CHANGAMOTO KATIKA TASISI



FUNGU: Mwanzo 16:6; Naye Abram akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.


1.0 UTANGULIZI:
Nawasalimu katika jina la Bwana wetu Kristo; Bwana Yesu Asifiwe binti na wana za Mungu. kwanSomo la leo linatoka katika kitabu cha Mwanzo 16:1-15, na Mwanzo 21:1-21. Mada itajikita katika tasisi iitwayo familia. Swali: Kwa nini familia iitwe tasisi? Tusome kwanza Mwanzo 16:1-15, na Mwanzo 21:1-21 kisha tuanze somo.

2.0. KIINI CHA SOMO:
Aya zote tulizosoma zinamhusu familia ya Abram ambaye ni Ibrahimu pamoja na mkewe Sarai ambaye ni Sara. Familia ya Ibrahimu na Sarai ilikuwa na mjakazi (mfanyakazi au dada wa kazi) aitwaye Hajiri mwenye asili ya Misiri.

Familia hii ya Abram na Sarai haikuwa na mtoto, toka wameoana. Kadri miaka iliposonga, Serai akamshauri Abram mumewe azae na kijakazi aitwaye Hajiri (Mwanzo 16:2-4).  Hajiri alijifungua mtoto wa kiume aliyeitwa Ishimael (Mwanzo 16:11).

Japo Sarai alimruhusu mumewe kuzaa na kijakazi, matokeo hayo hakuyakubari. Baada ya Mungu kufanya agano na Ibrahimu, Mungu alimpatia mbaraka wa mtoto kupitia kwa mkewe Sara (Mwanzo 21:1-3). Kuzaliwa kwa Isaka, Ibrahimu alikuwa na miaka 100 na Sara miaka 90.

Hivyo, baada ya Sara kuzaa, familia ikawa na watoto wawili ambao ni Ishimaeli kutoka tumbo la Hajiri (mjakazi) na Isaka kutoka tumbo la Sara mke halali wa Ibrahimu. Watoto hawa ndio chanzo cha mgogoro uliowatenganisha makazi baina ya Hajiri na Sara (Mwanzo 21:8-10), ambapo Sara alifukuzwa pamoja na mwanae aitwaye Ishmaili.

Kupitia familia ya Ibrahimu na Sara, kunamambo machache ya kujifunza:

1. Ibrahimu mfano wa mwanamume anayesikiliza ushauli wenye tija kutoka kwa mkewe (Mwazo 16:2-3), mwenye kusimamia haki (Mwanzo 16:6, 21:10-11).

2. Sara mfano wa mwanamke mwenye kigeugeu, (Mwanzo 16:5); mwenye jeuri na asiye na subira (Mwanzo 21:8-10):

3. Mara zote, Mungu hamuachi mtu anayeonewa pasipo kutendewa haki (Mwanzo 16:6-15).

4. Mungu mwenye uweza wa kuwapa watoto hata walio vikongwe (Mwanzo 17:15-17).

5. Ibrahimu kielelezo cha baba mwenye familia anayefuata maelekezo ya Mungu nje ya utashi wake mwenye (Mwanzo 21:10-12).

6. Ibrahimu mfano wa baba mwenye huruma katika familia (Mwanzo 21:14).

7.  Mungu husikia sauti ya yeyote anayemwita katika matatizo (Mwanzo 21:15-20).

8. Heshima ya mama wa familia hushuka pale jukumu lake kwa mumewe linapochukuliwa na kijakazi (Mwanzo 16:4).

9. Uadui wa wazazi huhamia pia kwa watoto kwani chuki hupandikizwa juu yao (Mwanzo 21:9).

10. Mama mwenye upendo hawezi kuvumilia kumuona mtoto wake akifa huku akiona (Mwanzo 21:15-16).

3.0 HITIMISHO:

Hareluyaaaa!! Bwana awabariki

Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU