UJASIRIAMALI NA BIASHARA KATIKA FAMILIA NA NDOA
Uchumi imara wa familia (kwa wanandoa) hurahisisha upatikanaji wa
mahitaji ya msingi ya familia pamoja na uhakika wa kuhudumia mahitaji ya
watoto. Lakini pia, familia yenye uchumi mzuri inaweza ikasaidia kusukuma au
kuendeleza na kukuza huduma ya uinjilisti na utume ulimwenguni kwa njia ya
kumtolea Mungu zaka na sadaka pamoja na kuchangia programu mbalimbali za kazi
ya utume ulimwenguni au katika kanisa mahalia.
Pale wanandoa au wanafamilia
wanapoitegemeza kazi ya Mungu, Mungu huwabariki na kuwapatia cho chote kile
wanachokiomba, kama vile Mithali 16:3 inavyosema kuwa: “Mkabidhi BWANA kazi zako,
Na mawazo yako yatathibitika”. Maana imeandikwa pia kuwa: “Ni heri kumkimbilia BWANA kuliko
kuwatumainia wanadamu” (Mithali 118:8).
Hivyo basi, ni vizuri wanandoa kujituma
katika kutafuta na kuzalisha ili kukuza kipato cha familia kupitia kazi za
mikono yao maana Mungu hatawaacha kuwabariki kwa kujituma kwao na kufanya kazi
kwa bidii. Bidii na jitihada ya kazi kwa wanando, iende sambamba na kumwomba
Mungu (Luka 11:9-10); maana imeandikwa kuwa: “Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa
jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka? Au akimwomba yai, atampa nge?”
(Luka 11:11-12).
Hata hivyo, ukiwa na Mungu atakupa uwezo
wa kuthubutu kuanzisha biashara au uzalishaji kama alivyothubutu Daudi katika
kumkabili Goliathi kwa jina la BWANA (1Samweli 17:32, 45). Katika sura hii
tutaangalia vipengere kadhaa vya muhimu juu ya kufanikisha kuanzisha biashara
(hususani ujasiriamali) kwa wanandoa ili kukuza vipato vyao.
A: Wazo la Biashara
Biashara yo yote huanza na wazo la
biashara. Wazo la biashara ni maelezo mafupi na fasaha yanayohusu uendeshaji wa
shughuli ya biashara iliyokusudiwa. Wazo la biashara ni vyema likajikita katika
gharama, bidhaa, huduma, mahitaji ya watu, bei, matakwa ya watu, ujuzi na
uzoefu [Philemon Frank, 2016. Secrets of
Success in Entrepreneurship].
Biashara yenye ufanisi ni ile inayokidhi
mahitaji ya wateja wake. Pia, biashara lazima iwapatie watu au wateja kile
wanachohitaji au wanachotaka; hivyo basi, wazo la biashara litakuambia: aina
ya bidhaa au huduma zitakazotolewa na biashara yako, nani watakuwa wateja wa
biashara yako, jisjinsi au kipi biashara yako itakavyouza bidhaa zake au kutoa
huduma zake na namna biashara yako itakayokidhi mahitaji ya wateja.
Jinsi ya Kutafuta Mawazo Mazuri ya Biashara
Zipo namna mbalimbali za kutafuta mawazo
mazuri ya biashara. mawazo yanayotokana na rasilimali zilizopo,
shughuli iliyopo na uliyonayo, mahitaji Mawazo mazuri ya biashara yaweza
patikana kwa vyanzo au njia zifuatazo:na
shauku za watu juu ya kipi wakipate, kutoka fursa za biashara zinazoonekana au
zilizo hai, mahitaji ya wateja
talajali pamoja na ujuzi, ufahamu au uzoefu wa mtu
husika. Sambamba na sababu hizo, Mungu anatakiwa apewe kipaumbele ili
kuyanyosha mapito yote ya wazo la biashara (angalia katika Mithali 3:6).
Mambo Yanayounda Wazo Zuri la Biashara
Unapohitaji kupata wazo bora au zuri la
biashara (kutoka miongoni mwa mawazo mengi ya biashara), ni lazima ufahamu
mambo yanayounda wazo zuri la biashara. Wazo zuri la biashara ni lile
linalozingatia mambo yafuatayo: bidhaa au
huduma inayotakiwa na wateja, biadhaa au huduma unayoweza kuuza kwa bei ambayo
wateja wako wanaweza kuinunua na ambayo itakupatia faida, maarifa na ujuzi ulio
nao au unaoweza kuupata ili kufanikisha uendeshaji wa biashara hiyo na mwisho
rasilimali au fedha unazoweza kuwekeza katika biashara husika.
Ubunifu wa Wawazo la Biashara
Wakati wa kutoa mawazo ya biashara ni
vizuri uweke mawazo yako wazi kwa kila jambo. Fikiria mawazo mengi kadri
uwezavyo na kuyaorodhesha kadiri uwezavyo juu ya biashara ambayo unaweza
kuifanya. Biashara yenye mafanikio msingi wake ni wazo zuri la biashara. Ni muhimu
kuwa na muda na kufanya juhudi, kufanya kazi kwa bidii katika kutambua mawazo
ambayo yanastahiki na yenye kufaa sawa na neno la Mungu linvyosema: “Nanyi jipeni nguvu, wala mikono yenu
isilegee; kwa maana kazi yenu itakuwa na ijara” (2Mambo ya Nyakati 15:7).
Mawazo ya biashara yanaweza kupatikana
kwa: kupeana mawazo (kukoleza bongo),
kutembelea eneo lako la biashara, kuchunguza mazingira yako, kutumia uzoefu
ulionao na kuazima orodha kutoka kwa wengine.
- Kukoleza Bongo
Hii ni njia ya kufungua au kuweka wazi
mawazo yako na kukusaidia kufikiri mawazo mengi tofauti. Unaanza na neno au
mada halafu andikika kitu kinachokuja katika mawazo yako. Kupeana mawazo ya
kunafanya kazi vizuri unapobadillishana mawazo na mtu mwingine au na kikundi
cha watu, lakini pia waweza kujaribu mwenyewe peke yako. Makampuni mengi
yanatumia njia hii kupata mawazo mapya ya biashara; njia hii husaidia kutoa
maono mapya kwani pasipo maono, watu huacha kujizuia (Mithali 29:18).
Anza na neno moja (mfano mbao, kuku).
Badala ya kuanza na neno la kubahatisha tu unaweza ukaanza na bidhaa maalumu,
halafu unajaribu kufikiria biashara zote zinazohusika nayo, mfano: zile zinazohusika katika uuzaji, zile
zinazohusika katika utengenezaji, zile zisizohusika moja kwa moja (faida ya
ziada) na zile zinazohusika katika kutoa huduma.
- Orodha ya Mawazo
Anza na orodha ya mawazo kwa biashara
yako, rudia shughuli za awali ulizokwisha kuzifanya hadi sasa. Chagua mawazo yo
yote ambayo yanaweza kuwa mawazo ya biashara ya kufaa na yaandike.Tenga
karatasi yako katika pande mbili, kulia (mawazo) na kushoto (maoni).
- Ziara Katika Eneo la Biashara
Tazama eneo lako unaloishi, tafuta aina za
biashara ambazo zinafanyika katika eneo lako, angalia kama unaweza kuona
mapengo katika soko. Kama ni kijiji au mji mdogo, zunguka mji wote na kama ni
jiji tembelea eneo la viwanda, soko na maeneo ya madukani. Tenga karatasi yako
ya utafiti katika orodha ya sehemu nne yaani; wafanya biashara wa rejareja,
wauzaji au wafanya biashara wa jumla, wazarishaji wa kubwa na wadogo na watoa
huduma; kisha chambua mapengo na fursa zilizopatikana.
- Kuchunguza Mazingira Yako
Kama orodha yako ilihusisha eneo kubwa la
soko lako, yumkini unaweza kuona ni aina gani ya viwanda au huduma ambayo
uchumi wa eneo lako unategemea. Itakuwa vizuri kufikiri kupata mawazo mazuri ya
biashara kwa kuzingatia nyenzo na taasisi zote zilizopo katika eneo lako. Kwa
mfano, fikiria kuhusu: nyenzo za asili
(vifaa vya asili), uwezo na ujuzi wa watu, taasisi, viwanda, bidhaa mbadala
zinazoagizwa, uchapishaji na maonesho ya biashara na maonesho ya bidhaa.
- Kutumia Uzoefu
Zingatia uzoefu wako pamoja na uzoefu wa
watu wengine ili kutoa huduma, uzalishaji au kufanya biashara kulingana na wazo
la biashara.
Namna ya kuchagua Wazo Linalofaa katika
Orodha ya Mawazo Yako
Ukiwa umepata mawazo machache
yanayotekelezeka kuanzisha biashara yako angalau matano au zaidi ya matatno;
hivyo, kazi inayofuata ni kuchukua orodha yako ya mawazo na kupunguza katika
mawazo matano na kubakiwa na yanayofaa zaidi. Inawezekana kuwa kuna mambo mengi
usiyofahamu kuhusu kuendesha biashara ambayo iko katika orodha yako; maswali
maswali yafuatayo yanaweza yakakusaidia kuchagua wazo bora la biashara miongoni
mwa mawazo mengine:
1.
Unafahamu kwa kiasi gani kuhusu bidhaa au huduma katika biashara hii?
(Aina ya hiyo huduma).
2.
Una uzoefu gani utakaokusudia kuendesha biashara?
3.
Una elimu na ujuzi gani ambavyo vitakusaidia kuendesha biashara hii?
4.
Unaweza kupata wapi ushauri na taarifa kuhusu biashara hii?
5.
Unajuaje kuwa biashara hii inahitajika katika eneo lako?
6.
Wateja wa biashara yako watakuwa ni akina nani?
7.
Je, watakuwepo wateja wa kutosha?
8.
Je, wateja wataweza kudumu kununua bidhaa au huduma?
9.
Je, hii itakuwa ndio biashara pekee katika eneo lako?
10.
Kama kunabiashara zinazofanana na hiyo utawezaje kushindana na wengine
bila kushindwa?
11.
Utawezaje kuuza idadi kubwa ya bidhaa bora na huduma wanazohitaji
wateja?
12.
Kwa nini unafikiri biashara hii itakuletea faida?
13.
Je, biashara hii inahitaji vifaa, jengo au wafanyakazi wenye sifa?
14.
Je, unafikiri unaweza kupata fedha kupata vitu vinavyohitajika?
15.
Utatoa wapi vifaa vya kuanzishia biashara hii?
16.
Unaweza kufikiria wewe mwenyewe kuendesha biashara hii katika kipindi
cha miaka kumi ijayo?
17.
Unadhani una sifa na uwezo wa aina gani unaokufanya wewe uweze kuendesha
biashara hii?
18.
Je, unavutiwa kiasi cha kutosha katika kuendesha biashara ya aina hii
hadi kuthubutu kutumia muda na nguvu zako ili ifanikiwe?
Kulikubali au Kulikataa Wazo Lako la Biashara
“Maana
ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiketi kwanza na kuhesabu
gharama, kwamba anavyo vya kumalizia?” (Luka 14:28). Kwa vile umepunguza
mawazo yako ya biashara kufikia matatu ambayo unadhani ndio yanayofaa zaidi,
unahitaji kupata taarifa zaidi kuhusu soko kwa ajili ya mawazo yako. Lengo lako
ni kuangalia mambo yatakayo kusaidia kukubali au kukataa wazo la biashara.
Kulikubali au kulikataa wazo la biashara zingatia njia mbili (2) zifuatazo
kuchambua mawazo yako: Utafiti katika maeneo na uchambuzi wa UMAFUTI (SWOT).
- Utafiti katika Eneo
Utafiti huu unatokana na kuzungumza na
wateja, wasambazaji na jamii inayoishi katika eneo hilo la biashara. Unaweza
ukakusanya taarifa nyingi za kufaa kuhusu mambo yanayoathiri mawazo yako ya
biashara. Ziara hizo zitachukua muda mrefu, lakini kwa kufanya utafiti wa aina
hii, tayari umekwisha anza kufanya kazi kama mfanyabiasha mwenye mafanikio na
mawasiliano unayofanya wakati wa ziara hizi, yatakuwa ya manufaa kwako
utakapoanza biashara yako.
Watu wa kuzungumza nao.
Zungumza na wateja muhimu kama vile
matajiri, wazee maskini, vijana, wanaume au wanawake. Zungumza na wasambazaji
au watoa huduma; zungumza na wazalishaji; zungumza pia na viongozi wenye hoja
wa kiserikali, wa taasisi na wa makampuni (wakiwa kama wahojiwa muhimu).
Jinsi ya kuendesha mahojiano yako.
Eleza wazo lako kwa matumaini, na eleza
kwa nini unafikiri kuwa ni biashara ambayo wateja wako wanahitaji. Andaa
karatasi kwa ajili ya kuandikia taarifa utakazozipata toka kwa mtoa taarifa.
Acha mada moja izae mada nyingine wakati wa mazungumzo. Usiulize maswali yanayohitaji majibu ya ndiyo au hapana bali uliiza maswali yaliyowazi ukitumia “nini?” “nani?” “kwa nini?” “wapi?” “lini?” “vipi?” “namna gani?”.
Usiogope kuuliza swali baada ya swali; uliza
swali moja moja. Jitahidi kusrudia maelezo watu wanayokueleza kuhakikisha
umeelewa walichosema.
- Uchambuzi wa UMAFUTI (Swot Analysis).
Njia nyingine ambayo watu wengi wanaitumia
kuchagua wazo la biashara linalofaa zaidi ni uchambuzi wa UMAFUTI (SWOT).
Uchambuzi huu husaidia kuona maeneo yanayoweza kuwa na matatizo na faida kwa
kila wazo. Angalia kirefu na maana yake kwa lugha ya Kiswahili na Kingereza:
U = Uwezo S = Strengths
MA = Mapungufu/madhaifu au W= Weaknesses
FU = Fursa O = Opportunties
TI = Tishio T= Threats
Jambo la kuzingatia, kumbuka kuwa,
uchambuzi wa UMAFUTI unategemea sana mambo yafuatayo ili kupata wazo la
biashara lililo bora na sahihi:
JA = Jamii S=
Social factors
SE = Serikali au P = Political factors
MA = Mazingira E = Environmental factors
TE = Teknolojia T= Technological factors.
Uchambuzi wa UMAFUTI Ndani ya Biashara
Zingatia kuwa ni mambo gani katika
mazingira ya ndani ya biashara unayotegemea kuianzisha yataleta faida katika na
yapi yatakayoleta hasara. Kuchambua uwezo na udhaifu wa wazo la biashara
unaangalia katika biashara iliyokusudiwa kwa kuzingztia mambo yafuatayo:
Uwezo: Uwezo ni mambo muhimu yanayoleta matumaini
ambayo yataifanya biashara yako kuwa na manufaa kuliko biashara nyingine
zilizopo na washindani wengine. Inawezakuwa umependekeza kuuza bidhaa bora
zaidi au kuwa na mahari ambapo ni rahisi kwa wateja kufika.
Mapungufu: Ni mambo ambayo biashara yako itashindwa
kuyamudu. Pengine bei ya bidhaa zako itakuwa kubwa kwa sababu biashara yako ipo
mbali na wasambazaji na itakubidi ulipie zaidi kwa ajili ya usafiri au gharama
za ushururu, leseni na pango.
Uchambuzi wa UMAFUTI Nje ya Biashara
Kuchambua fursa na tishio la biashara
uliyodhamiria kuianzisha, yakupasa uangalie nje ya biashara; yaani mazingira ya
nje. Zingatia kuwa ni mambo gani katika mazingira ya nje yataleta faida na yapi
yatakayoleta hasara katika biashara hasa katika vipengele vifuatavyo:
Fursa: Fursa ni maendeleo muhimu yanayotokea katika
sehemu yako. Inawezekana kuwa, mahitaji ya bidhaa unayokusudia kuitengeneza
yataongezeka kwa sababu ya vyuo vingi kuongezeka au kumiminika kwa watalii.
Tishio: Tishio ni mambo yanayoweza kuleta athari
mbaya katika biashara yako. Kwa mfano wazo la biashara linaweza likawa rahisi
mno kiasi kwamba watu wengine wakaanzisha biashara kama hiyo katika eneo lako
na kukupunguzia soko maana wateja kwa idadi ni wale wale.
Zingatia: Baada ya uchambuzi wa UMAFUTI katika wazo lako la biashara, jiulize
maswali yafuatayo na kujibu ndio au hapana: Je, uwezo ni mwing kuliko
mapungufu? Je, kunafursa nyingi kuliko tishio. Kama kunamapungufu, basi ni
vyema kujua ni jinsi gani ya kuyashughulikia mapungufu hayo.
Ufupisho wa Wazo la Biashara
Baada ya kumaliza hatua ya kujitayarisha
kuanzisha wazo lako la biashara, sasa unaweza kufanya ufupisho wa wazo lako la
biashara kwa kuandaa muhtasari kwa kufuata vipengele vifuatavyo:
1.
Wazo langu la Biashara …………………… (Jumla au
rejareja).
2.
Aina ya biashara ……………….… (Biashara ya
uzalishaji au utoaji huduma).
3.
Bidhaa au huduma yangu itakuwa
………………………….…………..…………….
4.
Wateja wangu watakuwa
………………………………………..……………..………
5.
Mahitaji ya wateja yatakayotimizwa ni
………………….………….……………….
6.
Ujuzi na uzoefu wa elimu niliyonayo katika
aina ya biashara ni ………………….
7.
Nimechukua wazo hili la biashara kwa sababu
……….…………………………….
Mashaka Juu ya Wazo la Biashara
Kama unamashaka na huna uhakika juu ya
wazo lako la biashara litakalokufaa, yakupasa uchague ni jambo gani litakufanya
usiwe na uhakika: Je, ni kuhusu uchaguzi huna uhakika kama unafaa kuanzisha
biashara? Je ni kwa sababu tu hufurahii mawazo yako matatu ya biashara
uliyochagua?
Endapo utabaini ya kuwa, huna ujuzi, uwezo wala ufahamu juu ya kufanya
biashara yako mwenyewe fanya yafuatayo ili kuboresha sifa na uwezo wako (kutoka
kwenye udhaifu kwenda kwenye uhodari):
Zungumza na watu walio katika biashara ya aina hiyo ili ujifunze kutoka
kwao, pata mafunzo ya muda mfupi kwa kusoma masomo maalumu juu ya biashara
hiyo.
Aidha, tafuta kazi kama msaidizi au
mwanafunzi wa mtu aliyefanikiwa katika biashara hiyo, soma vitabu na vyanzo
mbalimbali vitakavyokusaidia kuongeza ujuzi wako katika biashara hiyo, fikiria
na changanua kuhusu matatizo ya biashara hiyo na njia zake za kutatua matatizo
hayo ili kujidhatiti na kuiepuka hofu ya kuthubutu katika kuianzisha biashara.
Zaidi na zaidi, ili kuboresha uwezo
(ujuzi) juu ya biashara yako unayotarajia kuianzisha, fanya na zingatia
yafuatayo: fanya mazoezi ya kujadili faida na hasara ya wazo lako la biashara,
ongeza msukumo wako kwa kutengeneza mpango mkakati wa baadaye, wasome na
kuwafuatilia kwa makini wafanyabiashara waliofanikiwa, elewa kuwa mafanikio
yako yanategemea sana juhudi zako mwenyewe na msaada wa Mungu pekee, Jenga
uwezo wa kuangalia na kukadiria tatizo na jaribu kubahatisha, fikiria na
jifunze jinsi ya kufanya vizuri katika kubabiliana na hali ya matatizo.
Zungumza na familia yako kuhusu matatizo
ya kuendesha biashara yako na washawishi wakusaidie, uwe wazi zaidi na kukubali
mawazo mapya na maoni ya watu wengine, wakati mambo yanapokwenda vibaya
chunguza chanzo cha tatizo na boresha uwezo wako wa kujifunza kutokana na
makosa na ongeza juhudi yako katika kufanya kazi na tambua kuwa kufanya kazi
kwa bidii ndiko kunakoleta mafanikio.
Fahamu ya kuwa, watu wengi hawafai kuwa na biashara zao wenyewe na wapo
watu wanazo sifa nyingi za kufanya biashara zao na wanaweza kufanikiwa. Kama
wewe ni dhaifu, tafuta mshiriki mwenza anayekamilisha uwezo, badala ya kuanza
biashara peke yako na ukaikomeshea njiani au kupata hasara.
Kuchunguza Uwezo na Uzoefu
Uzoefu huja kwa kutenda mwenyewe; “Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli
zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe …….” (1Wathesalonike 4:11). Kabla hujaanza kutekeleza wazo lako la
biashara, angalia na zingatia mambo yafuatayo: uzoefu wako wa kazi, uwezo wa
kiufundi, utendaji kazi katika biashara, ushirikiano na watu, historia ya
familia utokayo na uliyonayo, mvuto na mambo unayopenda, shughuli unazofanya
nyumbani kwako nje na bishara, kazi ya kuajiliwa au kujiajili.
Aina ya Biashara Uitakayo
Kuna aina kuu nne (4) za
biashara: uuzaji wa rejareja, uuzaji wa jumla, uzalishaji na utoaji huduma.
Lazima ujiulize kuwa, je, ni aina gani ya biashara unaipenda na unaweza
ukaimudu kutokana na wazo au mawazo ya bishara uliyonayo? Hivyo, ni lazima kuwe
na sababu za msingi za kuipenda au kuichagua aina hiyo ya biashara ukusudiayo
kuifanya.
B: Njozi, Tunu na Malengo Katika Biashara.
Katika mafanikio na maendeleo yo yote ya
biashara ni lazima kuwepo hitaji la vitu vine, ambavyo ni vya muhimu sana kwa
mfanya biashara ye yote, ambavyo husimama kama daraja na msingi wa mafanikio na
maendeleo ya biashara. Vitu hivyo vinne ni pamoja na:
a)
Njozi au ndoto
b)
Mkakati au mikakati
c)
Thamani au tunu
d)
Malengo.
Njozi au Ndoto
Ni picha pana ambayo mfanya biashara
(mjasiliamali) hutegemea kuwa katika mafanikio yake ya biashara. Ni hitaji la
baadae ambalo linaongoza maisha ya sasa (yaliyopo) ya mtu, biashara au taasisi
kama inavyohitajika kuwa hapo baadae kwa miaka kadhaa ijayo.
Njozi inapatika kutoka katika tunu au
thamani ya mtu, biashara, kampuni au tasisi inavyotaka kuwa. Mala zote thamani
au tunu zinapatikana kutokana na hisia za mtu mwenyewe kuhusu au biashara
inavyotakiwa iwe hapo baadae.
Mikakati au
Mkakati
Ni mbinu au harakati juu ya jambo au kitu
kinachotegemewa kutimizwa katika ndoto. Mkakati unaundwa na lengo moja au
zaidi.
Malengo
Ili kupima maendeleo ya biashara, ni
muhimu kuwa na malengo uliyopanga awari.
Malengo husadia kufahamu ni kwa kiasi gani biashara yako imefanikiwa.
Sifa ya Malengo ni lazima: yawe maalumu, yawe yenye kupimika, yaweze kufikirika
au kupatikana, yawe katika muda maalumu na yaweze kutekelezeka kirahisi.
Jinsi ya Kupata Fursa katika Biashara
Ili kuzipata fursa za biashara yako ukiwa
kama mfanyabiashara au mjasiliamali, zingatia na fuata yafuatayo: panua wigo wa
kufahamiana na watu, kuwa msomaji wa vyanzo mbali mbali vya habari, angalia
hitaji la watu au wateja wa hiyo biashaya, kuwa mwanafunzi wa mazingira kila
wakati ukijifunza na kuyasoma mazingira ya biashara yako, hudhuria maonesho na
semina mbalimbali za biashara na ujasiriamali, Jitazame, je, wewe unanini ndani
yako (uwezo wako), fuatilia matangazo na mabandiko ya kijamii na kiuchumi ili
kujua mambo mapya katika ulimwengu wa kibiashara.
Vyanzo vya Mtaji
Wengi hushindwa kuanzisha biashara kwa
sababu tu hawana mtaji wa kuwekeza katika biashara. Ili kutafuta mtaji waweza
anzia hatua ndogo kabisa kisha kuyafikia malengo ya kuanzisha biashara
unayoitaka. Vyanzo vya mtaji wa biashara ni kama: rasilimali zako mwenyewe
ulizo nazo waweza ziuza au kuzitumia kama mtaji, mkopo binafsi (kutoka kwa watu
wa karibu), kufanya kazi kwa kuajiliwa au kama kibarua, program za maendeleo ya
kibiashara na misaada ya kijamii iliyokusudiwa kuwawezesha wafanya biashara. “Alimaye shamba lake atakuwa na chakula
tele; Bali afuataye mambo ya upuuzi hana ufahamu” (Mithali 12:11)
Vikwazo na Mafanikio Katika Kukua Kwa
Biashara
Biashara yo yote haikosi kukumbwa na
changamoto kadha wa kadha, maana biashara ili iendelee kukua kupitia hatua
kadhaa. Zifuatazo ni baadhi ya
changamoto zinzoweza kukwamisha biashara yako isiendelee au kukua: miundo mbinu mibovu ya kiuchukuzi na
usafirishaji, ufahamu mdogo wa kibiashara, kutolifahamu soko na wateja wake,
uhaba wa taarifa na vyanzo vya fursa, kukosekana kwa vyanzo vya ziada vya
fedha, uhaba wa mtaji, kukosekana aina bora ya wafanyakazi katika biashara na
kuwepo ushindani mkali juu ya aina hiyo ya biashara.
Ili mfanyabiashara (mjasiliamali)
afanikiwe, anahitaji mbinu zifuatazo: kutunza na kujali muda, kauli nzuri na
kumjali mteja, uaminifu na uvumilivu, kununua na kuuza bidhaa halali na bora,
kuwa mtafiti wa biashara (juu ya manunuzi, bei na masoko), kubana matumizi;
usafi katika eneo la biashara, usafi binafsi na usafi wa bidhaa na huduma; kuwa
na leseni na kulipa kodi ya mapato, Awe na vyanzo vya pesa na kuweka akiba yake
benki. Kuweka akiba benki humsaidia mfanyabiashara kuweka pesa wa ajiri ya
matumizi ya baadae, kuweza kupata mikopo ya kibiashara kirahisi na kuepuka
upotevu na matumizi mabaya ya pesa yasiyo na tija.
Utunzaji wa Kumbukumbu
Suala la msingi katika biashara, ni kuweka
kumbukumbu ili mali isipotee bila kujua. Kuna namna nyingi ya kutunza kumbukumbu
kwa mifumo tofauti tofauti. Kumbukumbu za biashara zinaweza zikatunzwa
kielektroniki, fomu maalumu zilizoandaliwa na kuwekwa katika mafaili pamoja na
madaftari. Yafuatayo ni aina ya madaftari ya kutunzia kumbukumbu: daftari la
matumizi, daftari la mauzo, daftari la stoo, daftari la wadaiwa, daftari la
manunuzi, daftari la matumizi binafsi (yasiyo ya kibiashara), daftari la
kibiashara na daftari la hasara ya biashara.
Zingatia: Wanandoa na wanafamilia yawapasa kutambua
kuwa, katika jitihada zote za kutafuta mafanikio, Mungu apewe nafasi ya kwanza
kwa ajili ya wokovu wa maisha yao, maana imeandikwa kuwa, “….utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote
mtazidishiwa (Mathayo 6:33).
Comments
Post a Comment
Thanks for viewing and passing through NMEE blog. Keep following the blog