MAISHA NA TABIA YA TAI CHACHU NA SOMO KWA MAISHA KWA MWANADAMU



Utangulizi
Kila kiumbe kilichopo duniani hapa cha weza kuwa fundisho zuri au baya katika maisha yetu kulingana na jinsi kilivyotumika katika lugha ya picha. Wanyama kama Sungura na Tumbili; ni wanyama wanaowakiliaha wanadamu wenye tabia za ujanjaujanja au wajuaji sana. Simba anasimama kwa niaba ya watu nguli, wababe na wakali wenye uwezo na mamlaka. Fisi anasimama kwa niaba ya watu warafi. Twiga kwa watu wenye malingo na mikogo. Njiwa anasima kwa niaba ya utaktaifu, upendo, uaminifu na upole kwa watu. Nyoka anasimama kwa niaba ya watu wenye tabia ya uongo; wachonganishi. Ndege aina ya kasuku kusimama kwa watu wenye kuongea sana.

Wasifu au Sifa Na Tabia Za Tai
Wanyama na viumbe mbalimbali wanapotumiwa katika lugha ya picha hutoa na huashiria tabia na mienendo ya maisha ya kila mwanadamu. Kwa sehemu kubwa nitazungumzia katika ‘wasifu na mwisha ya ndege Tai’ kama chachu na somo kwa mwanadau. Ndege tai yupo katika aina au makundi yanayozidi 55. Katika kufuatilia taarifa na mandiko mbalimbali, nilibaini kuwa; Tai ana wasifu ufuatao ambapo baadhi yake tutajifunza na kupata masomo mengi katika maisha yetu hapa duniani:
1)    Tai anaurefu unaofika nchi 30(vertical height) anapokua amesimama.
2)    Tai anaidadi ya manyoya kati ya 7200 kwnye mwili wake
3)    Tai anamwendo kasi mkubwa sana kuliko ndege wote (48 hadi 89 kwa saa).
4)    Akiwa ametanua mabawa, tai ana urefu (horizontal height) wa sentimita kati ya 200 hadi 243; saw na futi 6 had 7.9.
5)    Uwezo wa tai wa kuona mbali ni mara tatu hadi nne ya uwezo wa mwanadamu
6)    Tai hupunguza joto kwa kutanua mbawa zake pale anapokuwa angani
7)    Tai anamisuri takribani 175; miguu pekee inamisuli 35. Kwa asilimia 40 hadi 60 ya uzito wa tai, umechangiwa na misuli iliyopo katika mwili wake.
8)    Tai anauwezo wa kubeba windo lenye uzito wa kilogram 5 hadi 7 au zaidi kwenda angsani
9)    Anauwezo wa kufika umbali zaidi ya futi 10, 000 kwenda angani
10)                       Tai wanaoishi kwenye sehemu za maji, wanauwezo wa kuogelea vizuri juu ya maji
Kutokana na uwezo na sifa njema za wasifu wa tai; nchi baadhi na tasisi nyingi zinatumia picha ya tai kama alama na kielelezo pekee cha uimala, uwezo, ubora na uthabiti. Taifa la marekani ni miongoni mwa taifa linalotumia nembo ya tai. Sifa au tabia bainishi za tai ndizo ambazo ni fundisho jema kwa maisha ya mwanadamu; zimpasazo kuzijua, kuzitambua na kujifunza kwazo kama ifuatavyo:
1.     Tai anauwezo mkuba wa kuona mbali zaidi
2.     Tai anapaa umbali mrefu kwenda juu  kuliko ndege wengine
3.     Tai haogopi dhoruba awapo juu angani (hufurahia dhoruba)
4.     Tai ni mwepesi sana na anaspidi kubwa
5.     Tai hapendelei kula mizoga
6.     Tai hujenga ndoa yenye upendo na yenyekuaminiana
7.     Tai hulea na kufundisha watoto katika jujiamina na kuvumilia
8.     Tai anauhakika wa kuishi kwa muda mrefu
9.     Tai ananguvu na bidii
10.                        Tai ni mbunifu katika kupambana na adui zake

SURA YA KWANZA
UWEZO WA KUONA MBALI
Kiwawaida tai anafika umbali mrefu zaidi kuliko ndege wengine. Tai anafika umbali zaidi ya duti 10, 000 kutoka kwenye uso wa dunia. Japokuwa anakuwa umbali mkubwa sana kutoka uso wa dunia, lakini tai anauwezo mkuba wa kuona hadi ndani ya maji yam to au bahari pamoja na kwenye vichaka au nyasi. Kuona kwa tai hata awapo mbali sana angani juu; humfanya ajue na atambue wapi kitoweo kilipo na wapi kuna adui. Hivyo tai hujua na huona kabla ya adui au kitoweo kubaini kwa sababu tai huwa mbali sana. Uwezo wake tai wa kuona mbali humpelekea yeye khuona kwanza kabla yeye hajaonwa.

Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Mwanadamu yampasa awe na uwezo wa kuona mbali pale ambapo wengine hawajapaona bado.  Kuona kwanza ambapo wengine hawajapaona ni lazima kuwa na njozi au ndoto inayolenga mbali kwa kuyafikia malengo ya badae. Kuona mbali hakuji bila kuwa na mikakati kuweza kuifikia ndoto yako. Binadamu yeyote mwenye kuhitaji kuyafikia yale ayatarajiayo; yampasa kupanga mikakati (mission) ya kufanya njozi/ndoto (vision) yake itimie, sawa na tai aonapo kitoweo toka juu mbali na hupanga mikakati ya kukifikia kitoweo hicho ili atomize haja au adhima ya njaa yake.

Hivyo, mwanadamu asiye kuwa na mikakati ili atomize ndoto yake atakuwa anaishi maisha ya kubahatisha au kwa kufanya yale ambayo wengine wanafanya kwa jinsi ileile (atakuwa hajaona mbali). Kila mtu yampasa awe na njozi maishani mwake na ajitahidi sana kuifanya njozi hiyo itimie. Kuona mambo mapya ni kubuni mambo mapya ambayo hajafanyika bado. Kutokuwa mbunifu ili kuifikia njozi kunamnyima mtu mafanikio, kwa sababu hajalenga mbali.  Tuwe na njozi ili tuzifikie fursa katika maendeleo ya maisha na taifa letu juu ya misingi ya wakati na sayansi na teknolojia.
Haijalishi tupo mbali kiasi gani katika umri, elimu, au maendeleo; twaweza kuona  katika njozi na kufanya mikakati na kuyafikia malengo yetu kwa jinsi na namna yoyote. Umbali wa aina yoyote sio sababu ya kutukatisha tama. Fanya kama tai kupanga kukifikia kitoweo ukitarajiacho kukifikia. Kukifikia kitoweo hicho yakupasa uwe na njozi, mikakati, malengo, ujuzi, ufaham, uelewa, mtazamo chanya na bidii katika kutenda kazi. Kamwe tusiwaze kushindwa, maana kupanga kushindwa ni kupanga kushinwa kuyafikia malengo yaliyo katika njozi na ndoto yako.

SURA YA PILI
UWEZO WA KWENDA MBALI KULIKO WENGINE
Urefu na ubali awapo tai, huwezi kuona aina nyingine ya ndege. Zaidi ya futi 10, 000 kwenda juu angani kutoka kwenye uso wa dunia ni urefu mkubwa sana ambapo ndege wengine hawawezi kuumudu kulingana na changamoto za misukosuko, upepo mkali, mvua, baridi kali sana, kukokasa uwezo wa kuona chini, maana ni juu sana. Kwa hiyo maisha ya tai ni ya kusitajabisha sana, kwani yeye huwa juu zaidi ya ndege wengine wote. Lakini hata awapo juu zaidi hapotezi uwezo wake wa kuona mbali.

Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Kuna msemo unasema kuwa “ndege wenye tabia na manyoya ya rangi ya aina moja hupaa pamoja”. Ukanda wa juu alipo tai huwezi kukutana na ndege wengine zaidi ya tai pekee. Kwa mtu aliyemakini lazima afanye, afikiri na atende zaidi ya pale wengine walipofikia. Kufuata mkumbo na kuiga mienendo, tabia, jinsi ya kutenda, kufikiri na kuiga maisha ya watu wengi, hakuwezi kukuletea tofauti yoyote zaidi ya kuishi kwa mkumbo.  Jua kuwa kila mtu ni wa pekee kwa jinsi ya ajabu alivyoumbwa. Kuepuka mkumbo na kunakili maisha na mienendo yaw engine; yatupasa kuwa tofauti au zaidi ya wawazavyo, waishivyo, wafikiriavyo na watendavyo. Kama tai jinzi walivyo wa pekee katika ndege wengine; na sisi tuwe wa pekee kwa kila namna.

 Kama alivyo tai katika kuumbwa na Mungu; pia binadamu anamjumuiko wa maajabu na vipawa na vipaji vingi ambapo Mungu kampatia kwa jinsi ya ajabu na kustaajabisha. Binadamu yeyote akitulia vyema katika kufikiri, anaweza kufanya mambo makubwa katika maisha yake endapo atakubali kutumia uwezo mkubwa na vipaji alivyopewa na Mungu. Mungu kampa mwanadamu akili na uwezo mkubwa kuliko viumbe vyote alivyoviumba. Kutojitambua kwa mwanadamu ndicho kikwazo kikubwa cha kutokuwa na upekee.


SURA YA TATU
KUTOOGOPA DHORUBA NA CHANGAMOTI
Kutoogopa kwa tai juu ya dhoruba awapo juu angani ni mojawa ya sifa ya pekee kuzipenda na kuzimudu changamoto . Zipo changamoto nyigi anazokutana nazo tai pale awapo juu angani. Mfano wa dholuba au changamoto hizo ni; mvua, baridi, ngulumo, radi na upepo mkali.  Nyakati mbaya za dholuba yeye tai husherekea, hufurahi na wakati huu hutulia na hutandaza mbawa zake bila wasiwasi. Wakati tai ufurahiapo dholuba au changamoto, ndege wengine hukimbia ili kujiokoa.

Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Wanadamu wengi mara zote tumekuwa tukipatwa na hofu, mashaka, wasiwasi wkutwapo na jambo gumu na zito (changamoto). Mtu mwenyekuziogopa changamoto hawezi kuwa na uwezo wa kuthubutu hata kidogo, maana maisha yake yamejaa mashaka na hofu. Woga ni adui mkubwa wa mafanikio ya binadamu. Kama pangelikuwa na watu wengi wanaothubutu kuzikabili changamoto bila kukata tama ndani ya nchi zinazoendelea, umasikini ungelitoweka katika nchi hizo.

Wakati wa changamoto, ndilo wakati wa kufikiria na kupumzisha akili ili kupata jambo jipya na mbadala au mwarobaini wa kutatua changamoto zinazokukabili. Hofu, woga na kutojiamini wakati wa matatizo au changamoto zozote humkwamisha mwanadamu kupiga hatua. Kuna msemo unasema kuwa “Uoga wako ndiyo umaskini wako”. Tabia ya uoga hujenga hofu na tabia ya kutojiamini. Kutojiamini ndiko kunakoleta hofu ya kutokuthubutu.Godbless Lema (Mbunge Arusha mjini) yeye husema “uoga ni dhambi”
Endapo maisha yetu yakitawaliwa na hofu, hatuwezi kufanya wala kupiga hatua katika jambo lolotete. Uoga kwa mwanadamu humsababishia; hofu, mashaka, kukosa imani, kutojiamini na kitete  katika kulikabili jambo fulani au kutenda kitu. Uoga ulikithiri huzaa magonjwa ya mpoyo na kifikra. Msingi wa kujiamini kwa mwanadamu hunzia katika malezi ya mtu toka utotoni, na sio vinginevyo. Tuwalee watoto wetu katika kusimamia na kujiamini kwa kile kinacho wakabili kwa muda.

SURA YA NNE
TUWE WEPESI NA SHAPU KATIKA KUTENDA
Tai ni mwepesi, shapu katika utendaji na wmenye kasi kubwa katika kuendea jambo fulani. Tai hupaa kwa mwendo wa kasi wa maili 30 hadi 55 kwa saa, sipidi anayorudia aridhini (diving speed) ni maili 100 kwa saa, ambayo ni sipidi isiyo ya kawaida. Ushapu na kasi kubwa, ni sifa inayomtabanaisha tai kuwa tofauti na ndege wengine. Wepesi na ushapu wa tai hutokana na kufikiria kwa kasi, maana kufikili kunaanza kabla ya kutenda. Tai anauwezo wa kukamata nyoka au samaki, ashukapo kwa kasi toka angani juu, hivyo nyoka au samaki hushindwa kujiokoa kwa sababu ya ukasi na ushapu wa maamuzi ya tai tofauti na samaki au nyoka. Sio kwa samaki tu au nyoka pekee, hata vitoweo (viumbe) vingine hukamatwa kwa jinsi hiyohiyo.

Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Mara zote mtu asiyekuwashapu katika kufikilia, hawezi kufanya maamuzi ya ghafla na haraka. Uwezo wa kufikiri huendesha maamzi na kutenda; hivyo, wale wanaofikiria polepole huchelewa kutoa maamuzi na hata utendaji wao wa kazi huwa wa polepole sana. Kutembea na kutenda hutegemeana na ushapu wa mtu katika kufukiria. 

Jambo lolote lampasa mwanadamu kufanya hima na kwa ushapu au kasi ili kulikabili na kulikamilisha kwa wakati muafaka. Haina haja ya kuchelewa, maana wakati hausubiri na hautoshi daima. Lipaswalo kukamilika leo lisingoje kesho kwani muda sio rafiki, na hiyo kesho haijulikani itakuwaje. Kukosa ushapu na umakini wa kutoa maamuzi ya haraka, hupelekea kutofanikisha jambo kwa muda mahususi. Katika kazi na biashara; ushapu na wepesi ndio utakaomwezesha mfanya kazi au mfanya biasha ahudumie wateja wengi au kufanya kazi nyingi ili kuokoa muda na kuwahisha huduma.
SURA YA TANO
TUWE WATAFUTAJI ILI TUSILE MIZOGA
Tai hali mizoga bali hula kipaya (yaani freshi). Sifa na tabia mojawapo nyingie ya tai ni kutokula mizoga (vimudu). Tabia hii ni ya pekee kaw sababu anajituma na kujibidisha katika kutafuta vitoweo kwa nguvu zake mwenyewe. Tai sio mzembe, ni mwenye bidii kati utafutaji au uwindaji wa chakula chake mwenye. Hana tabia ya kula vitoweo vilivyojifia maana sio salama kiafya. Pia hali masazo kwa sababu anaouhakika wa kufanikisha kupata chakula. Kujiamini kwa tai ni kutona na bidii na uwezo mkubwa alionao wa kutafuta kwa nguvu na maarifa yake aliyonayo. Hategemei kutafutiwa au kula vyakula vya bila Jasho Lake.

Wakati tai anapokuwa amekwama kupa kitoweo, marachache huchukua mfupa wa kiumbe chocho huupasua kwa jitihada zote, kasha hula zile “bone barrow’ zilizo ndani katikati ya mfupa huo. Hata hivyo kuupasua mfupa kwa kuruka juu kasha anabamiza kwenye jiwe sio shughuli nyepesi, inahitaji ushupavu na biidi iliyotukuka. Iwe katika kuwinda au kupasua mifupa; tai hufanya kazi kwa biddi ili kufanikisha mlo wake.

Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Maisha siyo rahisi, hayanyooki siku zote; tunatakiw tuwe imara muda wote katika kutafuta ili kufanikiwa. Hakuna ambaye hafurahii kufanikiwa kwa jasho lake mwenyewe. Wengi wanaposhindwa kufanikiwa humlaumu Mungu, na husahau kuwa; kumuomba Mungu pekee bila kujibidisha hakutoshi, bali yampasa afanye kazi kwa bidii na moyo wake wote. Kila mwanadamu anasehemu kubwa sana ya kufanya ili kuleta maendeleo na mafanikio binafsi.

Kila jambo linafanywapo kwa bidii zote na moyo wote huleta uhakika wa mafanikio hapo baadaye.  Jambo la kufanya kazi kwa bidii ni jambo la msingi katika kuyatafuta mafanikio. Mafanikio hayaji kwa mtu kwa kuendekeza kulala, kuzulula, kushinda kwenye vijiwe na kupenda starehe bila kujibidisha katika kufanya kazi. Mwanadamu akifanya kazi kwa bidii na kuipenda kazi yake, atafanikiwa kwa namna ya ajabu sana.
Kufanya mambo makubwa hakuji hivihivi bila kufanya kazi kwa bidii zote na kujituma kwa moyo wote. Tuwe na tabia ya tai ya kutafuta na kutumia vitu tulivyovitafuta kwa jasho letu wenyewe, na wala sio kutumia vya watu wengine. Binadamu hawezi kuwa na uchungu wowote juu ya mali, vitu au mafanikio kama hajavitafuta kwa jasho lake.  Kutumia mali au vitu vya watu wengine ni aibu na huzaa masimango mengi; uhuru haupo kwani sio vyako, bali ametafuta fulani.
Wavivu na wazembe hawaishi kulalamika na kuhitaji misaada kila kukicha, hali kwamba hana ulemavu na nguvu anazo tena mwenye afya tele. Hakuna mtu wa kumletea mafanikio mtu mwingine tofauti na yeye mwenye kujishughulisha, kujituma na kufanya kazi kwa bidii kwa moyo wote.  “Asiyefanya kazi na asile” ni msemo tuliouzoea masikioni petu na kuuona ni wakawaida tu. Msemo huo ukikaa ukautafakari, ni msemo wenye maana pana sana katika namna ya kumtia mtu  hamasa ya kutafuta vya kwake, na sio kudandidandia vya watu wengine katika kutumia kama kupe au chawa (parasites) waishivyo kwa kutegemea viumbe wengine ili maisha yasonge mbele.
Angalau asilimia 40 tu ndani ya taifa (Tanzania) tukiwa watafutaji kama tai, tutaweza kuwa mbali kimafanikilo.  Sehemu kubwa ya watanzania sio wazalishaji, nitegemezi. Yaani ukichukua wanafunzi, watoto, wazululaji, wafungwa, wazee, wakinamama wa nyumbani, na wazembe wengine wengi, twaweza kuwa na asilimia 10 hadi 25 tu ya wanaozalisha na kulisha taifa letu. Sisi kama Wazarendo wa taifa, tukiamka, tunaweza kupiga hatua. Tusilalamikie serikali hali kwamba hata kwa mtu mmoja mmoja anao wajibu wa kulisukuma taifa, aidha kwa maendeleo ya yeye binafsi au taifa kwa ujumla.


SURA YA SITA
TUWE WENYE UPENDO NA WAAMINIFU KATIKA NDOA ZETU
Tai hujenga ndoa yenye upendo na yenyekuaminiana. Maisha ya tai katika kujenga mahusiano au ndoa ya mke na mme kabla ya kutafuta watoto, huanza na mitihani au majaribio ili kuthibitisha upendo wa kweli. Kipimo hutolewa na tai jike ili kujua kuwa tai dume atakuwa na upendo, utiifu na mwaminifu katika ndoa. Tai dume anapofudhu mitihani kadha wa kadha ya kupima uaminifu na upendo wake kwa tai jike, ndipo hatua na mikaka ya kupanga kuzaa pamoja hufuatia.

Tai (bibi na bwana) wanapotaka kukutana (kuzaa), tai dume humfuata tai jike juu, kasha tai jike agunduapo adhima ya tai dume ndipo neye (tai jike) hushuka chini na kuchukua gome la mti, jani au tawi na kupaa nalo juu kwa tai dume. Tai jike amfikiapo tai dume, ndipo huliachia hilo gome (jani, tawi) na kudondoka kuelekea chini; hivyo tai dume huliendea kwa kasi  na kuli kamata kasha kulirejesha kwa tai jike. Zoezi hili hufanyika mara kadhaa takribani muda wa nusu saa hadi lisaa limoja ili tai jike kumkubali tai dume na kukutanA kimwili (kujenga ndoa).
Baada ya tukio la kushirikiana kwenye tendo la kuzaa, tai jike anapotaka kutaga mayai (kuzaa); tai dume na tai jike hushirikiana katika kutafuta eneo la juu ya mlima ili kuanzisha makazi (kiota/kichali) ambapo maadui hawawezi kufika kwa urahisi. Kuweka makazi juu ya ncha ya mlima, kwa sababu za kiusalama na urahisi kuonekana kwa kila akati tai awapo juu angani.
Katika ujenzi wa kiota, tai dume huenda kutafta miiba, magome, miti, nyasi na ngozi. Kwa kushirikia; tai jike na tai dume huanza kujenga kwa kutanguliza miiba na kufuatiwa na magome ya miti, nyasi na mwisho kabisa ngozi inayofunika vyote vilivyotangulia.  Kiota hicho hufunikwa kwa miiba mingi kukizunguka ili kuzuia maadui kukifikia kiota hicho.
Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Majaribu huja ili kutupima imani zetu. Ni vyema tukawa na muda wa kutosha wa kupima upendo wa wachumba zetu na rafiki zetu wa karibu, ili kujua kama wanaoupendo wa kweli juu yetu. Kutobainisha upendo na uaminifu wa mtu wako wa karibu ni jambo ambalo sio salama sana katika maisha yetu. Mtu mwenye upendo wa kweli ni yule mwenye uwezo wa kuzibeba huzuni, shida, matatizo na changamoto zetu. Rafiki wa kweli na mchumba wa kweli ni Yule ashilikiye na kuvaa viatu vyetu vya maisha yetu ya kila siku.

Kuanza uhusiano (kuoa na kuolewa ) na mtu ambaye hujajihakikishia upendo na uaminifu wake juu yako ni kujipalia moto hapo badae; maana wapo ambao huanzisha mahusiano na mtu fulani kwa kutimiza haja zao za matamanio au kuchuma kitu fulani katika mtu fulani. Kwa wale wanaoelekea katika safari ya maisha ya ndoa na ambao bado wanatafuta; kipindi salama cha kumchuguza tabia mtu, ni kipindi cha urafiki na kidogo kipindi cha uchumba. Mtu ukisha mtamkia (wanamme) kuwa unataka kumuoa (mwanamke) atajifanya kuficha tabia zote mbaya kwa maana ya kuficha makucha, hadi umuoe. Akifika kwenye ndoa (mmeshaoana) anakunja makucaha yake; ndipo kujuta kwa majuto mjukuu huja.
Ukiweza kumpima kiwango cha uaminifu mwezi wako talajali wa maisha, utakuwa umejihakikishia ndoa imara na yenye upendo daima. Huwa ni vigumu kubadirisha tabia ya mtu mkiwa kwenye ndoa. Wakati wa kupima, kujua na kutibu tabia mbaya za mwenzi, huwa ni wakati wa urafiki na uchumba pekee. Ni nadra sana kutibu tabia ya mwenzi mkiwa mmeoana, tofauti hivyo, tegemea ndoa yenye maisha ya kuvumiliana; kila kukicha aheli ya jana.
Ndoa yenye upendo wa kweli, ni yenye umoja ambao umejengwa katika misingi ya kusaidiana, kushirikiana kwa namna moja au nyingine. Kusaidiana na kushikishana kupo kwa namna nyingi sana; mfano kazi za nyumbani, kupanga bajeti, kufanya maamuzi, vipato vya familia, mawazo ya kila mmoja. Ndoa ni mwili mmoja hivyo lazima wanandoa wawe kitu kimoja katika kutenda na maamuzi yao. Hakuna aliye bora, kila mmoja humtegemea mwenzie ili kuijenga himaya ya familia kwa wanandoa.
Katika ndoa, lazima kuhakikisha usalama na ulizinzi wa familia na watoto kwa ujumla. Wanandoa lazima wlinde amani na usalama wa familia zao. Katika familia lazima pawepo na usalama wa kiafya, uwepo wa amani, uhakika wa furaha kila muda, ulinzi wa Mungu na uhakika wa chakula na mahitaji mengine ya kifamilia.  Amani katika ndoa huletwa na upendo wa kweli. Upendo usiochosha, upendo wa dhati na kweli; upendo usio wa hofu ya mwingine. upendo wa pekee ni upendo ulioambatana katika kumcha na kumtumainia Mungu pekee kwa kila jambo.
Familia yenye upendo ni ile yenye kubeana madhaifu na mapungu kwa wanandoa, kutiana moyo na sio kukatishana tama; yaani baba anafanya, mama anatia moyo ili mme wake asonge mbele. Tujifunze yaliyo makuu na mema kutoka katika upendo wa kimbingu, ili tuyaishi mema ya ndoa zetu zilizotayali au tuzitarajiazo.

SURA YA SABA
TUWALEE WATOTO KATIKA UVUMILIVU, KUJIAMINI NA KUJITEGEMEA
Tai hulea na kufundisha watoto wake katika jujiamini, kuvumilia na kujitegeme katika maisha yao. Baada ya watoto wa tai kuwa wakwisha kutotolewa; mama yao huwatoa kwenye kiota, lakini watoto hurudi tena kwenye kiota. Mama wa watoto hufanya jambo moja ambalo huwafanya watoto watoke kwe kiota. Jambo hilo huwa ni kutoa ngozi, nyasi, magome ya miti katika kiota, na hubakisha miiba ambayo huwachoma watoto na kujihisi maumivu kwa kiasi kikubwa.

Lengo la mama wa watoto wa tai sio kuwaaumiza, bali kuwafanya watoto watoke katika kiota ili waanze maisha mapya, pamoja na kuzoea maisha mateso na raha.  Baadae mama yao huwasukuma pembeni ya kilele cha mlima ili wadondoke. Kabla watoto hawajaanguka, mama yao huwadaka kwa mbawa zake. Kitendo hicho cha kuwasukuma hufanyika mara kadhaa hadi watoto wote wajue huruka sawasawa. Mafunzo ya kuruka, hufanyika kwa mantiki hiyo ili kuondoa hofu na kujenga kujiamini.
Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Mara nyingi mateso hutupa ujasili pamoja na uvumilivu. Kupitia magumu katika maisha hujenga uvumilivu na kuzikabili changamoto katika uzoefu wa maisha.  Kuyapitia magumu katika makuzi ya mtoto, humjengea uwezo mkubwa wa kuzikabili changamoto na uwezo mkubwa wa kutoteteleka katika magumu ya maisha katika umri wa utu uzima.

Katika maisha; mateso hutupatia mbinu mpya za kuweza kukabiliana na mambo au changamoto mpya za maisha kulingana na mazingira mapya, maendeleo, teknolojia na changamoto mpya. Bila changamoto, mwanadamu hawezi kubuni au kugundua jinsi mpya ya kukabiliana na matukio mapya. Mateso (miiba), shida, dhiki na adha zitusongazo wakati mwingine hutupa uwezo wa kuwa bora zaidi kwa ajili ya hatua zingine zaidi.
Changamoto zitukabilizo hutufanya tukomae kiakili pamoja na kuwa na uwezo wa kupambanua, kufanya maamuzi na kutatua mambo mbalimbali yatukabiliyo. Akili zetu haziwezi kukomaa na kuwa na uwezo mkubwa wa maamuzi bila kukutana na changamoto za aina mbalimbali aidha, rahisi na ngumu.
Mototo ni vyema alelewe katika maisha ya aina zote; shida na raha zampasa kuzijua katika hatua zote za makuzi ili baadaye awe na uwezo wa kuzikabili changamoto na kuyaishi maisha ya shida na raha. Si vyema sana motto akaishi maisha ya raha pekee, siku za ukubwani yakitokea magumu anaweza akateteleka na kuathili hatua zote za maisha yake.
Kama alivyo tai kwa watoto wake; vivyohivyo .Mungu wakati mwingine hujifanya kama haoni yale yanayotukabili, ili tuweze kupiga hatua na kumtumainia yeye katika imani isiyokoma.

SURA YA NANE
TUWE WENYE UHAKIKA WA MAISHA YETU
Tai wanaouhakika wa kujiongezea maisha na kuishi tena afikapo umri wa kuchoka au kupoteza nguvu. Tai anaweza kuishi miaka mingi; kuanzia miaka 30 hadi 70. Wakati ambapo tai anakuwa ameanza kupoteza uwezo wake, kwa sababu ya kuishi miaka mingi (afikishapo miaka 30 na kuendelea), uwezo wa kukamata mawindo hupungua kutokana na kupungua ngu vu zake. Sanjali na kupungua nguvu, tai pia mdomo au urengu (sehemu za kudonolea) wake hupungua makali na uwezo wake kwa sababu huwa umepinda sana.

Aidha, kutokana na uzee na uzito wa mabawa, mabawa, manyoya yanarundikana kuelekea sehemu za kifuani na kupekea tai kushindwa kurukavyema.  Katika wa hali hii hubakiwa na maamuzi mawili pekee. Mosi; kukubali kufa kwa njaa kwa kukosa chakula kutokana na hali ya kuchoka alikokufikia. Mbili; kuendelea kuishi kwa kupitia mateso ya takribani 80 au 145 na kuendelea. Ili tai aendelee kuishi, humpasa kupanda juu ya ncha ya mlima kasha huanza kujitoa ganda la juu la midomo yake kwa kujipigiza kwenye mawe au kitu chochote kigumu.
Baada ya ganda la mdomo wa juu na wachini kutoka, tai husubiri hadi ganda la ncha ya mdomo wa juu na chini liote (iwe katika ugum wote).  Baada ya hapo tai huanza kujitolea manyoa yote katika mwili wake wote. Baada ya siku kadhaa (miezi miwili hadi mitatu) manyoya huwa yameota na kuongeza tena maisha mengine ya kuishi aidha, mika 30 au zaidi. 
Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Wakati mwingine watu hujiua au hujinyonga kwa sababu ya kushinwa kuvumilia na kuzikabili changamoto. Jambo hili la kujiuwa kwa watu wengine husababishwa na kukosa tumaini katika maisha kwa kukosa uwezo wa kuhimili changamoto na ugumu wa maisha.
Kutumia vileo, madawa, sigara na vitu vituleteavyo madhara na kuathiri afya zetu, hutukosesha uhakika wa kuishi tena. Kutojari kanuni na taratibu za afya katika miili yetu juu ya nini tule, tunywe na tuweke juu ya miili yetu husbabisha magonjwa katika miili yetu, hivyo hupunguza uwezo wa kuishi.
Kuteseka ni lazima kuje ili kuyafikia mafanikio mapya. Ni vigumu kuyafikia mafanikio bila kuteseka kwa namna moja au nyingine. Kupiga hatua na kulikabili jambo kunahita maamuzi yanayoumiza wakati mwingine. Hata kama mengine yanaumiza lazima tukubali, kuyapokea na kufanya badiliko.
Yatupasa kuibua mambo mapya mazuri yenye manufaa kwa jamii yaliyofichika ambayo wengine hawajayagundua wala kutambua. Lakini pia waweza kuibua mabo mapya mabaya yaliyofichika ili kuyaweka bayana kwa jamii ili jamii iyafahamu na kuyaacha.
Fanya matengenezo kwa kurekebisha pale ulipopelea na kukosea ili kufanya uwe mpya katika safari ya maisha yenye mafanikio. Matengenezo yatakupa nguvu mpya na kukukufanya uanze upya kwa ari na uwezo mpya kwa kufuta yale yote yaliyokufanya upoe, urudi nyuma au ukate tamaa.
Tusikubali kufa kizembe kwa kujitakia kinyume na mapenzi ya Mungu muumba wetu. Kutumi vitu, vyakula, vileo visivyofaa na vyenye kuhatarisha afya zetu. Utumiaji wa sigara, pombe, vipodozi vya kikemikali vyenye madhara pamoja na kufanya ngono kupita kiasi. Chochote unachotumia kwa wingi chenye madhara katika mwili kitakuletea madhara hatimae kifo. Kubadiri mitindo yetu ya maisha kwa kuiga kutoka nchi za magharibi na kuacha ulaji wetu wa asili na mienendo ya maisha ya kiafrika. 
Kuna muda, mtu hufanya mambo fulani kwa sababu, kila mtu hujikuta katika mkondo au maisha yalimchagulia namna ya kuishi, lakini hayo yote huwa ni matokeo ya bahati mbaya ambayo kuna muda kwa uzembe wetu au kwa kuyaamini tusiyoyamaanisha tukajikuta tumeyatenda ema. Kama umegundua ulipojikwaa yakupasa urudi nyuma na uanze upya.
Kila mtu anahistoria yake katika maisha yake lakini ikitokea ukajua unapokosea na kujirekebisha basi hiyo ni faraja ndani ya moyo wa kila mmoja aliyechukizwa na tabia yako ya awali, hivyo basi waweza kutubu dhambi zako na kungu atakusikia.
Kitu kidogo na cha pekee na cha thamani unachoweza kufanya katika maisha yako ni kutafuta nini unachokitumainia, na kikubwa unachoweza kufanya ni kuishi ndani ya matumaini hayo. Siyo tu kuyakubali kwa mbali ila kuyaishi kwa undani wake. Matumaini yanaweza kuwa nguvu kubwa yenye msukumo. Inawezekana kabisa kusiwe na miujiza ndani yake, ila ujuapo kinachokutumainia  sana na ukakikumbatia  kama mwanga  ndani yako, basi unaweza kutenda jambo na kufanya mambo yatokee kama miujiza. Kwa hiyo, yafanye matumaini yako yaishi. Jukumu moja wapo la binadamu ni kufikiri kwa niaba yako mwenyewe.
Katika kufanikiwa, binadamu lazima ajipange wajipange vyema. Kila mtu ananafasi ya kuwa vile atakavyo, haijarishi njia atumiayo ilimradi upo ukweli wa kila jambo. Mafanikio huja tu pale unapoamua kufanya mambo magumu kuwa mepesi unapoamua kulitazama jua kwa ukali ukali wake
Kila binadam anahadithi na simulizi juu ya maisha yake. Aidha,  ya kusikitisha  pengine ya kukatisha tama, bali tunatofautiana namna ya kuzikabili huzuni zetu. Kila mmoja alishawahi kupitia jambo gumu la kukatisha tamaa, na wengingine waliteseka na kukubali matokeo ya jambo hilo na walisonga mbele
Haitupasi kujiona kuwa hatuna bahati katika maisha. Yatupasa kujua kuwa maisha yanamambo mengi ambayo ni msamiati kwenye fikra zetu.  Majibu sahihi kwa msamiati ambao hauujui ni kubahatisha jibu la swali ambalo ambalo hujalisikia kamwe; hivyo unachotakiwa kufanya ni kuiambia nafsi yako itawale utashi wako.
Maisha hutupa changamoto ili kupima ujasili wetu wa kubadirika. Katika muda huo wa changamoto, nafasi ya kufanya kwamba hakuna linalotokea au kusema kuwa hauko tayari kuipokea hiyo changamoto. Changamoto hazisubiri utaya wako na maisha hayaangalii nyuma maana ni kama sheria mpya inayotungwa juu ya jambo fulani; huwa inaanza pale iliposainiwa. Wiki moja ni zaidi yawa kutosha tunaouhitaji ili kuamua kama tunakubali au la. Japokuwa pia kuhitaji kwenda mbele kwenye maisha yako, lakini unaweza kukuta umeweka mguu mmoja kwenye “break”.
Nini thamani ya maisha kama tunaamua kwenda mbele kwa maisha ya kukanyaga breki. Ili uwe uwe huru, lazima ujifunze kusahau na kuacha mambo mengine yaende.  Acha kuumizwa na machungu, acha yaende kasha sahau. Maumivu yako na maisha yako ya zamani ndiyo yanayokuvuta nyuma na kufanya usisonge mbele. Kubali kuanza upya.
Watu waliofanikiwa zaidi ni wale walioyajua matatizo, walizijua harakati za maisha, waliokumbana na  misukosuko na taabu, walioyakabili majaribu ya kila namna na changamoto zake na mwisho wa siku waliweza kusonga bele. Lolote ambalo haliwezekani leo, unaweza kulifany liwezekane kesho endapo utaamua tu juu ya mustakabali wa njia uipitayo.     

SURA YA TISA
KUMKABIRI ADUI KATIKA UWANJA VITA
Tai humshinda adui kwa kumbadirishia uwanja wa vita aliouzoea. Harakati za kujipatia kitowe kwa tai kuwa ni cha kufa na kupona maana anayewindwa huwa ni adui kwa namna nyingine. Tai anapokuwa katika harakati za kutafuta kitoweo, hukikamata kitoweo kutoka eneo husika na kupaa nacho angani katika uwanja wa vita aliouzoea ambao kwa adui (kitoweo) ni mpya. Kitoweo hicho cha weza kuwa nyoka, samaki au mnyama aliye na ukubwa wa kubebwa na tai. Tai hufanya mbinu kadhaa ili kumshinda adui/ kitoweo huyo kwa kumuachia angani na kumdaka tena kabla ya kufika chini. Tendo hili hulifa kwa vitoweo ambao ni hatari kwa maisha yake kama nyoka  ili kumpotezea adui uwezo na ujasili kukabiliana na tai. Wakati mwingine huwapelekea vitoweo hivyo watoto.

Fundisho tulipatsalo la kujifunza.
Wakati mwingine ili ushinde katika mpambano wa wa kutafuta, ni vyema ukabakia mazingira hayo hayo uliyoyazoea; maana unayafaham kiundani zaidi. Hivyo basi, usiruhusu mazingira yakubadirishe, bali jitahidi mazingira uyamudu na kuyabadirisha wewe kwa namna yoyote.

Mara zote inatupasa kufahamu uimara au uwezo wetu uko wapi, pia udhaifu wa washindani wetu upo wapi katika biashara ili kuweza kuwazidi katika ushindani juu ya soko huria
Katika harakati ya kutafuta mafanikio, waweza kwenda kutafuta mbali kasha ukarejea nyumbanili ili kula matunda ya mafanikio na wanyumbani kwako badala ya kutapanya hukohuko. Wengi huenda mbali sana kutafuta nje ya maeneo way ale wanayoishi ili kutafuta, lakini cha kushangaza hali na walio wa nyumba zao kwani huzamia hukohuko na wasirudi tena na kuacha familia zao zikiteseka. Kula matunda na wale wa familia yako kutakuzidishia mibaraka ili uzidi kufanikiwa zaidi; maana mchumia juani hulia kivulini na wa kwao
Elimu au taaluma uliyoipata mahala fulani; uichukue hivyohivyo lakini usisahau kujiendeleza zaidi ya walimu wako walivyokupatia katika kukufundisha. Daima mtazamo wako uende mbali zaidi ili kuweza kuwapita wengine katika fikra na maarifa yao katika kiwango walichofundishwa awali, wewe zidi kwenda mbele.
Kama ni mfanyabiashara, peleka bidhaa au mali uliyoinunua sehemu ambayo unaijua kwa uhakika. Eneo ambalo unalijua vyema; litakupa uhakika wa faida na kukuzalishia zaidi na zaidi.
Katika maisha kumbuka kuhesabu mibaraka badala ya matatizo katika kutafuta mafanikio. Mara nyingi kutokana na uzoefu, watu wengi huwa “busy” kuhesabu matatizo kuliko mafanikio yatokanayo na mibaraka. Twaweza kuyaelewa maisha kwa kuangalia nyuma, ila twaweza kuyaishi maisha kwa kuangalia mbele. Mafanikio huja kwa kuweza, kushindwa huja kwa kutoweza.
Kuanguka chini hakukufanyi kuwa ndiyo umeshindwa, bali kuendelea kukaa chini ndiko kutakuashiria kuwa umeshindwa. Hivyo, kushindwa kwa mtu husababishwa na ukosefu wa bidii na sio ukosefu wa kipaji. Mafanikio hayaji kwa kila mtu hivihivi, bali kwa mtu Yule anayejitahidi kuwa mwenye bidii, mwadirifu na mchapa kazi. Naamini ukifanya sehemu yako kwa bidii na moyo wako wote, Mungu atakuwa nawe katika mafanikio
NA MWL. FRANK PHILEMON


Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU