi. Kazi hii ifanywe kama itakavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo kwa kutumia vyombo maalum. Inashauriwa mkia ukatwe urefu wa sentimita 2.5 – 3.8 kutoka kwenye shina la mkia wakati kondoo akiwa na umri wa siku 3 mpaka mwezi 1.
Kumnyoa Kondoo wa Sufu                                                                                                  Sufu hunyolewa wakati kondoo akiwa hai au amechinjwa.  Kwa kawaida hunyolewa miezi 6 hadi mwaka 1 ambapo sufu huwa imefikia urefu wa sentimita 15 – 20. Vifaa vinavyotumika ni pamoja na mikasi au visu maalum. Uangalifu unahitajika wakati wa kunyoa ili ngozi ya kondoo isiharibike. Unyoaji ufanyike wakati wa kiangazi na siyo wakati wa mvua, kondoo akiwa na mimba au kipindi cha majani kutoa mbegu.
Udhibiti wa Magonjwa ya Mbuzi na Kondoo                                                             Magonjwa husababishwa na vimelea jamii ya virusi, bakteria, protozoa na riketsia. Magonjwa mengine husababishwa na upungufu wa viinilishe, vitamini na protini. Dalili za mbuzi/kondoo mgonjwa ni pamoja na:-
*      Manyoya husimama,
*      Kuzubaa, kusinzia, kukohoa na kupiga chafya, Kukosa hamu ya kula na kunywa maji,
*      Kujitenga na kundi,
*      Kuvimba taya la chini,
*      Kupumua kwa shida,
*      Kutokwa na machozi na makamasi, Kuwa na upele au uvimbe kwenye sehemu ya mwili; na
*      Kutupa mimba.
Hatua za haraka za kumuona mtaalamu wa mifugo zichukuliwe iwapo baadhi ya dalili hizi zitaonekana, 




Mbuzi na kondoo wachanjwe dhidi ya magonjwa ya homa ya maapafu. Ugonjwa huu ni hatari sana na huenea kwa njia ya hewa na unaweza kusababisha vifo kati ya asilimia 60-100,
Kila baada ya miezi 6 mifugo ipatiwe kinga dhidi ya ugonjwa wa miguu na midomo na magonjwa mengine kama Kimeta, bonde la ufa, kutupa mimba na chambavu (BQ) zitolewe kulingana na ushauri wa mtalaam wa mifugo,
Kama kuna wanyama walioathirika watengwe kwenye kundi, wasisafirishwe au kuuzwa,
 •  Mbuzi/kondoo  wapatiwe  dawa  ya  minyoo.  Vitoto  vya  mbuzi/kondoo vipatiwe dawa ya minyoo vinapofikia umri wa mwezi 1. viendelee kupatiwa
dawa ya minyoo kila mwezi hadi vinapofikia miezi 5 na baada ya hapo vipatiwe dawa ya minyoo kila baada ya miezi 3 - 4; na
Zingatia usafi wa banda ili kuwakinga na ugonjwa wa kuharisha na kuharisha damu na magonjwa mbalimbali.
Utunzaji wa Kumbukumbu za Mifugo                                                                                Kuweka kumbukumbu za mifugo ni muhimu katika uzalishaji kwa ajili ya kutambua kosaafu, gharama za utunzaji na faida. Pia, humsadia mfugaji kufanya maamuzi katika uendelezaji wa ufugaji wake. Mtalaamu wa mifugo pia anaweza kutumia kumbukumbu hizi ili kumsaidia mfugaji kuboresha ufugaji wake.
Kumbukumbu muhimu zinazohitajika kutunzwa ni:-
Kumbukumbu za idadi na ukuaji wa wanyamawaliopo, jinsi zao, uzito wa  mbuzi/kondoo  kwa  kila  mwezi  ili  kufuatilia  ukuaji  wake,  tarehe  ya
kuachishwa kunyonya na idadi ya waliouzwa,
 Kumbukumbu ya uzazi zinazoonyesha tarehe ya kuzaliwa, namba yake, jinsi
yake, aina (breed), namba ya dume/jike, na uzito wa kuzaliwa,  
 Kumbukumbu  za  upandishaji  zinazoonyesha namba  ya  mbuzi/kondoo
anayepandwa, tarehe ya joto na ya kupandwa, namba ya dume lililotumika kupanda, tarehe ya joto la pili kama atarudia na tarehe ya kuzaa,





Kumbukumbu za chanjo na matibabu zinazoonyesha namba ya mbuzi/kondoo, tarehe ya matibabu, aina ya chanjo au ugonjwa, dawa iliyotumika, idadi ya waliokufa na waliopona na jina la mtaalam aliyetibu,
Kumbukumbu za maziwa zinazoonyesha namba ya mbuzi/kondoo, tarehe ya kuzaa, kiasi cha maziwa kwa siku, na kiasi cha maziwa kwa kipindi chote cha kukamuliwa, tarehe ya kuacha kukamua na idadi ya siku alizokamuliwa,
Kumbukumbu za mapato na matumizi zinazoonyesha mapato na matumizi, vitu vilivyouzwa au kununuliwa kwa siku, kiasi cha fedha unachokuwa

nacho kila wakati, kiasi cha fedha unachodai na kudaiwa.

Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU