FAIDA ZA KUTOFANYA UZINZI AU NGONO HADI WAKATI WA NDOA
Yampasa kijana wa kike au wa kiume aliye Mkristo
ajiepushe kushiriki ngono. Ni vyema vijana wakahakikisha kutunza usafi wa miili
yao na kuheshimu utukufu na usafi wa tendo la ndoa. Vijana wa kike na wa kiume wafanye mambo yafuatayo ili
kuepuka kujamiiana kabla ya ndoa:
1. Waepuke kuwa katika mazingira hatarishi yanayoshawishi
kufanya zinaa, mfano sinema na sehemu zingine za starehe.
2. Waepuke marafiki wabaya katika kundi rika ambao
wanamatendo mabaya.
3. Waepuke utembeaji wa usiku bila sababu zo zote katika
mazingira yasiyo salama kwao.
4. Waepuke kuangalia au kusoma vitu vinavyohusu mapenzi na
ngono ili wasiziamshe hisia zao.
5. Waoe haraka kama umri umefika ili kuiepuka zinaa.
6. Wajihusishe na programu za kanisa juu ya ibada na
kumtumikia Mungu ili muda wote waufikirie utukufu wa Bwana.
7. Wapende kusoma na kulitafakari neno la Mungu ili Roho wa
Mungu akae ndani ya maisha yao.
8. Wajue kufanya ngono kabla ya ndoa ni dhambi na wanavunja
amri ya saba ya Mungu inayokataza kufanya uzinzi.
9. Wajiheshimu katika mavazi, mazungumzo na mienendo mizima
ya maisha yao ili wasimpe nafasi Shetani.
10. Wapende kufanya mazoezi hususani ya viungo vya mwili ili
kuondoa hisia na mawazo mabaya katika fikra zao.
Faida
za Kujilinda Bila Kutenda Ngono Hadi Wakati wa Ndoa
Kujitunza na kujilinda bila kutenda tendo la
ndoa kwa vijana wa kike na wakiume kunafaida zifuatazo:
1.
Kuwa mwenzi unayefaa katika ndoa.
2.
Huamsha ari na hisia za kujithamini.
3.
Ni kipimo kizuri cha uwezo wa kuzuia au kuzimudu hisia.
4.
Hujenga uwezo wa uvumilivu wa kihisia.
5.
Hutoa nafasi ya kujikita katika mambo na malengo ya msingi ya maisha bila
kuingiliwa na tamaa za mapenzi kabla ya ndoa.
6.
Hujenga taswira na msingi wa uaminifu kwa kijana.
7.
Huepusha maumivu ya mapenzi kwa vijana kabla ya ndoa.
8.
Husaidia kutunza via vya uzazi mpaka vikomae ili kuwa tayari kwa ajiri ya
kushiriki tendo la ndoa na kuzaa pindi kijana awapo ndani ya ndoa.
9.
Huepusha kuharibu hisia na ubongo katika kufikiria mapenzi kabla ya ndoa.
10.
Huepusha utumwa wa ngono kabla ya ndoa kwa vijana.
11.
Huepusha utoaji wa mimba zitokanazo na kushiriki tendo la ndoa bila malengo ya
kuzaa.
13.
Huondoa hofu kwa vijana juu ya kuhisi maambukizi ya magonjwa ya zinaa na Virusi
Vya Ukimwi kwa kushiriki ngono kabla ya kuoa au kuolewa.
14. Huwaepusha
vijana dhidi ya kupata mimba katika umri mdogo.
Nini
cha Kufanya Endapo Kijana Ameshiriki Uzinzi (ngono) Kabla ya Ndoa?
Kijana wa kike au kiume endapo atakuwa
ameshiriki ngono aidha kwa makusudi au bahati mbaya (ni mara chache sana bahati
mbaya hujitokeza) yampasa afanye mambo yafuatayo ili awe safi mbele za Mungu na
kujipanga kwa ajili ya kushiriki awapo ndani ya ndoa tu:
1.
Fanya toba ya dhati kwa
Mungu kisha acha kabisa.
2.
Badirisha mienendo na
mitindo yako ya maisha iliyokuwa inakuvuta kufanya uzinzi.
3.
Epuka makundi rika yaliyo
maovu na makundi yenye tabia mbaya na hatarishi kwako.
4.
Jilinde na vitu
vinavyosababisha kuleta hisia za kimapenzi mfano sinema, tamthiliya, program za
TV za mapenzi, majarida na vitabu vya mapenzi.
5.
Epuka kutembelea
mazingira yenye ushawishi mkubwa wa kubadili hisia zako na kutamani kufanya
mapenzi.
6.
Tenga muda mwingi kwa
ajili ya kujifunza neno la Mungu kwa kusoma Biblia na kushiriki ibada na
programu mbalimbali za kanisa.
7.
Pambana kuzidi kuwa
safi siyo kwa uweza wako pekee bali mkabidhi tatizo linalokusumbua Yesu Kristo
aliye mshindi wa dhambi na hutushindia pia.
8.
Chunga mdomo wako katika mazungumzo na aina ya
mavazi unayovaa maana kwayo huashiria urahisi na husadifu tabia ya mtu.
9.
Achana na tabia ya
kuangalia picha na mikanda ya watu walio uchi au nusu uchi maana huathiri
ubongo na hisia.
Madhara ya Kuharakisha Ngono Kabla ya Ndoa
Mtumishi wa Mungu
Gibsoni Ezekieli yeye anasema “vijana wote wa kike na wakiume yawapasa kujua
kuwa hakuna mstari unaotenganisha kutoka ujana kwenda utu uzima. Namna
unavyofanya mambo yako ukiwa kijana huathiri utu uzima wako. Tabia unazoendekeza wakati wa ujana
zitakufuata utakapokuwa mtu mzima. Vijana wengi wamekuwa na tabia ya kuwa
na mazoea mabaya, hususani juu ya kutoheshimu na kutilia umakini suala la tendo
la ndoa. Mazoea ya kubadirisha wasichana na wavulana kama nguo kwa kujiaminisha
kuwa wataacha kufanya hivyo endapo wataoa au kuolewa na kuwa katika ndoa zao”.
Anaendelea kusema
kuwa “Mazoea mabaya ni muuaji anayeonekana hana hatia mwanzoni, na vijana
hujifariji nitakapooa au kuolewa kwa sababu nitakuwa na mtu wa kunipoza haja
zangu nitaacha uzinzi na uasherati. Hawajui ya kuwa utegemezi au uraibu
(addiction) humfanya aliyezoea kuhitaji kufanya hivyo mara kwa mara. Pia
husababisha kitu ambacho wataalam wa saikolojia hukiita Objectification of women and men,
yaaani mwanamke au mwanamume anakuwa kama ni kitu tu cha kumridhisha mwanamume
au mwanamke. Mwanamke au mwanamume anakuwa si mtu bali kitu cha
kutuliza haja za kingono katika maisha”.
Kama tulivyoona
katika nukuu ya maelezo ya mtumishi wa Mungu Gibson Ezekiel; hivyo basi, mazoea
ya ngono kabla ya ndoa kwa wasichana na wavulana huleta athari badaye katika
nyanja zifuatazo:
1.
Kutokana na mazoea ya kubadirisha badirisha au kufanya ngono mara nyingi na kwa
hali ya juu kabla ya ndoa, mwanamke au mwanamume huonekana kama “sex machine” katika ndoa kwa sababu tendo hilo limejengeka
katika mawazo na fikra kama starehe na haja ya msingi kila wakati. Inapoonekana mke au mume hawezi kuwa
tayari muda wote kutenda tendo la ndoa kwa mara nyingi inavyotakiwa kufanya
kama miongoni mwa mmoja wa wanandoa kama alivyozoea kufanya mara kwa mara hapo kabla
ya ndoa, mmoja hutoka nje ya ndoa ili kukidhi haja yake ya tendo la ndoa.
2.
Yawezakuwa mke au mume huyo aliyepatikana kuwa tofauti na wale aliowazoea
kushiriki nao ngono hapo awali. Kwa ufupi unaweza ukaoa au kuolewa; mkeo au
mumeo asikupe ushirikiano kama ilivyotazamiwa kutokana na mazoea. Uhitaji
mwingi kati ya mmoja wa wanandoa itapelekea kuchepuka kwa sababu ya kushindwa
kuvumilia hisia endapo mwezi ameonekana kulegalega na kutokukidhi haja ya tendo
la ndoa aidha, kwa sababu ya majukumu na uchovu wa kazi au ugonjwa au ujauzito
kwa mwanamke. Ndiyo maana wanandoa wengi huendeleza tabia zilezile za kuwa na
wenzi wengine wengi hata baada ya kuoa au kuolewa, kwani hitaji lake lipo juu
sana. Kwa sababu hiyo, tabia ya uzinzi hujitokeza kwa wanandoa walio wengi.
Jambo la
kuzingatia:
Imeandikwa kuwa mume au mke kwa pamoja wasinyimane, tena mume ana mamlaka juu
ya mwili wa mkewe na mke ana mamlaka juu ya mwili wa mumewe. Lakini Paulo
akaonya ya kwamba, wanandoa wafanye tendo la ndoa kwa kiasi ili wasije
wakajaribiwa na Shetani katika hilo na kutenda dhambi (1Wakorintho 7:1-5).
Comments
Post a Comment
Thanks for viewing and passing through NMEE blog. Keep following the blog