KWA WANAWAKE WOTE WALIO KATIKA NDOA

MAFUNDISHO KUTOKA KATIKA KITABU CHA ‘MITHALI 31:11-31’ KWA WANAWAKE WOTE WALIO KATIKA NDOA
Tabia ya mwanada hujengwa au huathiriwa na mambo mawili; mosi ni nitabia aliyorithi kutoka wazazi (yaani Nature) 2.  Ni tabia aliyoipata kutokana na mazingira aliyokulia na kuishi kwayo (yaani Nuture). Tabia ya kurithi kutoka kwa wazazi yaweza athiriwa na  kubadirika kwa sababu ya mazingira anayoishi na kukuli, pamoja na jamii inayomzunguka. Hivyo basi, andiko hili linasehemu na mchango wa kuibadirisha jamii ya kinamama walio katika ndoa zao aidha, kwa muda mrefu au mfupi, na wale wanaotarajia kuingia katika tasisi hiyo ya wanandoa.
 Kwa hiyo, wanawake walio katika ndoa kunamambo ya kujifunza mengi yenye kujenga ndani ya kitabu cha tano cha Mithali za Mfalme Sulemani. Ni nukuu ya maneno ya Mfalme Lemueli; Muasia kama alivyofundishwa na mama yake ambayo Sulemani aliyaandika katika kitabu cha Mithali. Mafundisho hayo ni ya msingi kwa kiasi kikubwa kwa mwanamke aliye katika ndoa. Pitia kwa umakini ili upate mambo kadhaa ya kujifunza na yenye kujenga fikra njema na nzuri kwa ustawi wa ndoa na familia:

1.      Mwanamke katika ndoa yake, anamchango mkubwa wa kuleta mafanikio, hivyo mume yampasa kuweka imani kubwa juu ya uwezo wa mkewe katika kuleta mafanikio ya familia.  Mithali 31:11 “Moyo wa mumewe humwamini, wala hatakosa kupata mapato”
Kiasi kikubwa cha maendeleo ya familia kwa wanandoa huchochewa na mwanamke. Mwanamke ni katibu na mtendaji kazi mkuu wa familia. Mwanamke asiposimama imara katika familia, basi mambo mengi yatayumba katika familia au kwa wanandoa. Kwa dunia ya sasa, siungi hoja wala mtazamo juu ya mwanamke kuwa “goal keeper”. Dunia ya sasa ni kusaidiana katika kusukuma maendeleo na mafanikio ya familia. Maisha yamepanda na mahitaji yameongezeka katika kulea watoto na kuishi kwa ujumla.
Kunahaja ya mwanamme kumwamini mkewe kuwa anasehemu kubwa ya kuchangia maendeleo, sio kila mara atakapo kununua kitu aombe kwa mumewe pesa. Mwanamke kuwa tegemezi kwa mume kwa kila kitu, ni kuandaa janga kubwa hapo badae; maana mwanamme huyo abebaye jukumu lote la kuhudumia kunakufariki, kufukuzwa kazi, kuugua kwa muda mrefu,  au kufungwa; na hapo yaweza kuwa ndio mwisho wa watoto kusoma shule za gharama, na mambo mengine kupwaya.
Endapo mwanamke atapewa nafasi na kuaminiwa katika michakato ya kutafuta, kujishughulisha, mume aamini familia yake haitalala njaa, au kuombwa pesa mara kwa mara toka ukweni. Mwanamke mvivu, asiejishughulisha ni mzigo kwa mmewe, anakwamisha maendeleo ya familia na hafai kuwa mama wa kigwa isipokuwa kwa kukatazwa na mumewe.


2.      Mwanamke katika ndoa yake daima atende mema kwa mume wake pasipo kikomo.  Mithali 31:12 “Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake”  
Mwanamke mwenye hekima, anayemtumainia Mungu, hapaswi kumtendea mabaya mumewe siku zote za maisha ya ndoa. Si vyema kumsema vibaya mume wako, kutoa siri, mapungufu na udhaifu wa mme wako kwa watu wengine. Sio sawa kumuwazia mabaya mume wako, wala kutomthamini wala kutomjali, au kumdharau, kumsaliti na kumjibu kwa jeuli mume wako. Mtendee mema, mazuri, mume wako. Pale anapokukosea nena naye kwa adabu na hekima.
Ikitokea mume wako amekukosea, jitahidi kumsamehe na umuombee badala ya kumjengea chuki, au kumwekea kisilani na kumnunia. Epuka kuwa na hasira juu ya mume wako. Daima tambua kuwa, wewe na mume wako ni mwili mmoja, hivyo mnene, mnuwie mamoja ili kustawisha familia yenu. Upendo wako usipungue juu ya mumeo. Upendo wako udumu bila kujali muda, wakati, mazingira, sehemu na hari ya kimaisha; upendo wako juu yake utamalaki.


3.      Mwanamke katika ndoa yampasa afanye kazi zake kwa moyo na bidii. Mithali 31:13 “Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo”
Mwanamke mwenye kumtumainia BWANA, ni mwenye bidii katika kufanya kazi na kutafuta. Hufanya kazi za nyumbani na za kiuchumi kwa moyo wa bidii, na hakomi kuonesha bidii katika kutafuta, ilimladi yote hayo anatenda kwa sababu ya ustawi wa familia yake. Wakati mwingine, haina haja ya dada wa kazi kufanya sehemu ya majukumu yanayomhusu mmemeo. Mwanamke atawaliwapo na moyo wa upendo utokanao na upendo wa kimbingu, hana mawaa, kujivunga, kujiona, kujikweza katika suala la majukumu ya kifamilia, nay ale yote yanayohusu ustawi na afya ya familia yake.

4.      Mwanamke katika ndoa ni mtafutaji na ana moyo wa kujituma hata kweda maeneo ya mbali. Mithali 31:14 “afanana na merikebu za biashara; huleta chakula chake kutoka mbali”
Unajua kunawakati wmingine baba wa familia kukwama na hutingwa na majukumu kadha wa kadha, mwanamke-mwanandoa chukua sehemu ya majukumu mumeo katika kusimamia na kusaidia majukumu ya kifamila. Mathalani masuala ya shamba, miradi, kupeleka na kuona watoto shuleni au kufuatilia maendeleo ya watoto ya kishule hata kama ni mbali kiasi gani.
Jingine, mwanamke awe radhi kutembea umbali mkubwa ili kutafuta au kuvuna chakula kwa ajili ya familia yake. Wapo wanawake wanandoa, hawawezi kwenda kisimani kuchota maji, kwenda shambani kuvuna mazao, kwenda kwenye mradi kusimamia kisa pako mbali na nyumbani. Aina ya wanawake wa hivyo ni wavivu wa kutupwa na hawana moyo wa kufanya jambo ili kuhudumia na kustawisha familia yake. Wapo radhhi kulaza na kushindisha njaa familia wato kwa sababu ya umbali kiasi wa shamba, kisima, soko n.k.


5.      Mwanamke katika ndoa huamka mapema ili kupangilia na kuandaa chakula cha familia yake.  Mithali 31:15 “Tena huamka kabla haujaisha usiku; huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi sehemu zao”
Uhai wa familia upo mikononi mwa mwanamke. Katika masuala ya nini kipikwe, nini kiliwe na kwa kiasi gani na kwa wakati gani ni jukumu la kifamilia ambalo lipo chini ya mamlaka ya mwanamke.  Tena yampasa mwanamke kuamka asubuhi ya mapema kuhakikisha uhakika na upatikanaji wa chakula kwa wanafamilia wote. Haina haja ya kubagua katika utoaji wa huduma ya chakula, wote wapatiwe hata kwa wale sio wanafamilia ilimradi wapo malango mwa familia.
Hoja ya kuamka mapema asubuhi na kuandaa chakula cha familia, ni jambo la msingi kwa mwanamke katika ndoa. watoto waendapo shule waondoke wamekula (kunywa chai); baba wa familia aendapo kazini aondoke nae akiwa amekunywa chai au kula chakula. Kula kwa pamoja asubuhi kutawaepushia gharama za maisha katika kufanya mgawanyo wa pesa na matumizi. Haipo sababu ya baba, mama na watoto wa shule kutumia pesa ili kunywa chai migahawani wakati uwezekano wa mama kuamkana mapema asubuhi kuandaa chakula cha asubuhi kasha wanaoenda kazini waende na wanao enda shuleni waende.

6.      Mwanamke hutafuta mapato kwa ajili ya kuwekeza na kununua vitu, mali au miradi  itakayonyanyua uchumi wa familia yake. Mithali 31:16 “Huangalia shamba, akalinunua;  Kwa mapato yake hupanda mizabibu”
Wapo wanandoa (wanawake) wengi huwekeza pesa zao katika nguo, kula, mapambo, vipodozi na mambo mengine ya anasa. Mwanamke mwenye akili huchuma na kuweka kwa ajili ya manufaa ya badae ya watoto. Mwanamke jitahidi kubana matumizi, tumia pesa palipo na jambo la msingi. Endapo mama wa familia unapesa na inaweza kutumika kuwekeza kwenye mradi au shughuli fulai, wekeza; huwezi jua kesho inakuwaje, huo mradi uliowekeza waweza kusaidia watoto wenu au kuwainua kiuchumi.
Mwanamke mwenye kuipenda familia yake, huwekeza kwa ajili ya familia aipendayo, ili siku za usononi papatikane manufaa. Wekeza kwenye elimu ya watoto. Mwanamke uliye katika ndoa usiache kusomesha watoto utakuwa umewanyima hazina yao ya badae. Haina haja ya kutapanya pesa ovyo, wekeza kwa ajili ya maendeleo na mafanikio ya familia yako.

7.      Mwanamke ya mpasa awe shupavu na imara katika suala la kujituma na kuchapa kazi. Mithali 31:17 “Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi: Huitia mikono yake nguvu”
Mwanamke akiwa mlegevu na mtepetevu, kwa kila jambo, basi hapana asubuhi katika kufanikisha kuinyanua familia yake. Hataweza kuwajenga watoto wake katika moyo wa kupenda kazi, maana yeye hawezi kufanya hivyo. Mwanamke mwanandoa funga mkanda, kibwebwe, mshipi kiunoni kakamaza mikono ili kuikomboa familia. Mwanamke akijikomboa, amekomboa familia na taifa, hivhohivyo hata katika kujikomboa kifikra. Kwenye ndoa sio wakati wa kupiga vijembe na mashosti, huwa ni wakati wa kupambana ili kuimalisha uchumi, mafanikio na maendeleo ya familia.
Miaka ya nyuma kidogo, jamii ya wasukuma iliangalia sifa kuu ya mwanamke kuolewa ni uchapa kazi na sio sura wala uzuri wake, maana ilikuwa ni aibu familia kupata njaa hali kwamba shamba lipo na nguvu kazi ipo (bibi na bwana). Familiazilizojengwa katika uchapa kazi  zilikuwa na asilimia kubwa ya kutoka kimaisha, ndio maana anahimiza “Hapa Kazi Tu” sababu anajua msingi wa jamii ya wasukuma, anaamini na kalelewa hivyo. Sio kulima tu, kila kitu kinahitaji juhudi na moyo wauchapa kazi.

8.      Mwanamke katika familia yake, awe na akiba ya faida ya mapato yake  ili asipungukiwe.  Mithali 31:18 “Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku”
Mwanamke laziwa awe mwanauchumi, ajitahidi kuhifadhi faida iliyotokana na nguvu kazi yake. Lakini pai  yampasa afanye mahesabu mazuri kwa kile anachotaka kuwekeza (katika mali au bidhaa), kufanya na ajue kuwa kitamletea faida hapo badae na sio hasara. Taa (mtaji) yake ya idumu kuwaka ikiwa na mafuta tele. Yaani mtaji wake usidi kuongezeka kila siku bila kukata. Mwanamke mwenye fikra pevu, huwekeza kwenye mambo yaletayo faida na sio yatayo hasara.

9.      Mwanamke katika ndoa, mikono yake iwe shupavu katika kutenda na kufanya kazi. Mithali 31:19 “Hutia mikono yake katika kusokota; na mikono yake huishika pia”
Hapana kitu kizuri kama kuona maufaa na mafanikio yatokanayo na kazi ya miko yaklo. Vivyohivyo kwa mwanamke  kutia mkono katika kujenga maendeleo ya famila yake. Mwanamke atakuwa na amani, umiliki na amrijuu ya mali au mapato ya familia yake maana akili na mkono wake utakuwa umechangia kuyaleta. Mwanamke uliye na ndoa penda kujishughulisha kwa kutumia uwezo na mikono yako, kufanikisha ukuaji, ustawi, mafanikio na maendeleo ya familia yako. Usimuachie mume wako, ukaja kukosa sauti, amri na haki ya umiliki katika mali za familia yako.


10.  Mwanamke katika ndoa na familia yake, awe na moyo wa ukalimu, huruma, kutoa na kusaidia wengine (wahitaji na masikini). Mithali 31:20 “Huwakunjulia masikini mikono yake; Naam, Huwanyoshea wahitaji mikono yake”
Wanawake wengi wanaongoza kuwa na roho mbaya kwa kukosa hata tone moja la ukalimu na moyo kusaidia wengine. Huwanyanyasa na kuwasimanga wale wasio wa upande wa familia yake. Dada wakazi , kaka wa kazi, wageni n.k. huchambwa, hunyanyaswa, huonewa na huteswa na hawa mama wa familia. Hapana, mwnamke mwanandoa usifanye hivyo, mwanamke ameumbiwa roho ya huruma yenye rehema nyinngi.
Mwanamke anaemcha Mungu ni sehemu kisima cha busara na msaada wa mawazo kwa jamii na wanafamilia wanaomzunguka. Roho ya kutoa, kusaidia wahitaji na masikini pamoja na kukalimu wageni ndivyo hufungua mibaraka ya familia. Roho mbaya na ukali hukimbiza wageni katika familia, na kupelekea kufunga mibaraka kutoka kwa Baba wa Mianga. Hata kama umetokea ukulyani, roho yenye huruma ndiyo sifa kuu na tabia ya mwanamke. Mwanamke mwanandoa jenga tabia ya kuvaa viatu vya matatizo yaw engine (aweza kuwa mumeo), hurumia na kumbuka kuwaombea walio katika shida. Kufanikiwa kwako  usigeuke na kuwachapia na kuwatesea wengine mali zako.

11.  Mwamke ahakikishe usalamawa wa afya ya familia yake. Mithali 31:21 “Hawahofii theluji watu wa nyumani mwake; Maana wote wa nyumbani mwak huwavika nguo nyekundu”
Kuwavika nguo nzito wanafamilia wakati wa baridi kari, ni moja ya jambo linaloelezea kitendo na hari ya ujalifu (kujali) kwa mwanamke miongoni mwa wanafamilia wake. Ni jukumu la mwanamke kujali, kuzingatia suala la usalama wa kiafya la wanafamilia wote. Mfano kunya maji yaliyochemshwa, motto yupi amechemka kwa sababu ya homa, tiba, chanjo, na lishe kwa wanafamilia. Kwa hiyo kwa sehemu kubwa, mwanamke ndiyo mwangalizi na mfuatiliaji wa mambo mengi ya kifamilia kuliko baba wa familia. Hivyo basi uhai na usalama wa kiafya upo kwa mama wa familia hata kama kuna dada wa kazi.


12.  Mwanamke katika ndoa yake awe hodari katika ubunifu na na unadhifu katika mavazi yake. Mithali 31:22 “Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani”
Mambo ya upambaji, usafi wa nyumba, usafi wa vyombo, mpangilio wa vitu ndani, na utunzaji wa mali za ndani, sehemu kubwa ya jukumu la mama wa familia. Ubunifu wa mapambo ya ndani, mfano kusuka na kufuma vitambaa, kudalizi mashuka n.k. ni jukumu linalosimamiwa na mama wa nyumba pia.
Mama wa familia lazima ajijali katika usafi wa mwili na mavavi pia. Avae mavazi nadifu yenye kuvutia hata kama sio ya bei ya gharama kubwa, bali mpangili na usafi pekee ndio kinachomata. Kuolewa kwa mwanamke sio kuwa ndiyo kikomo cha kujiweka safi katika hali ya unadhifu. Usivae nguo zinazokushushia heshima, bali vaa nguo zinazostili mwili vyema. Usivae nguo zikupasazo kuvaa wakati mkiwa wawili; wwe na mme wako. Kuvaa nguo zisizo za heshima na za kuaibisha, ni kujiaibisha, kujidhalilisha, kujipunguzia heshima na kumdhalilisha mmeo na wanao pia.

13.  Mwanamke katika ndoa amletee na kumjengea heshima mumewe. Mithali 31:23 “Mume wake hujulikana malangano; Aketipo pamoja na wazee wa nchi”
Mke mwenye uchaji wa Mungu ni yule asiyeuaibisha ubavu wake, bali huuletea heshima kwa jamii inayomzunguka kutokana na matendo yake mema na mazuri. Sifa njema za mwanamke ni fahari kwa mume wake,  na tabia mbaya nia aibu kwa mumewe. Tabia mbaya kama usengenyaji, uchonganishi, uvivu, kiburi, matusi, majigambo, wizi, utapeli, ulevi kupita kiasi, umalaya, uasherati, utumiaji wa madawa ya kulevya kwa mwanamke, yote humchafua mumewe na aibu humjaa na asiwe na jambo la kujivuni juu ya mke wake.
Tabia njema kama ukarimu, hekima, busara, maarifa, uchapa kazi, matumizi mazuri ya lungha, heshima n.k. ni sifa kwa familia na mume wake. Mwanamke mwanandoa epuka kumuaibisha mme wako kwa mambo, mienendo na tabia mbaya na mbovu kuelezeka. Hujui tu yaweza kuwa hata hawezi kuongozana na wewe hata kukutambulisha kwa jamaa na rafiki zake kutokana na tabia mbaya.

14.  Mwanamke katika ndoa ajitahidi na yeye kujishughulisha ili asiwe mzigo na tegemezi kwa mume wake. Mithali 31:24 “Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara  mishipi”
Jambo la mwanamke kujishughulisha ili asiwe mzigo kwa jamii na mme wake, nimelizungumzia kwa kina katika aya zilizopia huko juu. Hoja ya msingi, nashauli si vyema mwanamke akawa tegemezi, japo mwanamme ananafasi ya msingi kumhudumia. Swali je, itakuwaje endapo mtafutaji atafariki, kupata ulemavu na ugonjwa wa akili wa kudumu? Fanya utafiti na wewe kw suala hilo.


15.  Mwanamke mwye hadhi Na atendae kazi Kwa nguvu, hawazi jinsi gani aishi kesho, Bali huufulahia wakati ujao maana anajiamini katika kutafuta. Mithali 31:25 “Nguvu na hadhi, ndiyo ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao”
Mwanamke mchapa kazi ana amani na matumaini juu ya kesho yake na familia yake. Kutokana na uchapa kazi, hana wasiwasi na maisha, maana anamoyo wa bidii ambapo anaamini haishi kwa kubahatisha wala hawezi kumtegeme mme wake na kukaa akiwaza juu ya kukosa na kufanikiwa kwa mmewe.mwanamke anaetegemea mafanikio ya mume wake, hanamatumaini kw a sababu uhakika wa kupata ama kukosa mkate wa familia upo juu ya kupata au kukosa kwa mme wake.
16.   Mwanamke katika ndoa ajitahidi kuwa mwema na mwenye hekima. Mithali 31:26 “Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake”
Inaaminika kuwa asilimia kubwa ya wanamke ni waongeaji sana kuliko wanaume. Kubarikiwa kuongea sana kwa mwanamke sio kigezo cha kinywa chake kukosa hema na utaratibu kunena yaliyomema. Mwanamke mwenyehekima hatumii ulimi wake vibaya ili kuleta magonvi ndani ya ndoa yake. Matusi ya ajabu na ya nguoni, lugha isiyo ya staha pamoja na majibu yasiyokuwa ya hekima na maadili yenye kuudhi si vyema ya katumiwa na mwanamke aliye katika ndoa juu ya mmewe na watoto wake.
Majibu ya ovyo, matusi maranyingi huchochea hasira kwa wale wagombanao kwa maneno. Mwanamke mwenyehekima hunyamaza kimya, na hujibu kwa ustarabu na hekima pale mumewe ajapo juu na akiwa amepandwa na hasira. Siraha kubwa ya kushusha hasira kwa mtu juu yako ni kusema nisamehe au naomba samahani. Mwanamke mwanandoa, tambua hekima haiji bila kuiomba kwa Mungu. Chanzo cha hekima ni kumcha Mungu, maana kwa Mungu ndiko kuliko na kisima cha hekima alikozitoa mfalme sulemani. Hekima zitokanazo na Mungu zitakuongoza kujua waka na maeneo ya kujibu, kunyamaza, kunyenyeke na kujishusha juu y mme wako unapokuwa umemuudhi au kashikwa hasira.

17.  Mwanamke katika ndoa fuatilia kwa ukaribu tabia na mienendo ya watu wa familia yake pamoja na kufanya kazi kwa bidii ili kuepuka kuwa mzigo au tegemezi kwa kila jambo. Mithali 31:27 “Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; wala hali chakula cha uvivu”
Mwanamke katika ndoa ndiye aliye makini katika kufuatilia kwa ukaribu mienendo na tabia za watoto pamoja na wanafamilia wote. Marazote wanaume huwa ni wavivu wa kufuatilia mienendo na tabia za watoto na wanafamilia wengine, lazima mama wa familia ujue kila kitu kasha amjulishe baba wa familia kila kitu. Mwanamke ni zaidi ya mwandishi wa habari katika uwezo wa kufuatilia vitu vingi kwa wakati mmoja, hiyo ndiyo sifa kuu ya pekee ya mwanamke, tofauti na mwanamke.
Sio kila jambo mke amfikishie mmewe, mengine yampasa kuyamaliza yeye mwenyewe, na yale ya watoto, endapo likiwa kubwa liwasilishe na kutolewa taarifa kwa baba wa familia ili asije akalaumu kwa kutokushirikishwa.  Mwanamke kufuatilia njia za watu wa familia ni jukumu lake la msingi, maana ndiyo katibu mtendaji wa familia, hivyo ni lazima awe makini.

18.  Mwanamke katika ndoa ahakikishe familia yake inamfurahia kumjivunia na kumsifia kwa mazuri na mema. Mithali 31:28 “Wanawe huondoka na humwita heri; Mumewe nae humsifu…”
“Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni”. Sifa njema ya mama wa familia ni Yule mwenye uwezo wa kuiunganisha familia katika upendo, umoja, mshikamano, furaha na amani. Mama mwenye kuonya, kushauri, kukemea na kufundisha kwa lugha ya upole na upendo. Kwa mazuri yote ayatendayo kwa mumewe na watoto wake hakika hawana budi kujivunia, kumfurahia, kumpenda na kumsifia.
Mama wa familia apendae magomvi na hatangulizi upendo kama ngao ya kuleta amani katika familia, hawezi akasifiwa na mumewe wala watoto, maana yeye kukicha kila siku ni magonvi kwa kukuza mambo hata kama sio makubwa. Mwanamke amchae Mungu na mwenye hekima, hutumia upendo kama siraha ya kurejesha amani, umoja na mshikamano katika familia yake.

19.  Mwanamke katika ndoa awe mfano wa kuigwa kutokana na mazuri yake. Mithali 31:29 [Mumu humsifu  na kusema] “Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote
Mwamke mwenye kujua majukumu na kuisimamia familia yake, jina lake kutajwa na kutamkwa kwa mema na mazuri, kuanzia ngazi ya family na jamii inayomzunguka. Mazuri yake watu wa jamii imzungukayo imtolee mfano wa kuigwa na barua njema kwa wengine. Mwanamke mwenyekutenda mema na mazuri, mume wake hujivunia, hana budi kumsifiwa maana jina lake jema lasomeka vyema kwa watu.
Kama mama wa familia hasomeki vizuri katika mienendo na tabia yake, hawezi akarisisha mambo mazuri kwa binti zake, hivyo basi binti zake waweza kukaa bila kuchumbiwa au kuolewa, maanatabia ya mama yao sio nzuri. Sifa mbaya haiuziki hata kwa kuitembeza.

20.   Mwanamke katika ndoa; wanafamilia na jamii imsifie kwa ucha Mungu na sio uzuri wake. Mithali 31:30 “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchae BWANA, ndiye atakayesifiwa”
Wanawake wengi walio katika ndoa huwa na mikoko, ujivuni, kujisikia na kujiona eti kwa sababu ni wazuri wa sura na umbo, hivyo hawezi kuheshi, kumnyekea mumewe. Marazote uzuri wa sura hudanganya, hivyo huharibu tabia ya mtu. Mwanamke amtumainie na kumcha Bwana ndiye apatae sifa maana upendo na uzuri wa moyo watoka kwa Mungu.
 Maranyingi wanawake walio wazuri wa sura ndiyo wanaoongoza kwa roho mbaya na matendo mabaya pia na ndiyo waongozao kuleta migogoro na kuvunja ndoa, maana anaamini kwa uzuri wake atapata mwingine. Mama mwanandoa si vyema akatumia uzuri wake kama fimbo ya kumnyanyasa mume wake. Heri uzuri wa moyo wenyekujenga, kuliko uzuri wa sura udanganyao wenye kubomoa.

21.  Mwanamke katika ndoa hata ukimpatia mapato ya mikono yake hatabadirika kuiacha tabia yake njema. Mithali 31:31 “Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake ya msifu malangoni”
Kunawanawake katika ndoa hubadirika tabia wanapomiliki vipato vikubwa. Tabia hii imewafanya wanaume wengi kuwazuia wake zao kufanya kazi/biashara ili kujiingizia vipato vyao binafsi na hivyo kuwafanya kuwa mama wa nyumbani wakiwategemea waume zao kwa kila kitu na kila jambo. Mwanamke amchae Mungu, habadiriki tabia, habadiriki katika kiwango cha upendo eti kwa sababu ya mali, kazi, elimu au chochote kinachompatia kipato.
Upendo wa kweli na tabia njema ya mwanamke kwa mume wake haujalishi kiasi gani cha pesa au mali alizonazo. Hivyo basi, mwanamke mwenye upendo wa kweli na tabia isiyobadirika kwa sababu ya pesa, mumewe hawezi kujizuia kumpatia mali, hwala kumzuia kuchakalika katika utafutaji wa kipato chake binafsi. Si salama mwanamke akamsaliti mume wake kwa sababu au tamaa ya pesa.

NB: Andiko hili ni sehemu ya kitabu changu ninacho tarajia kukitoa, hivyo mchango wako wa kunikosoa na kunijenga unahitajika isipokuwa lugha ya matusi pekee. Bado sijafanya editing, najua kuna typhos nyingi
Mwl. Frank Philemon © 2016


Comments

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU