SOMO: UASI WA KANUNI YA KIROHO TUSIOUJUA:



FUNGU: WAEFESO 5:15-21 “15Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16mkiukomboa wakati kwa maana zama hizi ni za uovu. 17Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya bwana. 18Tena msilewe Kwa mvinyo, ambamo mnaufisadi; Bali mjazwe Roho; 19mkisemezana Kwa zaburi Na tenzi na nyimo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; na kumshukuru Mungu Baba siku zote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana Yesu Kristo; 21hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo.

1.0 UTANGULIZI:
1.1. Katika maisha yangu ya kiroho; Nahau zifuatazo zimenifunda:
1)   Kama hujui mahala unapoelekea uwapo safarini, njia yoyote miongoni mwa nyingi itakuchagulia uelekeo na Kama hujishughulishi kujua unakoelekea, njia haiwezi kukuchagulia uelekeo sahihi uutakao.
2)   Eneo lenye giza zaidi kuliko maeneo yote katika mshumaa lipo chini ya mshumaa.
3)   Debe lililo tupu ndilo lipigalo sana kele.
4)   Maisha yetu ya kiro ni sawa na kuendesha baiskeli, ili udumu kuwa na stamina yakupasa uendelee kuendesha
5)   Bahari isiyo na dhoruba haiwezi kumfanya nahodha awe imara katika ujuzi na uzoefu.
6)   Usipojifunza yale usiyoyajua huwezi kujua usiyoyajua
7)   Akili ya binadamu inafananishwa na mwamvuli, hufanya kazi vyema pale inapofunguliwa.
8)   Mpiganaji mzuri si yule ajilindaye, bali ashambuliaye katika kujilinda

1.2. Maelezo ya fungu, wimbo.
(a) Mkatadha mkuu wa fungu kwa mujibu wa somo la leo juu ya wakati (reje fungu kuu). Kwa kuwa Mtume Paulo alikuwa mhanga katika kuupoteza muda wake huko mwanzo, hivyo anasisitiza sana juu ya kuukomboa wakati katika wokovu wa mkristo: Wenye hekima huukomboa wakati kwa kutenda mema, bali wajinga na wapumbavu hutenda maovu.

Wenye hekima walio na akili hutenga muda wao kwa ajili ya kumtukuza Mungu hasa katika kuimba, kusemezana kwa zaburi, tenzi, nyimbo za rohoni, kumshukuru Mungu, Kumshangilia Bwana Moyoni mwao na kunyenyekeana wao kwa wao katika Kristo ili wajazwe Roho. Lakini waovu na wapumbavu hulewa mvinyo (aidha mafundisho mapotofu), kufanya kila aina ya ufisadi.

(b)Wimbo namba 71 katika vitabu vya nyimbo za Kristo (Kesheni Kaombeni-kwa kusoma beti zake) nao pia umetuhimiza kutenga muda wa kutosha katika wa maisha yetu kwa ajili ya kushikamana na Mungu katika kuomba.

2.0. KIINI CHA SOMO:
2.1. Maelezo mafupi juu ya somo:
Mungu alianza na muda katika siku zake zote za uumbaji (Mwanzo 1:1-5) ili kufanikisha uwekaji wa nyakati/majira kwa ajili kumuwekea kumbukumbu sahihi minadamu hapo badae. Hivyo huwezi ukatenganisha muda na uumbaji pamoja na ibada Zetu kwa kwa Mungu aliyetuumba.

Katika nuru yaani mwanga ambao hufanya mchana pamoja na giza ambaao hufanya usiku hutupatia kujua kuhesabu massa siku, juma, mwezi, mwaka na miaka. Au kwa sasa kutokana na teknologia tunahesa wakati katika milsecond, sekunde, dakika, saa, siku, juma, mwezi, mwaka, mlongo, karne na millennia.

Biblia ambamo limo neno lake Mungu, limeandikwa kwa kuzingatia wakati aidha, jambo lilishatokea, limetimia, litatokea. Hivyo Mungu kutupatia wakati alikuwa na makusudi makuu ya sisi tuweze kuutunza muda kwa ajili ya kumwabudu na kumtukuza kwani sis ni mawakili tu wa muda.

Swali la kujiuliza: Je, sisi ni mawakili waaminifu wa muda wa Mungu aliotupatia? Kushindwa kumpatia kipaumbele Mungu kwa kuhodhi muda Wake kwa kufanya mambo yetu binafsi kinyume na ufanywaji wa wakati kama yalivyokuwa makusudi yake ili kumwabudu na kumtumikia Yeye hatufanyi dhambi ya kumwibia Mungu kama tunavyomwibia mali zake (yaani zaka na sadaka)?

2.2. Muda katika mambo ya kiroho
Muda ni miongoni mwa aina sita za uwakili. Muda unasehemu kubwa katika wokovu wetu, maana unaashiria mambo yafuatayo:
a)    Wakati unaweka bayana Ukombozi wetu,
b)   Wakati unaonesha kikomo chetu cha rehema,
c)    Wakati unabainisha kutumika kwetu kwa Mungu,
d)   Wakati unapima ukomavu na ukuaji wetu kiroho,
e)    Unatuelekeza kutimiliza mpangilio wa maagizo ya Mungu,
f)    Wakati unatudhihirishia nini tufanye na kipi tusifanye,
g)   Wakati unatutanabaisha mambo yaliyopita katika histori yanayotufunza yaliyopo na yajayo ili yatimie katika unabii,
h)   Wakati ni kumbukumbu kwenye hatima ya hukumu; maana kila jambo na kila tendo kwa wakati ulipolitenda litaletwa hukumuni.

2.3. Je, huwa unakuwa naye Bwana kila muda?:
Muda wako ni zawadi ya thamani sana ambayo Mungu amekupatia kwa makusudi ya kumtumainia Yeye. Muda ni mali, muda sio rafiki unapochelewa kutimiliza jambo, muda ni mstari hivyo kuwa nao makini sana kwa ajili ya wokovu wko. Mkristo asiyetunza muda na kuutumia vizuri katika kuweka uhusiano wake na Mungu avunja sheria kwani anamwibia Mungu Muda wake. NB: Tasisi za kidunia zimeweka watunza muda, je vipi sisi tusiojari na kutunza muda tupo salama? (Kisa cha interview)

2.4. Mpango wa Mungu kutupatia Muda wanadamu ni nini?
1. Tuwajibike kwake yeye: Waefeso 5:16 “mkiukomboa wakati kwa maana zama hizi ni za uovu”
2. Tuyafuate maelekezo yake: Waefeso 5:8 “Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru”
3. Tupange ratiba kwa ajili yake yeye: Zaburi 55:16-17 16Nami nitamwita Mungu, Na Bwana ataniokoa; 17Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye atasikia sauti yangu”
4. Tuwe katika utaratibu sahihi: Kutoka 40:1-16 “…...16Musa akafanya hayo yote; kama yote Bwana aliyoagiza ndivyo alivyofanya”
5. Tujikite katika hekima yake: Zaburi 90:12 “Basi utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima”
6. Tuutafute ufalme: Mathew 25:34-35 34Kisha Mfalme atawambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njooni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; 35kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha”
7. Atuponye na maovu katika nyakati zote: Zaburi 31:15 “Nyakati zangu zimo mikononi mwako; Uniponye na adui zangu, nao wanaonifuatia”  
8. Kuwashuhudia na kuwahubiri wasio mjua: Yohana 9:4 “Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana; usiku waja asipoweza mtu  kufanya kazi”
8. Tuyajue mazingira na hari yake: Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu” (waweza soma hadi fungu la 8)
9. Tukumbuke kuzishika amri zake: (Soma mafungu yafuatayo; Kutoka 20:8-11, Kutoka 20:12)
10. Tuepuke kufikiwa na kikomo cha rehema: Mhubiri 12:1-2 “1Mkumbuke Mungu wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala hazijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 2Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; ………”

2.5. Tunapotezaje muda wa Mungu?
1. Kwa kufanya mambo maovu na uasi wa sheria: 1Yohana 3:4 “Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi wa”
2. Kwa kutumia muda mwingi kujiwekea hakiba duniani: Mathayo 6:19-21 “19Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; 20Bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; 21Kwa kuwa hazina ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako”
3. Kutokufanya kazi yake Mungu: Mathew 28:19-20 19Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; 20Na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa hadari”.
4. Kiburi cha uzima: Yakobo 4:13-14 13Haya basi, ninyi msemao, leo au kesho tutaingia katika mji furani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; 14Walakini hamjui yatakayokuwako kesho”

2.6. Tutunze vipi muda wa Mungu?
1. Tuyape kipa mbele yaliyo maagizo ya Mungu: Zaburi119:6 “Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote”
2. Muda wa ibada na huduma uwe kipambele: Isaya 55:6 “Mtafute Bwana, Maadam anapatikana, Mwiteni, maadam yu karibu”
3. Tumia muda wako wa starehe na burudani kwa ajili mambo ya kiroho: Luka 4:4 “Yesu akamjibu, imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu”
4. Andaa, tambua na fuata ratiba yako: Kutoka 34:21 “Utafanya kazi siku sita, lakini katika siku ya saba utapumuzika; wakati wa kulima mashamba, na wakati wa kuvuna pia, utapumzika”, Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u-karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini”

NOTE: Tumia fomula ya “D-O-I-T-N-O-W” Kwa lugha y Kiingereza na “GA-PA-E-TU-FA-FU-VI” kwa lugha ya Kiswahili unapona ratiba yako na Mungu huitekelezi:

3.0 HITIMISHO:
Mtumishi wa Mungu Daudi alijua makusudi ya Mungu kuweka muda: Zaburi 90:12 “Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima” na Zaburi 39:4-5 “BWANA, unijulishe mwisho wangu, na kiasi cha siku zangu ni kiasi zangu”.

Mungu alipanga mpango wa wokovu, na wakati ulipotimia ikawa: Wagalatia 4:4 “Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezariwa chini ya sheri, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana”.

Hivyo tu baada ya dakika tano yesu kufa msalabani palikomeshwa: 1.Sadaka ya dhambi kwa ajili ya ondoleo la dhambi (Yesu alisimama badala yake), 2.Sadaka ya upatano wa amani ikakoma (Yesu akawa mbadala), 3.Pasaka ya Israel ikakoma (Meza ya Bwana ikaanza), 4.Huduma ya upatanisho duniani ikakoma (maana Huduma ya ukuhani duniani ilikoma; Yesu akaendelea nayo huko mbinguni kama kuhani mkuu) 5.Ulimwengu ukawekwa pamoja katika kukombolewa (Kutoka kwa taifa la Israeli) 6. masabato na miandamo ya miezi ikakomeshwa (Maana Tunaye roho Mtakatifu anayetukumbusha kutenda mema).

Hareluyaaaa!!


Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU