UWEZO WA KWENDA MBALI KULIKO WENGINE


Urefu na ubali awapo tai, huwezi kuona aina nyingine ya ndege. Zaidi ya futi 10, 000 kwenda juu angani kutoka kwenye uso wa dunia ni urefu mkubwa sana ambapo ndege wengine hawawezi kuumudu kulingana na changamoto za misukosuko, upepo mkali, mvua, baridi kali sana, kukokasa uwezo wa kuona chini, maana ni juu sana. Kwa hiyo maisha ya tai ni ya kusitajabisha sana, kwani yeye huwa juu zaidi ya ndege wengine wote. Lakini hata awapo juu zaidi hapotezi uwezo wake wa kuona mbali.


Fudisho Tulipatalo Katika maisha yetu:
Kuna msemo unasema kuwa “ndege wenye tabia na manyoya ya rangi ya aina moja hupaa pamoja”. Ukanda wa juu alipo tai huwezi kukutana na ndege wengine zaidi ya tai pekee. Kwa mtu aliyemakini lazima afanye, afikiri na atende zaidi ya pale wengine walipofikia. Kufuata mkumbo na kuiga mienendo, tabia, jinsi ya kutenda, kufikiri na kuiga maisha ya watu wengi, hakuwezi kukuletea tofauti yoyote zaidi ya kuishi kwa mkumbo.  Jua kuwa kila mtu ni wa pekee kwa jinsi ya ajabu alivyoumbwa. Kuepuka mkumbo na kunakili maisha na mienendo yaw engine; yatupasa kuwa tofauti au zaidi ya wawazavyo, waishivyo, wafikiriavyo na watendavyo. Kama tai jinzi walivyo wa pekee katika ndege wengine; na sisi tuwe wa pekee kwa kila namna.


Kama alivyo tai katika kuumbwa na Mungu; pia binadamu anamjumuiko wa maajabu na vipawa na vipaji vingi ambapo Mungu kampatia kwa jinsi ya ajabu na kustaajabisha. Binadamu yeyote akitulia vyema katika kufikiri, anaweza kufanya mambo makubwa katika maisha yake endapo atakubali kutumia uwezo mkubwa na vipaji alivyopewa na Mungu. Mungu kampa mwanadamu akili na uwezo mkubwa kuliko viumbe vyote alivyoviumba. Kutojitambua kwa mwanadamu ndicho kikwazo kikubwa cha kutokuwa na upekee. 

Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU