MAMBO YA KUTAMBUA (‘A’ TO ‘Z’) KWA MCHUMBA ANAYETAKIWA KUWA Mwenzi wa maisha

MAMBO YA KUTAMBUA (‘A’ TO ‘Z’) KWA MCHUMBA ANAYETAKIWA KUWA Mwenzi wa maisha

Kumekuwapo na changamoto nyingi sana za ndoa na hizo changamoto zimesababishwa na kufanya makosa kwa wanandoa katika suala zima la uchaguzi wa wenzi au wachumba wao katika hatua ya uchumba kabla ya ndoa kuja. Changamoto mojawapo katika ndoa imesababishwa na mitazamo tofauti na utashi binafsi wa watu katika kuingia kwenye ndoa. Kutofahamu umuhimu wa ndoa katika wanadamu kumepelekea kuvunjika kwa ndoa nyingi sana maana wengi wao wameoana kwa kuangalia vitu, kazi, mali, sura, kipaji, mvuto, umaarufu au chochote kutoka kwa mchumba kama kigezo cha kumvuta na kuiingia katika mahusiano ya uchumba ili kuifikia hatua ya ndoa.
Ndoa (kama tasisi) ni takatifu, na Mungu aliruhusu ndoa kwa makusudi matakatifu. Ndoa ya kwanza iliasisiwa na Mungu mwenyewe katika bustani ya edeni kati ya Adamu na Hawa (mume mmoja na mke mmoja). Hivyo basi mchakato mzima wa kumpata mwenzi wa maisha kunahitaji kumshirikisha Mungu ili akupatie mtu mwenzi wa maisha wa kufanana naye. Vijana wa kike na wa kiume wanaotegemea kuingia katika ndoa wanatakiwa wajue kuwa, panahitajika umakini mkubwa sana ili kumpata mchumba na mwenzi sahihi wa ndoa.
Hivyo; ni vyema kutambua cha kuzingatia kumpata mchumba afaaye kuwa mke mwema. Mithali 2:11 inatuambia kuwa “Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi” hivyo na mimi naomba kuwapa elimu, busara ufahamu ambao vijana wa kike na wa kiume utawahifadhi kwa kufuata hatua zitakazokuwatia mchumba anayestahili kwa ajili ya ndoa njema na kuishi maisha ya ndo kwa furaha:

 ‘A’ Azima ya kuingia kwenye ndoa uitambue
Azima na nia ya kuingia kwenye ndoa yampasa mtu aitambue. Jambo la kuwa katika ndoa halikwepeki, muda ukifika wakufanya hivyo yampasa mtu kuazimia kwa dhati kabisa. Biblia inasema kwenye kitabu cha Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”. Kunuia kwa mtu na kuwa tayali kutamwandaa kisaikolojia pamoja na kujipanga kwa ajili ya azima hiyo. Kwa namna nyingine, kuingia kwenye ndoa sio suala la kuigiza wala kujaribu, bali kunahitaji kunahita azima ya kuingia kwenye ndoa.

 ‘B’ Bidii katika kazi
Mchumba anayefaa ni Yule mwenye bidii katika kazi nasiyo alichonacho, mali alizonazo, kazi aliyonayo mchumba. Mtu mwenye bidii katika kutafuta anauhakika wa kufanikiwa, hivyo mchumba huangaliwa katika kufanya kazi kwa bidii na mipango thabiti kwa ajili ya kuyatafuta mafanikio kwa nia halali. Mithali 10:4 na Mithali 12:27 mafungu haya yamesadiki juu ya bidii katika kazi. Kulingana na mfumo wetu wa elimu (miaka 16 na zaidi hutukika kwa ajili ya elimu toka chekechea hadi chuo kikuu) kumpata kija aliyefanikiwa kuwa na funguo tatu yaani nyumba, ofisi na gari ni nadra sana.

Hivyo kwa wale wanaotafuta waenzi wenye funguo tatu hasa kwa kijana ya mpasa amtafute mtu mzee, mtu aliyefiwa na mwenzi wake au kwa binti aingie katika ndoa ya mitala. Mchumba mvivu na tepetevu na asiyejibidisha hafai kuwa mke au mume kwani dunia ya sasa inahita kusaidiana katika kutafuta ili kuyafikia maendeleo mapema. Huu ni ushauli wangu mwenyewe, maana uzoefu unaonesha madhara yake. Mfano baba ambaye mtafutaji afarikipo au kupata ulemavu wa kudumu au gonjwa la kudumu, familia huyumba na kusambarati. Hili jambo lipo hata kwa upande wa wanaume, maana wapo wasiotafuta wala kujibidisha katika kutafut hivyo hulishwa na wanawake (ambapo sio salama pia).


‘C’ Chunguza Tabia
Kipengele hiki ni nyeti sana maana ndipo kiini cha mchumba anayefaa kuwa mke kinabeba mkitadha mzima wa mchumba mwema atokaye kwa Mungu. katika tabia ndipo unaweza kupata wife material (mke mwema). Wasifu wan je wa mtu kuutambua ni rahisi sana kuliko wasifu wa mtu wa ndani; vivyohivyo tabia za ndani na tabia za nje kwa mchumba. Ukikosea kuchunguza tabia ya mchumba katika kipindi cha urafiki, ni ngumu kuzibaini gtabia katika uchumba maana atazificha ili kifikia lengo la kuolewa au kuoa.

Tabia ni sawa na ngozi, kuibadirisha ni vigumu sana. Usijipe moyo kwa kusema na kufikili “ngoja anioe au nimuoe naye kasha nitambadirisha tabia yake”. Japo pia mwenye uwezo wa kumbadirisha mtu tabia ni Mungu, hivyo itahitaji maombi mengi ya dhati kwa kumuombea mchumba au mume/mke. Mafungu yaliyo katika Mithali 7:10-12, Mithali 11:16 na Mithali 12:4 yanaelezea juu ya tabia bainishi zinazofaa na zisizofaa kwa mtu anayemwabudu na kumcha Mungu wa mbinguni. Kuna aina kuu mbili za tabia kama ifuatazo:

1. Tabia zinazojipambanua kwa nje: Tabia za nje zinajipambanua katika matumizi ya ulimi katika kuongea, faasheni na aina za mavazi avaazo mtu (Mwanzo 3:7, Kumb 22:5, 1pet 3:1-6,), kujipamba kwake kwa sura au mwi na manukato (Hosea 2:13, Wimbo 1:3, Ezekiel 23:40), vyakula na vinywaji apendeleavyo(Mithali 23:20-21). Tabia zote za nje kuzibaini hazihitaji muda mrefu sana mfano uchafu au usafi wa mtu.

2. Tabia zinazojipanua kwa ndani: Tabia hizi hazionekani kwa urahisi maana ni za ndani mno; mfano wa hizo ni wivu, upole, uchoyo, kutojali, dharau, mtazamo. Warumi 3:12 imezungumzia tabia njema. Ugunduzi wa tabia hizi juu ya mtu, kunahitaji kiawango na ujuzi mzuri wa saikoloji. Kubadilika kwa tabia hizi za ndani kunahitajika uwezo wa Roho mtakatifu na utayali wa mtu baada ya kugundua udhaifu na mapungufu yake.

‘D’ Dini/Dhehebu
Dini au dhehebu katika mahusiano ni kipengele cha kuzingatia na kutilia maanani zaidi. Napendekeza kuwa, wale wanaotalajia kuwa wenzi ni vyema pakawepo ufanano wa dini au dhehebu. Kila dini na dhehebu panamafundisho yake (doctrines) ambayo yanapishana kutoka dhehebu au dini moja kwenda dhehebu au dini nyingine.  1Wakorintho 1:10 na 1Wakorintho 1:12 aya hizi zinatoa umuhimu na faida za wanandoa kuwa wenye dini au dhehebu moja, maana hawatapisha katika misingi ya mafundisho bila kuwagawanya watoto katika imani za mafundisho. Ukitaka familia iwe chini ya kiwango katika mambo ya kiroho, jaribu kuchanganya dini mbili tofaiti katika kuoana miongoni mwa wanandoa.


‘E’ Elimu
Kunaelimmu ya kweli ambayo inahusu uelewa na maarifa juu ya Mungu wa kweli wa mbinguni na elimu ya kidunia ambayo tunaipata mashuleni kupitia masomo mbalimbali. Nitazungumzia juu ya elimu ya kidunia ambayo inaweza ikaleta utofauti kwa wachumba watakapo kuwa katika maisha ya ndoa. Nashauri wachumba wanaotarajia kuoana wasipishane sana viwango vya elimu au walingane viwango vya elimu ili kuleta uwiano katika mitazamo, uelewa na tafakari.

Sanjali na viwango vya elimu kuwiana au kutotofautiana, kigezo cha elimu lazima kipewe nafasi ili kila mmoja kati ya wachumba kuridhia wao kwa wao, endapo mmoja hajui kusoma wala kuandika au hajaenda vidato katika elimu. Suala la elimu pia laweza kutatuliwa kwa wenzi kukubaliana katika kuendelezana katika masuala ya elimu. Mafungu yafuatayo yanaelezea juu ya elimu ya kweli na elimu dunia: Mithali 4:13, Waefeso 5:22 na
Esta 1:22.

‘F’ Familia atokayo (historia yake)
Suala la ufahamu wa historia na familia atokayo mchumba ni vyema kuifahamu bayana na kujiridhisha kwayo. Kuifahamu familia atokayo mchumba ni jambo jema sana, kwani litasaidia kujua endapo kunamagonjwa ya kurithi, malezi mabaya na tabia mbaya za wazazi au walezi wa mchumba ama sivyo. Mara nyingi tabia ya wazazi/mzazi hubainisha tabia ya mchumba hususani binti kama anavyoelezewa katika Ezekieli 16:44. Mafungu mengine yanayoelezea juu ya umuhimu wa kuijua historia ya familia atokayo mchumba Hosea 2:4-5 2Samweli 13:8-12. Yapo matendo yaliyofanywa na wazazi na kupelekea matokeo yake kuendelea kuandama vizazi vinavyofuata (Kutoka 20:5).

 ‘G’ Gharama kwa mchumba
Kila jambo halikosi kuwa na gharama aidha muda au pesa. Zipo gharama kwa mchumba, hivyo ni vyema (kijana wa kiume) akazitambua ili kujua endapo atazimudu ama sivyo. Pamoja na gharama nyigi; ipo gharama kubwa ambayo huwa inawakabili vija wa kiume ni lazima aipitie ili kuifikia hatua ya kumuoa mchumba aliyempata. Ghara hiyo huhusisha mahali pamoja na viambata vya zawadi na gharama mbalimbali (Mwanzo 24:48-53). Suala la mahali linapisha tamaduni na tamaduni, sehemu na sehemu, imani moja kwenda imani nyingine.

Kunawakati ghara hubebwa na wazazi, na wakati mwinine kijana badala ya wazazi aweza kuzibeba mwenyewe. Wakati mwingine gharama za mahali huwa ni kubwa mno, hivyo mchakato wa wachumba kuoana hushindikana na ndoto za kuwa wezi hukwama kwa sababu ya gharama kubwa iliyotajwa ili kumuuoa binti. Suala la mahali kuwa la gharama kubwa, limesababisha madhara makubwa katika jamii nyingi. Mfano: vijana kuoana bila kufuata taratibu, kkukatisha tama vijana kuoa au kuolewa hivyo kupata mimba na watoto nje ya ndoa.  

‘H’ Hiari ya Yule mchumba kuishi naye
Upendo wa kweli hauhitaji shuruti wala kulazimisha, bali upendo huandamana na hiari juu kuridhia toka moyoni. Hivyo, mchumba ni vyema akakubali yeye mwenyewe ili kuingia ndani ya ndoa. Uhuru katika kukubari hakuleti majuto hapo baadae ndani ya ndoa, maana mtu amefanya maamu mwenyewe. Sio salama sana kutumia ushawishi wa kipesa, mali au misaada yoyote ili kumtengenezea mazingira mchumba akubali kuolewa, kwa sababu vitu au pesa vyaweza kuwa mvuto badala ya upendo kutoka moyoni. Rushwa yenye ushawishi katika uchumba si jambo jema, maana hapo baadae kwa weza tokea upungufu au ukosefu wa upendo wa dhati ndani ya ndoo. Kunajambo zuri la kujifunza katika Mwanzo 24:54 ambapo Rebeka alihiali yeye mwenye kwenda kuunga na mume wake baada ya kutolewa zawadi na mahali.

‘I’ Imani
Suala la imani ni jambo nyeti sana sawa sawa na kile kipengele cha “D” juu umuhimu wa wachumba kufana kwa dhehebu au dini kabla ya kuoana. Yapendeza wachumba wanaotaka kuoana wawe wa imani moja, maana kutofautiana imani huzaa migogoro katika ndoa. Zipo imani ambazo huruhusu kula vyakula vyote, kuoa na kuacha (kutalakiana), kunywa pombe, kuoa wake wengi na kuvuta sigara, hivyo mwingine akiwa na masharati katika hivyo vipengele, kutaleta migogoro mikubwa ndani ya ndoa. Sambamba na hayo, hata taratibu za ibada kupisha kati ya imani moja na nyingine kwa weza sababisha makwazo miongo mwa wanandoa
Sio salama pia kutumia silaha ya kumtangazia mtu (mchumba) kuwa nitaolewa au nitakuoa wewe endapo utabadiri imani yako na kuja kwenye imani yangu; kwa sababu mchumba aweza kukubali kubadiri imani yake ili aolewe au kuoa kwa sababu ya kukidhi hitaji lake na siyo kwa kuikiri imani.  Kitabu cha 1 Wafalme 11:4 kinasema hivi: “Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa BWANA Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake.”  Ni vyema wachumba wanaotarajia kuoana wawaze mamoja, wanuie mamoja, watende mamoja, waamini mamoja katika imani ili kuondoa mpasuko.

‘J’ Julisha wazizi
Uchumba wa Yusufu na Mariam ulitambulika nyumbani kwao na jamii inayowazunguka. Wakati mwingine hata urafiki utambulike kwa wazazi ili wazazi nao wapime uaminifu wa rafiki huyo kama ilivyotoke kwa Musa (Kutoka 2:16-21).  Wachumba wanaotalajia kuoana ni vyema wakazijulisha pande zote mbili za wazi wao ili kuweka uwazi na kulinda uchumba wao ili kuepuka kusalitiana kama ambavyo wangekuwa wawili kwa uchumba wa kisiri. Huwa ni moja ya heshima kubwa sana kwa wazazi kujulishwa juu ya uchumba wa binti au kijana wao endapo amefikisha umri wa kufanya hivyo ili nao wapate ya kushauri au kutoa Baraka zao kwa ajili ya hatua zingine kuelekea katika ndoa.  


‘K’ Kasoro alizonazo mchumba zibaini mapema
Kubaini kasoro alizonazo mchumba ni vyema ni vizuri ili kujipima kama zitaweza kuvumilika au kubailishwa kama ni za kufanyiwa mabadiliko haraka kabla ya kuamua kuingia kwenye ndoa. Biblia inamzungumzia Lea kasoro yake ya kuwa na makengeza lakini Yakobo alimkubali kwa kasoro (Mwanzo 29:17). Lea huyo huyo mwenye kasoro na asiyependwa alibarikiwa kupata motto mapema kuliko Raheli. (Mwanzo 29:31). Yatupasa pia kujua kuwa hakuna mtu ambaye hakosi kasoro asilimia mia, labda awe malaika.

‘L’ Linganisha umri wenu
Kipindi cha umri wa miaka 12-21 unapenda anasa na umri wa miaka 40 na kuendelea ni umri ambao watu hutunza pesa. Umri wa miaka 18 hadi 25 kwa wanawake huwa umri wa mabadiriko makubwa ya kimaumbile, na wengi wao hunenepeana kutoka umbo la awali kwa sababu ya mabadiliko ya homoni na maumbile. Umri wa miaka 25 kuendele ndio umri sahihi wa kutambua umbo la mwanamke maana atakuwa amepitia hatua zote za mabadiriko. Jambo la msingi kutambua katika umri wanamke hukomaa kiakili mapema, kuliko wanamume; lakini pia wanamke huchakaa mapema lakini hawazeeki mapema, bali wanaume hawachakai mapema ila huzeeka mapema. Hivyo basi ni vyema mwanamke awe chini kidogo ya umri wa mwanamume kutokana na kuchakaa au kukua kwao haraha.

Ulinganifu wa kiumri ni mzuri ili kubaini umri sahihi wa kuzaa pamoja na kuweza kusimamia majukumu ya kifamilia.  Kiafya inashauliwa kuwa, mwanamke asiendelee kuzaa afikishapo umri wa miaka 34 hadi 36, hivyo ili mwanamke aweze kuzaa watoto watatu wenye kutofautiana miaka mitatu, akichelewa sana aanze kuzaa akiwa na umri wa miaka 25 hadi 26 ili ukijumlisha miaka tisa ya watoto watu atafikaka au kabla ya miaka 36. Si wote wanaowezakutendewa miujiza kama Sara kuzaa katika umri wa uzee (Mwanzo 17:17). Suala la umri kwa wanaume halina changamoto sana, bali sio vyema kulea watoto katika umri uzee, hivyo angalau akichelewa sana miaka 32 na kurudi numa.


‘M’ Miliki alizonazo mchumba zitambue
Panatakiwa ukweli na uwazi kwa wachumba juu ya mali na miliki alizonazo mchumba kila mmoja kabla ya kuoana. Kukosekana kwa uwazi wa miliki alizonazo mchumba kwa weza kusababisha kukosekana kwa uaminifu endapo siku moja atabaini kuwa ulukuwa umemficha. Kumficha mchumba juu ya miliki na mali hupelekea kuotea endapo mmoja atafariki ghafla waka wawapo katika ndo. Uwazi wa miliki utawaweka huru wachumba wote wanaotaka kuoana hapo baadae ili kurahisisha mipango ya maendeleo mapema. Wakati mwingi mali alizonazo mchumba hujulikana bila hata kumuuliza mhusika, kama ilivyo katika kisa cha kitabu cha Ruthu, ambapo Ruthu alitambua mali za Boazi kwa kumuona katika usimamizi wa hiyo miliki (Ruthu2:3-4).


‘N’ Ndoto zake mchumba za maishani maishani

Kila mwanadamu aliyenahakili timamu na mwenye uwezo wa kufikiria japo hata kido huwa hakosi kuwa na ndoto za maisha anazotalajia kuzitimiza katika kipindi cha muda fulani katika maoisha ysake. Ni vyema ndoto za wachumba zibainike kwa kila mmoja, ili waweze kuona namna na jinsi yakuweza kuzitimiza aidha ndani ya ndoa au kabla ya ndoa. Endapo ndoto ya mmojawapo miongoni mwa wachumba itahitajika kutimilizwa kwanza ndipo suala la ndoa lifuate, itabidi mwingine aheshimu na kusubiria au kama itakuwa ni vigumu kusubiri, basi huyo asiyeweza kusubiria amuache mchumba wake na awe huru kutafuta mwingine aliyetayari kuingia katika ndoa. 



NA MWL. FRANK PHILEMON


ITAENDELEA, SIKU NYINGINE

Comments

Post a Comment

Thanks for viewing and passing through NMEE blog. Keep following the blog

Popular posts from this blog

MAJINA YA WANAWAKE KATIKA BIBLIA ‘A’ HADI ‘Z’

MFANO WA MPANGO KAZI

SOMO: MADHARA YA KUKATAA KUMTII MUNGU