Posts

CHANGAMOTO KATIKA TASISI

FUNGU: Mwanzo 16:6; Naye Abram akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake. 1.0 UTANGULIZI: Nawasalimu katika jina la Bwana wetu Kristo; Bwana Yesu Asifiwe binti na wana za Mungu. kwan Somo la leo linatoka katika kitabu cha Mwanzo 16:1-15 , na Mwanzo 21:1-21 . Mada itajikita katika tasisi iitwayo familia. Swali: Kwa nini familia iitwe tasisi? Tusome kwanza Mwanzo 16:1-15 , na Mwanzo 21:1-21 kisha tuanze somo. 2.0. KIINI CHA SOMO: Aya zote tulizosoma zinamhusu familia ya Abram ambaye ni Ibrahimu pamoja na mkewe Sarai ambaye ni Sara. Familia ya Ibrahimu na Sarai ilikuwa na mjakazi (mfanyakazi au dada wa kazi) aitwaye Hajiri mwenye asili ya Misiri. Familia hii ya Abram na Sarai haikuwa na mtoto, toka wameoana. Kadri miaka iliposonga, Serai akamshauri Abram mumewe azae na kijakazi aitwaye Hajiri (Mwanzo 16:2-4).   Hajiri alijifungua mtoto wa kiume aliyeitwa Ishimael

TAMTHILIYA YA KWELI

FungU: Ayubu 42:10 “Kisha BWANA akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; BWANA naye akampa Auyubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza”. 01: UTANGULIZI Hapa duniani zipo tamthiliya lukuki zilizoandaliwa na wanadamu kwa njia za maigizo katika majukwaa ya sanaa; maandishi katika vitabu, majarida na magazeti; sauti katia redio na katika sinema. Tamthilia hizo kwa sehemu kubwa zina sifa za kufanana kimuundo wake na zinatofautiana kimtindo (yaani namna ilivyowasilishwa tamthiliya hiyo). Muundo wa tamthiliya hizi unasifa kuu nne: 1.      Tamthiliya ya aina yoyote lazima iwe na majibishano (yaani daiolojia) 2.      Tamthiliya lazima iwe na wahusika ( wahusika wakuu (aweza kuwa nguli), wahusika wadogo (bapa au mviringo), pamoja na mtoa maelezo au mfafanuzi (maranyingi huwa ni sauti). 3.      Tamthiliya lazima iwe katika muundo wa pembe tatu, japo si tamthiliya zote (yaani socretic plays): Mwanzo (maisha mazuri na kuibuka kwa mgogoro); Kilele

NGUVU YA MSAMAHA

Katika injili ya Marko 11:25-26 kusameheana kumesisitizwa kama ifuatavyo: 25 ”Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili Baba yenu aliyembinguni awasamehe na ninyi makosa yenu. 26” Lakini kama ninyi hamsamehi, wala Baba yenu aliye Mbinguni hatawasemehe ninyi makosa yenu” Kwa Nini ni Muhimu Kusamehe? Zipo sababu nyingi za kusamehe, zifuatazo ni miongoni mwazo: 1.       Kusamehe ni tabia ya Mungu, na wamchao: Mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu ( Mwanzo 1:26 ). Mwanadamu amchae Mungu kwa kweli yote, lazima awe na tabia ya Mungu kwa maana Mungu ni kielelezo cha kwanza cha kusamehe kwa mwanadamu ( Isaya 43:25. Isaya 1:18, 1Yohana 1:9). 2.       Kusamehe ni hali ya Upendo: Kama tunda la roho ni upendo vivyo hivyo kusamehe ni tunda la upendo ( 1Wakorintho 13:4-7 ) . Tabia ya mtu amchae Mungu ni upendo kwa wengine hata kama atakwazwa. Mungu ni pendo, hata mwanadamu pia yampasa awe na upendo utokanao na Mungu. Kusamehe ni ishara na kielelezo

MAISHA NA TABIA YA TAI CHACHU NA SOMO KWA MAISHA KWA MWANADAMU

Utangulizi Kila kiumbe kilichopo duniani hapa cha weza kuwa fundisho zuri au baya katika maisha yetu kulingana na jinsi kilivyotumika katika lugha ya picha. Wanyama kama Sungura na Tumbili; ni wanyama wanaowakiliaha wanadamu wenye tabia za ujanjaujanja au wajuaji sana. Simba anasimama kwa niaba ya watu nguli, wababe na wakali wenye uwezo na mamlaka. Fisi anasimama kwa niaba ya watu warafi. Twiga kwa watu wenye malingo na mikogo. Njiwa anasima kwa niaba ya utaktaifu, upendo, uaminifu na upole kwa watu. Nyoka anasimama kwa niaba ya watu wenye tabia ya uongo; wachonganishi. Ndege aina ya kasuku kusimama kwa watu wenye kuongea sana. Wasifu au Sifa Na Tabia Za Tai Wanyama na viumbe mbalimbali wanapotumiwa katika lugha ya picha hutoa na huashiria tabia na mienendo ya maisha ya kila mwanadamu. Kwa sehemu kubwa nitazungumzia katika ‘wasifu na mwisha ya ndege Tai’ kama chachu na somo kwa mwanadau. Ndege tai yupo katika aina au makundi yanayozidi 55. Katika kufuatilia taarifa na m