NGUVU YA MSAMAHA
Katika injili ya Marko
11:25-26 kusameheana
kumesisitizwa kama ifuatavyo: 25”Nanyi,
kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili Baba yenu
aliyembinguni awasamehe na ninyi makosa yenu. 26”Lakini kama ninyi
hamsamehi, wala Baba yenu aliye Mbinguni hatawasemehe ninyi makosa yenu”
Kwa Nini ni Muhimu
Kusamehe?
Zipo
sababu nyingi za kusamehe, zifuatazo ni miongoni mwazo:
1.
Kusamehe ni tabia ya Mungu, na
wamchao: Mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu (Mwanzo 1:26). Mwanadamu amchae Mungu kwa
kweli yote, lazima awe na tabia ya Mungu kwa maana Mungu ni kielelezo cha
kwanza cha kusamehe kwa mwanadamu (Isaya 43:25. Isaya 1:18, 1Yohana 1:9).
2.
Kusamehe ni hali ya Upendo: Kama
tunda la roho ni upendo vivyo hivyo kusamehe ni tunda la upendo (1Wakorintho 13:4-7). Tabia ya mtu amchae Mungu ni upendo kwa wengine hata kama
atakwazwa. Mungu ni pendo, hata mwanadamu pia yampasa awe na upendo utokanao na
Mungu. Kusamehe ni ishara na kielelezo cha upendo, kwa hiyo mtu anayesamehe
anakiwango kikubwa cha upendo (Yohana
3:16. 1Yohana 4:8. Yeremia 29:11).
3.
Ni kufanya kama Mungu anavyotusame:
Kama
Mungu anavyomsamehe mwanadamu bila kuchoka binadamu pia yampasa kusamehe
wengine vivyohivyo bila kuchoka (Yohana 1:12-13).
4.
Hakuna mwanadamu aliyemkamilifu
asilimia 100: Endapo mtu atagundua kuwa, hakuna
aliyemkamilifu asilimia zote, basi atakuwa anajua nini maana ya kutoa msamaha
kwa wengine. Mwanadamu yeyote hukosea na kukosewa pia. Sio salama mwanadamu
kujihesabia haki kuliko mwingine; maana hata yeye akikosea huhitaji kusamehewa
pia. (Warumi 3:10, 23).
5.
Kusamehe kunaondoa mawazo ya
kulipiza kisasi: Mwanandoa asipojenga tabia ya kusamehe
hujenga mawazo ya kisasi; kutosamehe na kuwaza jambo baya juu ya mwingine ni
sawa na yule aliyetenda kwa vitendo. Kisasi ni kile unachokirejesha kwa mtu; mfano kumnunia mtu, kutopokea simu
yake, kumchongea na kumsema vibaya, kuua au kupanga njama za kuua mtu, kuchawia
au kuloga, kumpiga mtu (Warumi
12:19.Yakobo 4: 12).
Madhara Yanayoweza
kumpata Mtu Asiposamehe
Tabia
ya kutoweza kusamehe hujenga hali au tabia ya kulipa kisasi. Kuwaza kulipa
kisasi ni sawa na kutenda katika kulipa kisasi, hivyo mawazo au hatua za kisasi
huwa na hasara zifuatazo kwa mmoja au wanandoa wote:
1.
Kunapelekea kujitenga na uwepo wa
Mungu: Roho Mtakatifu hawezi kukaa mahali
palipo na machafuko au Mungu hawezi akashikamana na mdhambi ambaye anawaza maovu
bila kutubu. Kutosamehe kwa mtu huondoa uwepo wa Mungu kwa mtu huyo (Warumi
12:17, 21).
2.
Hupelekea matatizo mengine juu ya
mlipa kisasi: Mtu asiyesamehe hutengeza ongezeko la
majaribu mengine kumwandama maana mkono wa Mungu unapotoweka Sheteni huweka makazi
ili kuzidi kumpoteza mtu huyo. (Mithali 17:13).
3. Hupelekea
kutenda au kuchuma dhambi ya mauaji (1Yohana 3:15, 1Yohana 3:11-12, Mathayo 5:21-22): Kumuwazia
mtu mwingine babaya, hujenga moyo wa
visasi hivyo, kujichumia dhambi ya mauaji maana dhambi hutendeka katika fikra (moyoni)
matendo hufuata.
4. Mtu
alipaye kisasi hujiongezea uadui au maadui: Tabia
ya kulipa kisasi haitatui tatizo bali huongeza matatizo na maadui
Namna ya Kufanya ili
Mtu Aweze Kusamehe
Kusema
“nimekusamehe lakini sintosahau” ni
kutojua maana ya kusamehe, ili mwanadamu aweze kusamehe, yampasa kusahau kabisa
juu ya kosa au baya alilotendewa. Mkristo amchaye BWANA yampasa ajue, kufuata,
kufanya na kuyaishi mambo yafuatayo yatakayopelekea kusamehe na kusahau:
1. Ajue kuwa yeye ni
mtoto wa Mungu hivyo yampasa kusamehe na kusahau kama Mungu awasameheavyo
wanadamu na kufuta makosa yao (1Petro
1:18-19).
2. Ajitahidi kuwaombea
mema na kuwapenda adui zake siku zote na siyo kulipa baya kwa baya (Mathayo 5:44-45), hivyo awawazie mema
adui zake siku zote (Warumi 12:20-21)
3. Ajue kuwa yeye siye
mwenye kujipigania, bali Mungu ndiye huwapigania walio wake, hivyo vita vyote
si vyake bali ni vya Mungu mwenyewe na mwanadamu yampasa kumkabidhi Mungu
matatizo yake (Ayubu 19:25, 2Nyakati
20:15).
4. Mwanadamu atambue
kuwa, vita vyake si juu ya damu na nyama, bali ni ya kiroho zaidi maana pambano
kuu bado linaendelea kati ya wema na ubaya yaani Shetani na Kristo (Waebrania 12:2-3, Wagalatia 4:7).
5.
Ajuwe kuwa si mtu amkoseae au kumtendea mabaya bali ni Shetani anamtumia
mwanadamu kutenda yaliyo maudhi.
Comments
Post a Comment
Thanks for viewing and passing through NMEE blog. Keep following the blog