TAJI ZA WASHINDI.


Wimbo # 58: Zitakuwa nyota taijini
Fung kuu: 2Timotheo 4:7-8 7Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; 8Baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake”
                                                                                                                                                UTANGULIZI                                                                                                                                                                                                                                                                        Dunia imejaa mashindano kila kona ya nyanja zote za maisha. Kama mashindano ya: mbio za magari, riadha, farasi, ng’ombe, kuku, kuvuta kamba au mashindano ya ubingwa wa kula upesi, urembo, mpira, ngumi, Mieleka, kucheza mziki, au kuogelea. Mashindano yote hayo ni kutafuta sifa ya kuvikwa taji ya ushindi. Taji hizi zaweza kuwa katika mtindo wa medal za dhahabu au shaba au fedha, tuzo za vyeti, mkanda pamoja na kitita cha pesa! Vyote hivyo ni taji kwa aina zake, haijalishi kuwa ni taji itokanayo na kitita cha fedha au la!
Taji ni utambulisho wa juu kupita yote katika ulimwengu wetu huu. Taji ni alama ya kutambua jitihada za mtu anayepewa taji kama pongezi au stahili/stahiki kwa jambo fulani au mchango wake! Ukipitia historia za watu kadhaa mashuhuri ulimwenguni ambao taji zao zinaheshimika sana ulimwenguni. Mfano; Tuzo ya Nobel Prize ya Martin Luther Jr, Marcom X inahusisha wale wote walioshinda vita vya kupinga ubaguzi wa rangi.
Mambo ya Taji za ushindi chanzo chake ni Mbinguni. Paulo anazungumza na kijana Timotheo kuwa akaze mwendo katika huduma yake ya kichungaji, maana pia Wagiriki (Wayunani) ni watu ambao walikuwa na mashindano mengi kama vile ngoma, riadha, watoahoja za nguvu (falsafa), n.k. hivyo Paulo anapoeleza kwa Timotheo aliyaelewa mazingira ya Wakorintho vyema kuwa wataelewa lugha hii. (2TIMOTHEO 4:7-8) 
Kwa mujibu wa Paulo; Taji ni kwa wote ambao wanapenda mafunuo ya Mungu, na wamekubali kuisikia Sauti ya Mungu katika maagizo yake yote. Wenye sifa ya kupokea taji ya Ushindi, Paulo anataja mambo yaliyowastahilishi kupokea taji kuwa ni Kuhubiri Injili (SOMA 2TIMOTHEO 4:1-6).
JE, NI WAPI WALIO NA SIFA ZA KUPATA TAJI ZA USHINDI? 
1. Wanaoihubiri na kuishindania injili (WAFILIPI 4:3 “Naam, nataka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa maana waliishindania Injili pamoja nami, na Klementi naye, na wale wengine  waliotenda kazi pamoja nami, ambayo majina yao yamo katika kitabu cha uzima”). 
2. Waliosonga mbele bila kukata-tama, kwa kujua majukumu, wajibu na mamlaka waliyopewa na Kristo. (MATHAYO 28:18-20).
3. Watakao beba neno la AMANI kwa watu waliokata tamaaa na wasio na matumaini. (SOMA ISAYA 52:7).
4. Wanaoelewa uthamani wataji ya ushindi (SOMA 2 TIMOTHEO 4:9-18).

TOFAUTI TA TAJI YA ZA KIDUNIA NA KIMBINGU                               
Taji za kidunia hazina nyota; bali taji ya mbinguni LAZIMA iwe na NYOTA. MBINGUNI HAKUNA TAJI BILA NYOTA.
Nyota ni nini???  (Nyota ni roho za watu:) 
1. MITHALI 11:30 Mazao ya wenye haki ni mti wa uzima; Mwenye hekima huvuta roho za wtu”
2.DANIELI 12:3 “Na walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga, na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota mile na milele”.
 3. Ellen White katika MATUKIO Uk. 257, 258, & 269 anasema hivi: “Wale 144,000 walisimama juu ya bahari ya kioo katika mraba kamili. Baadhi yao walikuwa na taji zilizong’aa sana, wengine hazikung’aa sana. Baadhi ya taji zilionekana nzito kwa sababu ya nyota, wakati nyingi zilikuwa na nyota chache. Wote waliridhika kabisa na taji zao. Taji ya uzima itakuwa angavu au iliyofifia, itametameta kwa nyota nyingi au iangazwe na vito vichache kulingana na jinsi mambo yetu yalivyotendeka. Mbinguni hakutakuwa na mtu yeyote aliyeokolewa mwenye taji isiyokuwa na nyota. Ikiwa utaingia, kutakuwa na roho fulani katika makazi ya utukufu ambaye atakuwa amepata fursa ya kuingia pale kupitia kwako.” …… “Wakati waliokombolewa watakaposimama mbele za Mungu, roho za thamani wataitikia kwa majina yao ambao wapo pale kwa sababu ya juhudi ya uaminifu wako, uvumilivu, nguvu zilizowashughulikia, maombi, ushawishi uliotolewa kwao ili wakimbilie ngome. Hivyo wale ambao katika ulimwengu huu wamekuwa wafanya kazi pamoja na Mungu watapokea thawabu yao. 8T 196, 197. Wakati malango ya lile jiji zuri lililoko mbinguni yatakapofunguliwa na kugeuka katika bawaba zake zinazomeremeta, na mataifa yale ambayo yameshika kweli yataingia ndani yake, taji za utukufu zitawekwa juu ya vichwa vyao, na wao watamtolea Mungu sifa, na utukufu mkuu. Na katika wakati huo, baadhi watakuja kwako na watasema, ‘Kama isingekuwa ni kwa sababu ya maneno (ya hekima ) uliyonizungumzia katika wema wako, na kama isingekuwa kwa sababu ya machozi yako na maombi yako na juhudi zako za uaminifu, kamwe nisingaliweza kumwona Mfalme katika uzuri wake.”
4. Wimbo wetu wa ibada

HITIMISHO                                                                                                                                          Yaweza kuwa tusiweze kuuona ufalme kwa kuwa tu hatukupeleka mtu yeyote pale juu mbinguni, maana tutahesabika kuwa hatukuleta wokovu wowote duniani. Yesu anakuja kumvika taji ya ushindi kila aliyeshinda vita.                                                                                                                                                         
Swali ni nani atakaye nifanya niweze kupata nyota pale? Tazama hili wote watakaoingia mbinguni kwa juhudi zangu sio wale waliongoka kisha wakatoka – lazima ile roho iwepo pale! Kama salama yangu ni kufanya kazi kwa juhudi na kuleta wengi kwa kadri iwezekanavyo maana sijui ni ipi itaingia pale! 

MHUBIRI 11:4-6 4Mwenye kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna. 5Kama vile vile wewe usipojua njia ya upepo ni ipi, wala jinsi mifupa ikuavyo tumboni mwake mjamzito; kadhalika huijui kazi ya Mungu, afanyaye mambo yote. 6Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiuzuie mkono wako”

Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU